Salam za weekend wakuu...
Jana katika uteuzi wa baraza la mawaziri kulitokea jambo lisilo la kawaida.
Mara baada ya rais kumaliza alitoa nafasi kwa waandishi waweze kumuuliza maswali yeye ama waziri mkuu au Makamu wa rais.
Lakini waandishi waliamua kukaa kimya.
Jambo hili sio la kawaida kabisa,hasa kwa hali ya mambo yalivyo maana kuna mambo mengi ya kuhitaji kupata ufafanuzi,iweje wao wakae kimya?
Wamechoka kufanya kazi? Maelekezo kutoka juu wasiulize chochote?
Ushauri,
Press nyingine zifanyike vyuoni kama pale udsm ili waweze kumuhoji vizuri.
wasalam..