Wanaitwa ‘MANTIS SHRIMP’ mwenye pigo sawa na nguvu ya risasi

Wanaitwa ‘MANTIS SHRIMP’ mwenye pigo sawa na nguvu ya risasi

Thewildlife_tz

Senior Member
Joined
Apr 23, 2019
Posts
127
Reaction score
85
Wanaitwa ‘MANTIS SHRIMP’ mwenye pigo sawa na nguvu ya risasi

Hawa ni moja kati ya viumbe hatari sana wanaopatikana baharini hasa bahari ya Hindi hapa Tanzania Kitalaam wanaitwa “Stamatopoda”

Wana urefu wa cm 20 sawa na inchi 8 na uzitowao ni Gram 90 – 100 lakini mambo yao ni konki
Kwa umbo wanamagamba mazuri yenye kuvutia lakini ni moja ya viumbe hatari sana baharini

Wana uwezo wa kupiga sehemu na kuvunja na nguvu yake ni sawa na risasi, na wanauwezo wa kupasua vile vioo vya mabwawa ya kuhifadhia samaki (aquarims) kwa Single Hit)

Mantis huwa hawaishi kijamii, ni wakali sana hasa kwenye mipaka yao yaani ukiingia bahati mbaya kwenye anga zao ni lazima watakujeruhi

Huwa wanatoa sauti za chini sana ambazo huwasiliana kama ikitokea wakakutana na nadra sana kuona wanapigana

Macho yao yako kwa juu kama antena na yana uwezo mkubwa wa kuona na kujua direction ya predators au prey
pia yana uwezo wa kwenda direction tofauti tofauti yaani moja kaskazini na moja kusini, Vile vile wanakucha ambazo hutumia kumkamata prey anapokua karibu

Chakula chao kikuu ni ngadu, Samaki na baadhi ya viumbe vingine na wanakula samaki ambao huwa wakubwa kuliko hata umbo lao

Huwa wanatumia mechanism tofauti sana pale wanapotaka kutafuta chakula wanauwezo wa kupiga maji yakatengeneza mawimbi makubwa tu kuelekea direction ya prey na kabla ya prey hajafanya maamuzi anapigwa round kick kali sana..

Wanauwezo wa kugundua Mgonjwa wa cancer kwa macho yao na hii ni kwasabu macho yanauwezo mkubwa sana wakuona na kugundua movement nampangilio wa neurons (Hii ni kwa mujibu wa Chuo Kikuu cha Queensland)

Kwa kawaida huwa na life partner yaani bebi mmoja tu kwenye maisha yao na muda wa kutaga jike na dume hulalia pamoja mayai mpaka muda wa kupata watoto

Adui yao mkubwa ni binadamu maana nchi kama Japan na China huwa wanawala sana na wakati mwingine huwa wanaaminishwa na imani fulani kama moja ya viumbe vyenye kuongeza sana nguvu ya mwili kwa kuimarisha seli hai nyeupe (white blood cells)


.instagram @thewildlife_tz
sciencechannel-20190430-0001.jpeg
 
Hivi ndo huyu aliyecheza kwenye animation movie ya moana?
 
Back
Top Bottom