Lilifungiwa kwa sababu lilikuwa linasema ukweli na kwa uwazi. Viongozi wetu wamesahau kuwa ukweli huwezi kuufunika kwa kiganja cha mkono. Kwa kulifungia ndiyo kwanza walizidi kujianika kwani sasa tunajua serikali ndiyo inayojihusisha moja kwa moja na vitendo hivi.
Tanzania Daima si lipo? Au mbowe yupo kibiashara zaid so anaogopa lisifungiwe? Maana slaa katuambia wale watu wake wa kwenye system walimjulisha juu ya mpango huo
....mkuu ukitaja Mwanahalisi, ikulu ya Salva wanaweweseka....nina mashaka kama litafunguliwa....kwangu mie nina "maktaba" ya gazeti hili nilikuwa sikosi "hardcopy" yake....siku CCM ikitoka madarakani huo utakuwa ni ukombozi wa pili kwa Mtanzania, mpenda haki....
Salamu wakuu,
natumain mwanahalisi ungekua barabarani ungetutegulia vitendawili vingi vinavyoendelea kulizonga taifa,pamoja na sinto fahamu nyingi. Kuanzia kibanda,lwakatare na mazonge zonge kibao. I miss you mwana halisi. Leo nimeshika gazeti la mwisho kutolewa na hali halisi na kusoma mtekaji wa ulimboka dahh,
Kubenea naona anapiga mahesabu pa kuanzia. Maana wanamfunga mdomo, mikono, miguu. Walitaka kumfunga macho kwa kutumia tindikali lakini naona Kubenea is far stronger than them - akaipangua!
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.