Intellect
Member
- Apr 1, 2011
- 34
- 20
Ninasikitishwa sana na wanafunzi wa leo katika taasisi za elimu ya juu kutokana na kuharibu taswira iliyokuwepo juu ya mwanafunzi kama balozi wa wananchi ambao hawana taasisi inayosimamia matatizo yao kikamilifu, hii inajidhihirisha katika matukio ya wanafunzi kuanzisha migomo ambapo mingi inalenga maslahi yao binafsi na sio maslahi ya taifa kwa ujumla. Katika maswala ya msingi kama vile ufisadi, matumizi mabaya ya fedha za uma nk. wanafunzi wamekua wagumu kuwasilisha hisia za wananchi hata kwa kugoma, ila pesa za mkopo zikicheleweshwa utauona moto wake!
​
Hivi karibuni wanafunzi wa kiislam waligoma kwa kile walichodai haki ya kuabudu, hii ilitokana na kufukuzwa kwa wanafunzi wa shule ya Ndanda kwa kushinikiza ujenzi wa msikiti katika eneo la shule ambapo pia kuna kanisa. Nilidhani wanafunzi hao walipaswa kujua kama haki nyingi katika "Bill of Rights" ndani ya katiba yetu ikiwamo haki ya kuabudu haziko "exclusive" kwamba serikali hailazimiki kuzisimamia katika baadhi ya mazingira. Ikumbukwe kwamba nchi yetu haina dini kwa mujibu wa katiba sambamba na hilo ikumbukwe kuwa shule ya Ndanda ilikua mali ya kanisa katoliki kabla ya uhuru, na ni kwa jitihada za Mwl. Nyerere shule hii na nyingine nyingi zilitaifishwa pamoja na makanisa ndani yake ili kuwapa fursa hata watoto wasio wakristu kupata elimu! Sasa sioni tija ya wanafinzi hawa wa kiislam kuishurutisha serikali kujenga msikiti hapo shuleni ikiwa hata kanisa halikujengwa na serikali!
Ninawashauri wanafunzi hawa wazishurutishe taasisi za dini yao kujenga nyumba ya ibada karibu na shule na ikiwa serikali itatia ngumu hapo wanaweza kugoma kwa mujibu wa sheria!
Mwisho, nadhani wakati umefika kwa wanafunzi kuanza kugomea mambo ya msingi yanayo wagusa wananchi kwa ujumla!
​
Hivi karibuni wanafunzi wa kiislam waligoma kwa kile walichodai haki ya kuabudu, hii ilitokana na kufukuzwa kwa wanafunzi wa shule ya Ndanda kwa kushinikiza ujenzi wa msikiti katika eneo la shule ambapo pia kuna kanisa. Nilidhani wanafunzi hao walipaswa kujua kama haki nyingi katika "Bill of Rights" ndani ya katiba yetu ikiwamo haki ya kuabudu haziko "exclusive" kwamba serikali hailazimiki kuzisimamia katika baadhi ya mazingira. Ikumbukwe kwamba nchi yetu haina dini kwa mujibu wa katiba sambamba na hilo ikumbukwe kuwa shule ya Ndanda ilikua mali ya kanisa katoliki kabla ya uhuru, na ni kwa jitihada za Mwl. Nyerere shule hii na nyingine nyingi zilitaifishwa pamoja na makanisa ndani yake ili kuwapa fursa hata watoto wasio wakristu kupata elimu! Sasa sioni tija ya wanafinzi hawa wa kiislam kuishurutisha serikali kujenga msikiti hapo shuleni ikiwa hata kanisa halikujengwa na serikali!
Ninawashauri wanafunzi hawa wazishurutishe taasisi za dini yao kujenga nyumba ya ibada karibu na shule na ikiwa serikali itatia ngumu hapo wanaweza kugoma kwa mujibu wa sheria!
Mwisho, nadhani wakati umefika kwa wanafunzi kuanza kugomea mambo ya msingi yanayo wagusa wananchi kwa ujumla!