WanaJamiiForums nakuja kwenu kukiri maisha ni magumu, naomba mnisaidie nipate kazi

Mimi nikijana mwenye umri wa 25yrs, nimemaliza chuo mwaka jana na degree ya sheria kutoka chuo kikuu kimoja huko Arusha, Tangia nimalize chuo niliamua kuhamia dar na kujichanganya kwa vibiashara vya hapa na pale kama mnavyojua tatizo la ajira kwasasa, kweli nimejaribu sana kuuza hiki na kile km viatu, nguo, vyakula, ila kila ninachofanya nafeli mahitaji yanazidi kipato, mpaka muda huu ninavyo andika hapa ht ule mtaji kidogo nao nimelipa kodi,

Nimeuza karibia assets zote nilizonunua kipindi nipo chuo, nimebaki na kitanda na godoro tu na jiko navyo km maisha yataendelea kuwa hivi nitauza navo nirudi nyumbani tu, Sioni thamani yakusoma kabisa, najuta muda niliopoteza nisingeishi maisha mabaya km haya, Naomba mwenye connections ya kazi zifuatazo anisaidie japo nijiokoe nisiuze kitanda na godoro.

Utaniboy, Saidia fundi, kubeba zege, Viwandani, pia hata udereva naweza ingawa sina leseni ila naweza uza simu nikaipata, nisaidieni ndugu zangu, Vyeti vyote na ushahidi ninavyo. Nawashukuru sana mungu awabariki ndugu zangu.
Nenda sumbawanga Kuna "Alot of fortunes out there"
 
ukiwa na mawazo usome ili uje uajiriwe.
haya ndo matokeo yake..
Mada yake inaonesha analalamika kuwa kasoma lakini kazi HANA.
Kwa akili yake na mawazo yake alijua akimaliza chuo atapata kazi nzuri, atajenga, ataoa mke mzuri.kumbe kanuni za maisha hazipo hivyo.
Kwanza aondoe HYO DHANA MIMI NIMESOMA SINA KAZI.
Unamkosea heshima huyo mzee wa kwenye avatar yako, kijana anapambana katika kujiajiri yet unaleta kebehi, unataka aibe sasa? Hivi hivi Umomi alipotea kwa kauli kama hizi

Sent from my SM-G928F using JamiiForums mobile app
 
Shule ni mtego wa Umaskini...Wajanja wachache wameukwepa.
Na wanamaisha bora
Mkuu Da'Vinci nakuunga mkono!

Tanzania elimu kama elimu kumsaidia mtu moja kwa moja kwa wakati huu hakuna hiko kitu maana hata akipata ajira mshahara wenyewe mdogo haukidhi mahitaji kumtoa mtu kwenye umasikini,kama upo uwezekano kukikwepa hiki kipengele kwenye maisha,bora muhusika afanye hivyo mapema.

Ndiyo elimu ni muhimu sana ila tukubali tukatae kwenye maisha asili na halisi ya Mtanzania haina tena msaada,maana bora nisisome then nikutane na kiboko cha maisha sitakuwa na cha kulaumu sana ila nitakaza kiubishi kupambana na uzembe wangu ila nimepoteza miaka minne ndani ya kuta nne kisha nirudi mtaani nikidhani kuna maisha nijikute ndani ya hali hiyo....huwezi kuwa sawa kiakili utachizika na wengi mtaani wapo ktk hali hiyo ni kwa vile wanajikaza tu!!!
 
Shule ni mtego wa Umaskini...Wajanja wachache wameukwepa.
Na wanamaisha bora
Hapana watoto wa maskini tuna lack connection na bahati unafikiri angekua mtoto wa lowasa au job ndugai may be angekua afisa ubalozi Switzerland au usa, kuna dogo mmoja tulimaliza nae chuo then dingi yake alikua na connection nying serekalini wakati ss tunaangaika na interviews za tume ya ajira yy akapelekwa London school of economics kuchukua M.A baada ya miezi tisa likarudi liliniambia kwamba yy kazi alishatafutiwa tokea first year so anakamilisha vyeti tu, lipo taasisi moja inayohusiana na ukusanyaji wa mapato ana noti balaa.
 
Hapana watoto wa maskini tuna lack connection na bahati unafikiri angekua mtoto wa lowasa au job ndugai may be angekua afisa ubalozi Switzerland au usa, kuna dogo mmoja tulimaliza nae chuo then dingi yake alikua na connection nying serekalini wakati ss tunaangaika na interviews za tume ya ajira yy akapelekwa London school of economics kuchukua M.A baada ya miezi tisa likarudi liliniambia kwamba yy kazi alishatafutiwa tokea first year so anakamilisha vyeti tu, lipo taasisi moja inayohusiana na ukusanyaji wa mapato ana noti balaa.


Hahhaa..inauma...anakuambia anakamilisha tu vyeti dah
 
Pole Sana..ipo SIKU yako tu usikate tamaa..zidi Kupambana ukimtegema Mungu.
 
Hiv
hivyo vyote ni mlengwa uleule wa kuomba ajira au kujiajiri locally...nafiri kumuwekea akiba mtoto ndio akiri skills zingine atajifuanza mwenyewe ila huku akiwa na pesa ya kujifunza bila stress na kugharamia kila kinachotakiwa.

Imagine mtoto umemuandaa kwa skills za graphicsdesign, Online business nk huku akimaliza chuo anapesa yake kwa account hata 7M.
Mimi naenda mbele kidogo, pamoja na kuwa na skills hizo, na badala ya kumkabidhi pesa taslim, mtoto aandaliwe mradi wa kimkakati ambao atashirikishwa moja kwa moja kama msimamizi chini ya uangalizi wa wazazi anapokuwa likizo. baada ya masomo yake ataanzia hapo.
 
Mimi naenda mbele kidogo, pamoja na kuwa na skills hizo, na badala ya kumkabidhi pesa taslim, mtoto aandaliwe mradi wa kimkakati ambao atashirikishwa moja kwa moja kama msimamizi chini ya uangalizi wa wazazi anapokuwa likizo. baada ya masomo yake ataanzia hapo.
Nakubaliana na wewe kabisa inabidi Sasa ukiwa na mtoto uanze kumuandaa mapema kwa kumuwekea saving asome bila stress Ila pia kumfundisha ubunifu wa kutafta fursa mbalimbali za kuingiza kipato bila hivo stress zaweza ua mtoto.
 
Hapana watoto wa maskini tuna lack connection na bahati unafikiri angekua mtoto wa lowasa au job ndugai may be angekua afisa ubalozi Switzerland au usa, kuna dogo mmoja tulimaliza nae chuo then dingi yake alikua na connection nying serekalini wakati ss tunaangaika na interviews za tume ya ajira yy akapelekwa London school of economics kuchukua M.A baada ya miezi tisa likarudi liliniambia kwamba yy kazi alishatafutiwa tokea first year so anakamilisha vyeti tu, lipo taasisi moja inayohusiana na ukusanyaji wa mapato ana noti balaa.
Kweli connection ka huna unapata tabu Sana, Ila kikubwa ni kutokukata tamaa kunusa fursa mbalimbali na kujaribu mbona unatoka tu vizuri
 
Back
Top Bottom