ngoshwe
JF-Expert Member
- Mar 31, 2009
- 4,131
- 931
Wana JF, sina nia ya kuponda products za vyuo vikuu binafsi, ila kuna tofauti kubwa sana hasa katika utendaji kazi kati ya wanafunzi wanaomaliza vyuo vikuu vya umma na wale wanaotokea vyuo vikuu binafsi. Nina uzoefu wa zaidi ya miaka 10 katika ajira niliyonayo sasa. Kwa mujibu wa majukumu niliyonayo, nimekuwa nikikutana na watendaji wa umma tofauti na wengine wamefanya kazi chini yangu. Hata hivyo, ukichunguza uwezo wa kufaulu, inaonekana kuwa wale waliotoka vyuo binafsi wengi wamefaulu kwa viwango vya hali ya juu ukilinganisha na wanaotokea vyuo vya umma. Lakini kwenye utendaji, inakuwa vigumu sana kwa baadhi ya wanaotokea vyuo binafsi kuelewa mambo haraka tofauti na ufaulu wao kitaaluma unavyoonyesha. Sijui tatizo lipo wapi!!!