Wanaharakati walalamikia vurugu za mchina Songea

Wanaharakati walalamikia vurugu za mchina Songea

Joined
Mar 23, 2012
Posts
64
Reaction score
13
NA, STEPHANO MANGO,SONGEA

WANAHARAKATI wamelalamikia Kitendo cha Raia wa Nchi ya China Zhouguang Zheng (27)maarufu kwa jina la Dani Johnson Kumpiga na Kumsababishia Maumivu Makali Mfanyabiashara Maarufu Na Mkurugenzi wa Kampuni ya Mabasi ya Kisiwa Sport, Kisiwa Kisiwa (40) na kumsababishia Kulazwa Siku Mbili katika Hospital ya Serikali ya Mkoa wa Songea na Wengine wawili walijeruhiwa katika Vurugu hizo

Wakizungumza kwa Nyakati Tofauti na Gazeti Hili jana Walisema kuwa Kitendo hicho ni kibaya sana kwani kimekiuka Sheria za Uraia na Uwekezaji, ingawa pia ni ukiukwaji mkubwa wa Haki za Binadamu na kinavuruga amani na Utulivu Miongoni Mwa Jamii

Hamis Abdala Ally alisema kuwa kitendo cha Mwekezaji huyo wa Kampuni ya Mabasi ya NewForce inayosafirisha Abiria kutoka Songea Kuelekea Jijini Dar Es Salaam kimevuka mipaka yake ya Uwekezaji na Ukiukwaji mkubwa wa Sheria na Taratibu

Ally Alisema kuwa ni kosa sana Raia wa Kigeni kwenye Nchi ya Watu kufanya Vurugu na Kusababisha Raia wa Nchi Husika kupata Maumivu Makali katika Mwili wake , kwani kitendo hicho kinaweza Kusababisha chuki na amani kuvurugika miongoni mwa Jamii
Alisema kuwa Tukio hilo linahatarisha uwekezaji wake, ushirikiano uliojengeka kwa kipindi kirefu kwenye jamii husika kwani mahusiano ya Watu yamepungua kutokana na Jambo hilo

“Tunalitaka Jeshi la Polisi Kutenda Haki Katika Jambo Hili la Mchina Kufanya Vurugu na Kusababisha amani kutoweka Katika eneo la Stendi Kuu ya Mabasi Songea kwa Zaidi ya Masaa sita na kuongezeka kwa Chuki Miongoni mwa jamii ya Wafanyakazi wa Kampuni ya Mabasi ya Super Feo na NewForce”Alisema Ally
Alieleza kuwa Wananchi wa Songea hatuna utaratibu wa kuwadhuru au kuwanyanyasa Raia wa Kigeni wawapo kwenye Shughuli zao lakini Tumeshangazwa na Mchina Huyu ambaye ameanzisha Utamaduni Mpya wa Kuwajeruhi Wazawa

Mukhtar Simba Alisema kuwa Wanaruvuma ni watu Waungwana na Wakarimu sana na kwenye Swala la Uwekezaji Kuna Sheria na Taratibu ambazo zinamuongoza Mwekezaji kufanya shughuli zake pia ana mipaka ya uwekezaji wake katika eneo husika

Simba Alisema Tunalaani na kushangaa Kumuona Mwekezaji Huyo bado anaendelea Kutamba Mitaani huku Mwenzake akiendelea na Matibabu ambayo yamesababishwa na Kipigo chake wakati sheria zipo wazi

Akizungumzia Tukio Hilo Mkurugenzi wa Kampuni ya Super Feo Omari Msigwa Alisema kuwa Kitendo alichokifanya Mchina Siku hiyo Cha Kumpiga Msaidizi wake Haruna Msigwa na Kisiwa Kisiwa na Kuifanya Stendi kuwa ni Uwanja wa Vurugu kimemshtua Sana kwani Hakukitegemea katika Sekta ya Usafirishaji Mkoani Ruvuma

Msigwa Alisema kuwa licha ya Jambo hilo kuwa ni Ukiukwaji Mkubwa wa Haki za Binadamu na Sheria za Nchi Lakini pia kimeleta picha mbaya sana Katika Sekta ya Usafirishaji kiujumla kwani Vurugu hizo zimetokea Mbele ya Abiria ambao hawajawahi kuona wala kutarajia vurugu katika Stendi hiyo

Alieleza kuwa Sheria ziko wazi za Uwekezaji na za Kijinai hivyo ni Muhimu Mamlaka zinazohusika kuchukua Hatua Stahiki Katika Jambo hilo kwani kutochukua hatua madhubuti kutasababisha ulipizaji wa Kisasi miongoni mwa Jamii hizo

“Ili Kuepuka chuki hizo ni Vyema Mamlaka zinazohusika Zikatenda Haki kwa Kila Mmoja aliyeenda Kinyume cha Sheria na Taratibu katika Tukio hilo Kwani Kitendo cha Kumpendelea Mtu huku Ukweli wa Jambo ukiwa wazi kitaanzisha utamaduni mbaya ambao utaleta athari nyingi baadaye” Alisema Msigwa

Alieleza zaidi kuwa Siku za Nyuma Kulikuwa na Kampuni Nyingi za Usafirishaji Abiria kama Vile Sabco, Saibaba,Scandnavia,Ottawa, na Nyinginezo lakini hakuna Siku Hata Moja Wafanyakazi wake au Wafanyakazi wa Kampuni nyingine hizo Kupigana lakini leo Mwekezaji wa Kigeni Amempiga Mwekezaji wa Ndani hali ambayo inazua Mashaka sana

Akizungumza na Gazeti hili Nyumbani Kwake Kisiwa Kisiwa alisema kuwa Ni ukweli ulio wazi kuwa nimepigwa tena kipigo Kikali na Mchina hadi kulazwa Siku Mbili kutokana na Maumivu Makali Katika Sehemu mbalimbali za Mwili wangu

Kisiwa Alisema licha ya Kushonwa Nyuzi kumi na nne Mdomoni kutokana na Kipigo bado mwili wangu haujatengamaa na maumivu makali bado nayasikia na sijaanza kufanya kazi zangu za kila siku kama ilivyo ada

Alisema kuwa Mchina huyu amekosa Utu wala aibu Toka anisababishie Maumivu katika Mwili wangu ameshindwa hata kunijulia hali bali yeye amekuwa akiendelea na shughuli zake huku mie nikiendelea kuumwa

Kamanda Wa Polisi Mkoa wa Ruvuma Mihayo Msikhela alisema Tukio hilo lilitokea Januari 13 Majira ya Saa 12:10 asubuhi katika eneo la Kituo Kikuu cha Mabasi Kilichopo Msamala Mjini hapa , ambako ilizuka Vurugu kubwa baina ya Wafanyakazi wa Kampuni ya Mabasi ya Usafirishaji Abiria ya New Force na Kampuni ya Super Feo wakigombaniana ratiba ya kuondoa Mabasi yao kutoka Songea Kuelekea Jijini Dar Es Salaam

Msikhela Alisema kuwa Katika tukio hilo Watu watatu wamejeruhiwa ambao ni Zhouguang Zheng (27) ambaye ni Raia wa China, Danford Thomas (40) Mkazi wa Mfaranyaki na Abdurabi Kisiwa ambaye pia ni Mkazi wa Mfaranyaki na Mmiliki wa Mabasi ya Kisiwa Sports

Alieleza zaidi kuwa inadaiwa katika vurugu hizo vitu mbalimbali vimepotea zikiwemo Simu mbili aina ya Tecno ambazo thamani yake bado haijafahamika ambazo zilikuwa mali ya Kisiwa, simu moja ya IPhone 5s yenye thamani ya milioni 1.5 pamoja na fedha taslim shilingi milioni nne zimeporwa na watu wasiofahamika ambazo ni mali ya Zhouguang Zheng

Alisema kuwa kufuatia tukio hilo watu 14 wamekamatwa na Kuhojiwa na Polisi kwa tuhuma za kujihusisha katika vurugu hizo na wapo nje kwa dhamana na kwamba Jarada la Uchunguzi Limefunguliwa na Kupewa namba SO/IR/ 189/015 Na kwamba upelelezi bado unaendelea kufanywa na kwamba ukikamilika Jarada hilo litapelekwa Ofisi ya Mwanasheria wa Serikali ili kulifanyia kazi kabla halijaenda Mahakamani
MWISHO
 
Ni upumbavu kulalamika umepigwa na mgeni ukiwa nyumbani kwako!
Ni muhimu wageni wafinywe kidogo, kama hamuwezi moja kwa moja, wafanyiwe hujuma waogope kidogo!
Katika hali ya kawaida tunategemea mgeni alalamike kuhusu kufanyiwa fujo na siyo mwenyeji!
 
mm n mkaz Wa songea na Mara nyng huwa na safar za Dar.sijui Sana kuhusu ugomv Wa new force na super feo but nlichokishuhudia asubuh moja ni kuwa super feo wanatumia ubabe Wa uzawa na kumnyima new force nafac za kufanya biashara.
kwa mfano super feo anataka gar zake zote ztoke sa 12 kamili Zen new force atoke nusu saa baadae.kumbuka Dar n mbali na abiria akichelew kufka kesho hapand tena new force.
cha kushangaza mpaka uongoz mkubwa Wa polic mkoa nliwaona sikuile stand wakihakksha new force hatoki.nkajiuliza mbona nkitoka Dar wote tunatoka kawaida tu.
nkajiuliza Kama kunasheria kwann zctende haki.kwamba superfeo atoe bac yake kwanza na new force atoe,la pili hvyovlhvyo na la Tatu pia ila sio super feo zote tatu kwanza then new force afuate.
pia mleta mada amejikita kwenye kumshutum mchna bla kueleza sababu ya ugomv .this show jamaa n mtu Wa superfeo.so kojoa kalale usilete unafki humu!!
ofcoz nmechangia tu but sihusk na yeyote Kati yao,bye!!
 
Wafanyabiashara wa Usafirishaji Songea badilikeni ndg zangu acheni kufanya biashara kimazoea na kizamani biashara ya sasa hivi ni mashindano.huyo Kisiwa na Omary ni wapuuzi tu acheni huduma bora iongee kwa ninavyowajua mmemshindwa huyo mchina kwa mbinu za giza mnaanza fitina.kiutaratibu Songea ilitakiwa Super feo ikitoka moja New Force ifuatie sasa Omary na watu wake kisa mmeishika Selikari ya Mkoa mnafanya vurugu ila mtawaharibia kazi hao watu wa Serikali tutaona huko mbele
 
Ni upumbavu kulalamika umepigwa na mgeni ukiwa nyumbani kwako!
Ni muhimu wageni wafinywe kidogo, kama hamuwezi moja kwa moja, wafanyiwe hujuma waogope kidogo!
Katika hali ya kawaida tunategemea mgeni alalamike kuhusu kufanyiwa fujo na siyo mwenyeji!
Hahahahaa baada ya wanaume wa dar es salaam kuhenyeshwa na panya road kumbe na ruvuma nako hakuna lolote, yaani wanaume wa miaka 40 unapigwa na kamchina kamoja ka miaka 27??? Tena katika ardhi yenu? Shame on you!
 
mm n mkaz Wa songea na Mara nyng huwa na safar za Dar.sijui Sana kuhusu ugomv Wa new force na super feo but nlichokishuhudia asubuh moja ni kuwa super feo wanatumia ubabe Wa uzawa na kumnyima new force nafac za kufanya biashara.
kwa mfano super feo anataka gar zake zote ztoke sa 12 kamili Zen new force atoke nusu saa baadae.kumbuka Dar n mbali na abiria akichelew kufka kesho hapand tena new force.
cha kushangaza mpaka uongoz mkubwa Wa polic mkoa nliwaona sikuile stand wakihakksha new force hatoki.nkajiuliza mbona nkitoka Dar wote tunatoka kawaida tu.
nkajiuliza Kama kunasheria kwann zctende haki.kwamba superfeo atoe bac yake kwanza na new force atoe,la pili hvyovlhvyo na la Tatu pia ila sio super feo zote tatu kwanza then new force afuate.
pia mleta mada amejikita kwenye kumshutum mchna bla kueleza sababu ya ugomv .this show jamaa n mtu Wa superfeo.so kojoa kalale usilete unafki humu!!
ofcoz nmechangia tu but sihusk na yeyote Kati yao,bye!!
Atleast maelezo yako yako fair maana mleta hoja kakaa kipilatopilato tu ,ukianzisha ugomvi wa maneno tegemea matusi na ukianzisha ugomvi mwilini manundu na mishono ni kawaida sana mwambieni kisiwa augue pole na akome kuchokoza vishaolin vya miaka 20++ ilhali yeye jizee la miaka 40++ na mazoezi pekee ayafanyayo ni kujamba tu!
 
Pole bwana Island ila ukipona nawe jitahidi ulipe kisasi, usikubali kirahisi bwana mdogo akudharirishe bila kuchukua hatua yyte. Wenzako tumemjaza gris tumboni mchina kwa kupitia tigo yake, nawe jitahidi umpasue na wheel spanner.
 
Hahahahaaaaa!!!! Jamii Forum kwangu ni kiburudisho tosha!!!! Mleta mada kaegemea upande mmoja. Mimi ni mkazi wa Songea,kwetu panaitwa Shule ya Tanga km chache kutoka Songea mjini japo kwa sasa naishi Dar,lakini ninasafari za mara kwa mara za Dar/Songea. Hawa Superfeo biashara imewashinda,wanatumia uenyeji wao kudidimiza wawekezaji wakigeni. Nakubali kwa asilimia kubwa kuwa ushindan wakibiashara kati ya hizi kampuni mbili ni mkubwa sana.Na kwa yeyote anayejua atakiri hili.Baada ya Newforce kuanza rout za Songea Dar,mabadiliko makubwa ya kihuduma ktk mabas ya Superfeo zilibadilika na kuanza kuwa nzuri tofauti na hapo awali. Bahati nzuri nshasafiri sana na makampuni yote mawili. Newforce wako vizuri sana kihuduma hasa ktk lugha za kibiashara,tofauti na Superfeo. Sasa,superfeo mmemshindwa mchina kishirikina mnataka ngumi. Mchina kaanza kuruka karate toka akiwa tumboni mwa mamayake. Kizuri chajiuza,kibaya chajitembeza.
 
Super Feo kazidiwa, naijua kampuni ya New Force wanatoa magari mapya kila baada ya miezi mitatu.

Mchina alianza kwa kupeleka gari moja Songea sasa hivi anapeleka gari tatu hadi nne kwa siku, wakati Feo alikua anatoa gari hadi sita kwa siku sasa hivi anatoa mbili hadi nne.

Kwa hiyo sasa hivi kuna ushindani wa hali ya juu sana, Watu wanataka huduma nzuri za uhakika na nafuu.

Huo uzawa haumsadii mwananchi wa Kawaida kama huduma zako mbovu na gharama.
 
hii ratiba nashindwa kuielewa mantiki yake mana nimotoka songea trh 20 january na nilikuwa nasafiri ni hii kampuni ya new force inafika saa kumi na mbili dereva anawasha gari tuondoke trafiki akazuia eti mpaka saa kumi na mbili na dk 10 wakati huo gari feo toka za dar, mbeya,dodoma na iringa zote zinatangulia huo muda sasa najiuliza wanatumia kigezo gani kwa kuruhusu feo atoe gari zake zote halafu wengine wafuate mwishoni?
 
Unataka kumpiga mchina kwa ngumi... thubutu.... labda utumie gobore.
 
NINACHOKIJUA MIMI TOKA NDANI KABISA YA HUU UGOMVI ni kwamba super feo ana time table ya saa 6:00am na 6:10am kutoka songea na gari zake zote za dsm zipo ndani ya muda huo wakati huo huo mbeya na iringa na dom ana gari za saa 6:00am na 6:20am katika hali hii super feo inabidi atoke saa kwanza ndiyo new force afate saa 6:30am sasa inapoonekana super feo zinatoka zote kwa mara moja inaonekana kuna upendeleo kwake lakini si kweli ana vigezo vya kutoka muda huo sasa kilichofanyika hapa karibuni ni kwamba new force alipewa muda wa saa 6:10am na sumatra kwa madai kuwa super feo hana gari semi luxury ikabidi super feo alalamike kwanini iwe hivyo yeye pia ana semi luxury katika muda huo sumatra wakaingilia kati na kuamua kila kampuni ikae katika muda wake yaani super feo saa 6:00am na new force saa 6:30am sababu ikumbukwe kuwa mbeya express muda wake ni saa 6:20am ingawa hayupo kwa sasa!

CHANZO CHA UGOMVI SASA! super feo baada ya kuona kuna ushindani mkubwa baina yake na new force na magari wanayotumia ni tofauti yaani zhongtong newforce na yutong super feo,super feo akaenda kwa newforce ambae zamani alikua ni ajent wa yutong kwa sasa ni ajent wa zhongtong ili auziwe gari kama za newforce lakini new force akakataa kumuuzia gari hizo yaani zhongtong na hata super feo alipojaribu kuagiza gari hizo moja kwa moja kiwandani alikataliwa na wachina kununua gari hizo kwa kumwambia kuwa arudi kwa ajent wao wa TZ ambae ni new force ambae anamkatalia kununua gari hizo kwa hofu ya ushindani kuzidi ona Mtanzania huyu anavokandamizwa na mchina

KILICHOTOKEA SIKU YA TUKIO!baada ya sumatra kuwaondoa new force katika muda wa saa 6:10am ambao ni wa super feo newforce siku ile alitaka kutoka katika muda huo ndipo mfanyakazi wa super feo alihoji kwanini watoke katika muda huo wakati muda wao ni saa 6:30am ndipo mchina alipoanza vurugu na bwana kisiwa alipokwenda kuamua yakamkuta yale yaliyomkuta.

MASWALI YA KUJIULIZA
1>ni kweli uwekezaji wa mabasi umewashinda wazawa mpaka aje muwekezaji wa kichina
2>kama wazawa kama huyu watadidimizwa na mchina kwa kuendelea kukataliwa kununua gari zenye ushindani ajira za watanzania waliopo kwenye makampuni haya ya wazawa zitakuaje?
3>tusaidiane ni kweli wachina nauli wanazotoza zinaingia kwenye akaunti za benk zilizopo hapa kwetu au wanapeleka kwao
4>inasemekana kuwa hayo mabasi wanakopeshwa huko kwao je wanalipaje au ndo wanahamishia uchumi wetu kwao?
 
sumatra wana majibu yote
wao ndio wapanga hizo taratibu
 
hii ratiba nashindwa kuielewa mantiki yake mana nimotoka songea trh 20 january na nilikuwa nasafiri ni hii kampuni ya new force inafika saa kumi na mbili dereva anawasha gari tuondoke trafiki akazuia eti mpaka saa kumi na mbili na dk 10 wakati huo gari feo toka za dar, mbeya,dodoma na iringa zote zinatangulia huo muda sasa najiuliza wanatumia kigezo gani kwa kuruhusu feo atoe gari zake zote halafu wengine wafuate mwishoni?
sumatra ndio wapanga ratiba wanajua kila kitu mjomba na ukumbuke newforce alikuja kuuza magari na spea kwa wazawa c kusafirisha abiria
 
hapa naona hakuna mtu anaeelewa kuhusu usafiri wa songea, mimi daily niko road na hayo magari. hivi kwa nini hamjiulizi why superfeo haifi miaka nenda miaka rudi? zimepita kampuni ngapi na zikafa? sio kwamba ni wababe or sheria iko mikononi, hawa ni wafanya biashara na wanajua nini mteja anataka. superfeo wanajua kucheza na muda, ukiambiwa muda wa kuwasir ni 05:30 nenda muda huo sababu mara nyingi muda wa kutoka ni 06:00 na gari huwa saa 05:50 zishawashwa zinawahi foleni kukaguliwa na askari theni ziondoke. SASA EBU WEWE UNAESEMA HUO NI UBABE NIKUULIZE SWALI, je wewe kuwahi kazini kwako saa 11 kila siku kabla ya wenzako ni ubabe? kwa hiyo wao kuwahi foleni ni ubabe? labda wangekuwa wanawachomekea kwa mbele huo ndio ubabe. Hii new force mi nshapanda zaid ya mara mbili kwa mwaka jana. mara ya mwisho nakumbuka iliwahi kutoka ubungo kabla ya superfeo, hii gari.
USILETE USHABIKI KWA KUWA ULISAFIRI MARA 1 AU UNASAFIRI MARA 2 KWA MWAKA. KAMA UNAIJUA STAND ILE ILIYOKO KWENYE UKARABATI NA HII YA SASA UWEZI ONGEA POINTLESS. KILA MTU ANAJUA SUPERFEO ZINAPAKI WAPI, MBEYA/SUMRY KWA WAKATI HUO, OTTAWA ENZI HIZO, TONDA NA MENGINE YANAPAKI WAPI. HAIWEZEKANI SUPERFEO ILIYOKUWA INAPAKI KWENYE KONA KULE MWISHO IWAI FOLENI USEME NI UBABE, NADHANI NI UBWEGE WA KAMPUNI NYINGINE NDIO UNACHANGIA. Biashara ni ushindani, lakini ushindani wa kijuha ni upuuzi, sheria zipo, polisi wapo, kwa nini kama unaona unaonewa na kampuni nyingine usifuate sheria uishie kupigana.
 
Back
Top Bottom