Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu nchini, umetoa tamko kwa Serikali ya Rais Jakaya Kikwete, kuagiza watendaji wake kulifungulia gazeti la Mwanahalisi.
Tamko hilo lilitolewa na Mwenyekiti wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRD), Marcos Albanie, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari, jana jijini Dar es Salaam.
Albanie alisema tangu serikali itangaze kulifungia gazeti la wiki la Mwanahalisi ni jana siku 175 sawa na kipindi cha miezi mitano na siku 24, wadau wa habari na wananchi wamekuwa wakipaza sauti kuiomba serikali kulifungulia gazeti hilo lakini imekuwa kimya.
Aliongeza kufungiwa kwa gazeti hilo kulitokana na taarifa kuhusiana na kutekwa, kuteswa na kisha kutupwa katika msitu wa Mabwepande, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari nchini, Dk. Stephen Ulimboka.
Tamko hilo lilitolewa na Mwenyekiti wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRD), Marcos Albanie, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari, jana jijini Dar es Salaam.
Albanie alisema tangu serikali itangaze kulifungia gazeti la wiki la Mwanahalisi ni jana siku 175 sawa na kipindi cha miezi mitano na siku 24, wadau wa habari na wananchi wamekuwa wakipaza sauti kuiomba serikali kulifungulia gazeti hilo lakini imekuwa kimya.
Aliongeza kufungiwa kwa gazeti hilo kulitokana na taarifa kuhusiana na kutekwa, kuteswa na kisha kutupwa katika msitu wa Mabwepande, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari nchini, Dk. Stephen Ulimboka.