Mwanantogakulya
Senior Member
- Mar 18, 2025
- 154
- 153
Wanafunzi wenye mahitaji maalum katika shule ya msingi Sima A iliyopo katika Hamlashauri ya mji wa Bariadi mkoani Simiyu wamepatiwa misaada mbalimbali kwa matumizi ya shule
Misaada hiyo imetolewa na waendesha baiskeli kutoka Dar Es Salaam kuelekea wilaya ya Butiama mkoa wa Mara kwa lengo ni kusaidia wanafunzi hao kuweza kusoma katika mazingira yaliyo rafiki
Waendesha baiskeli hao walikabidhi viti mwendo,magongo ya kutembelea, magodoro 40, vitanda 20 pamoja na kusaidia ujenzi wa matundu 10 ya vyoo kwa ajili ya wanafunzi hao pia wamepanda miti 100 katika eneo la shule hiyo kwa lengo la kuhifadhi mazingira.
Akizungumza baada ya kupokea misaada hiyo, Afisa Elimu Maalum wa Mji wa Bariadi, Rutherford Magayame alikiri kuwa msaada huo umetolewa kwa wakati mwafaka, akisema utasaidia kuboresha mazingira ya ujifunzaji
Soma pia:
www.jamiiforums.com
“Tunatoa shukrani za dhati kwa moyo wa upendo,walimu wenye taaluma ya kufundisha wanafunzi wenye mahitaji maalum wakiwemo viziwi na wasioona ni wachache hivyo tutatumia vifaa hivi kupunguza changamoto nyingi kwa watoto wetu na kuongeza ari ya kujifunza,”amesema
Awali Gabriel Lando ambaye ni kiongozi wa waendesha baiskeli hao wakiwa wanatoka mataifa mbalimbali ya nchi za Afrika Mashariki na Kati wakiwemo Kenya, Rwanda, Burundi, Uganda,Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na Tanzania amesema kuwa safari yao siyo kwa ajili ya michezo pekee bali ni kuchochea mabadiliko ya kijamii katika sekta ya elimu,afya na mazingira
“Tunaendeleza ile kampeni yetu kuboresha amani,umoja na mshikamano kwa kuchochea shughuli za maendeleo katika sekta ya elimu,afya na mazingira pia ni kuenzi urithi wa Mwalimu Nyerere kupitia vitendo vya mabadiliko katika jamii,tunataka wanafunzi wenye mahitaji maalum wapate fursa sawa ya elimu,”amesema
Msafara huo umewezeshwa na Vodacom Tanzania na Benki ya Stanbic, akizungumza Meneja wa Vodacom,kanda ya Ziwa, Stratton Mchau amesema kuwa wataendelea kudhamini safari hizo za kwenda Butiama kumuenzi Baba wa Taifa, Mwl Nyerere katika kuchochea na kuleta mabadiliko katika jamii
“Kwa mwaka huu Vodacom Fondation tunategemea kuzitembelea shule 30,kupanda miti zaidi ya 50,000 na zaidi wa watu 700,000 watagushwa kwa namna moja au nyingine,”amesema
Waendesha baiskeli hao wanatarajiwa kuhitimisha safari yao Butiama kwa shughuli maalum ya kumuenzi Mwalimu Nyerere ambaye alisimamia misingi ya haki, elimu kwa wote na usawa katika jamii
.
Misaada hiyo imetolewa na waendesha baiskeli kutoka Dar Es Salaam kuelekea wilaya ya Butiama mkoa wa Mara kwa lengo ni kusaidia wanafunzi hao kuweza kusoma katika mazingira yaliyo rafiki
Waendesha baiskeli hao walikabidhi viti mwendo,magongo ya kutembelea, magodoro 40, vitanda 20 pamoja na kusaidia ujenzi wa matundu 10 ya vyoo kwa ajili ya wanafunzi hao pia wamepanda miti 100 katika eneo la shule hiyo kwa lengo la kuhifadhi mazingira.
Akizungumza baada ya kupokea misaada hiyo, Afisa Elimu Maalum wa Mji wa Bariadi, Rutherford Magayame alikiri kuwa msaada huo umetolewa kwa wakati mwafaka, akisema utasaidia kuboresha mazingira ya ujifunzaji
Soma pia:
TET: Wanafunzi Wenye Mahitaji Maalum hawajasahaulika katika mifumo ya Kujifunza
Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Elimu Tanzania (TET), Dkt. Aneth Anselmo Komba, amesema kuwa taasisi hiyo imefanikiwa kuweka mazingira jumuishi ya kujifunza kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum kwa kuhakikisha wanapata vifaa na nyenzo sahihi za kujifunzia na kufundishia. Mafanikio ya Elimu...
“Tunatoa shukrani za dhati kwa moyo wa upendo,walimu wenye taaluma ya kufundisha wanafunzi wenye mahitaji maalum wakiwemo viziwi na wasioona ni wachache hivyo tutatumia vifaa hivi kupunguza changamoto nyingi kwa watoto wetu na kuongeza ari ya kujifunza,”amesema
Awali Gabriel Lando ambaye ni kiongozi wa waendesha baiskeli hao wakiwa wanatoka mataifa mbalimbali ya nchi za Afrika Mashariki na Kati wakiwemo Kenya, Rwanda, Burundi, Uganda,Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na Tanzania amesema kuwa safari yao siyo kwa ajili ya michezo pekee bali ni kuchochea mabadiliko ya kijamii katika sekta ya elimu,afya na mazingira
“Tunaendeleza ile kampeni yetu kuboresha amani,umoja na mshikamano kwa kuchochea shughuli za maendeleo katika sekta ya elimu,afya na mazingira pia ni kuenzi urithi wa Mwalimu Nyerere kupitia vitendo vya mabadiliko katika jamii,tunataka wanafunzi wenye mahitaji maalum wapate fursa sawa ya elimu,”amesema
Msafara huo umewezeshwa na Vodacom Tanzania na Benki ya Stanbic, akizungumza Meneja wa Vodacom,kanda ya Ziwa, Stratton Mchau amesema kuwa wataendelea kudhamini safari hizo za kwenda Butiama kumuenzi Baba wa Taifa, Mwl Nyerere katika kuchochea na kuleta mabadiliko katika jamii
“Kwa mwaka huu Vodacom Fondation tunategemea kuzitembelea shule 30,kupanda miti zaidi ya 50,000 na zaidi wa watu 700,000 watagushwa kwa namna moja au nyingine,”amesema
Waendesha baiskeli hao wanatarajiwa kuhitimisha safari yao Butiama kwa shughuli maalum ya kumuenzi Mwalimu Nyerere ambaye alisimamia misingi ya haki, elimu kwa wote na usawa katika jamii
.