Mimi nikijana mwenye umri wa miaka 25,
Nimemaliza chuo mwaka jana na degree ya sheria kutoka Chuo Kikuu kimoja huko Arusha, lakini tangu nimalize chuo niliamua kuhamia Dar es Salaam na kujichanganya kwa vibiashara vya hapa na pale kama mnavyojua tatizo la ajira kwa sasa, kweli nimejaribu sana kuuza hiki na kile kama viatu, nguo, vyakula, ila kila ninachofanya kinafeli mahitaji yanazidi kipato, mpaka muda huu ninavyo andika hapa hata ule mtaji kidogo nao nimelipa kodi.
Nimeuza karibia assets zote nilizonunua kipindi nipo chuo, nimebaki na kitanda na godoro tu na jiko navyo kama maisha yataendelea kuwa hivi nitauza navo nirudi nyumbani tu
Sioni thamani yakusoma kabisa, najuta muda niliopoteza nisingeishi maisha mabaya kama haya, naomba mwenye connections ya kazi zifuatazo anisaidie japo nijiokoe nisiuze kitanda na godoro.
Nawashukuru sana mungu awabariki ndugu zangu.
Nimemaliza chuo mwaka jana na degree ya sheria kutoka Chuo Kikuu kimoja huko Arusha, lakini tangu nimalize chuo niliamua kuhamia Dar es Salaam na kujichanganya kwa vibiashara vya hapa na pale kama mnavyojua tatizo la ajira kwa sasa, kweli nimejaribu sana kuuza hiki na kile kama viatu, nguo, vyakula, ila kila ninachofanya kinafeli mahitaji yanazidi kipato, mpaka muda huu ninavyo andika hapa hata ule mtaji kidogo nao nimelipa kodi.
Nimeuza karibia assets zote nilizonunua kipindi nipo chuo, nimebaki na kitanda na godoro tu na jiko navyo kama maisha yataendelea kuwa hivi nitauza navo nirudi nyumbani tu
Sioni thamani yakusoma kabisa, najuta muda niliopoteza nisingeishi maisha mabaya kama haya, naomba mwenye connections ya kazi zifuatazo anisaidie japo nijiokoe nisiuze kitanda na godoro.
- Usaidizi wa kwenye magari ya mzigo,
- Saidia fundi, kubeba zege,
- Viwandani,
- Pia hata udereva naweza ingawa sina leseni ila naweza uza simu nikaipata, nisaidieni ndugu zangu
Nawashukuru sana mungu awabariki ndugu zangu.