Wanafunzi wa IFM fanyeni haya kama mnataka kuishi salaama

Usitetee uzezeta. Kichwa cha habari na habari yenyewe kifo na usingizi ukiachia mbali kujikanyaga. Kuna nini la lipi hapa gumu la kutafuniwa. Jaribu kupitia maoni yote uone ulivyochemsha hata kama uking'aka vipi mwanangu Mwanaweja.
acha uzezeta na ukichwa maji, wewe usiyejua kusoma maana inaonekana hauna utofauti na hao jamaa walikuwa wamejaa kwenye feri bila kujua nini kitatokea mbeleni
 
binafsi nakuunga mkono kwa point yako ya kupinga hao wanachuo kujazana kwenye kivuko kwa lengo lao la kushinikiza madai yao. uko sahihi kabisa. tatizo langu topic yako iko vipande vipande...ungeiweka pamoja katika para. pili sioni kama ni sawa kulinganisha mazingira ya Mbeya na Dar...mazingira na watu ni tofauti katika maeneo hayo mawili. otherwise concern yako ni sawa!
Unachokisema nakiunga mkono lakini, kwa maana ya mazingira, ni juu yao kichagua kipi kilitokea mbeya kitafaa kigamboni. Kila mtu humu atatoa uzoefu na nini kifanyike kutegemeana na mahali alipoupata uzoefu huo. Si mpaka uwe umekaa kigamboni ndo utoe uzoefu wa huko. Kuna comon logic ambayo ipo applicable popote regardless hapo mahala panafananaje. Kwa mfano, amezungumzia kujazana kwenye feri, huko MTC hakuna feri etc. Na vile vile kasema idadi yao inatosha kabisa kukomesha tabia hizo hapo chuoni. Wao waikuwa 150, lakini IFM wapo 600. Ni wao kuamua tu.

Kuna mwizi tulimkamata pale hall 3 UDSM. Jamaa alikuwa katoka mwenge lakini kimuonekano utadhani mwanachuo. Akamtaimu dada mmoja floor ya kwanza na akaondoka na begi. Tulimtilia shaka na kwenye kumuhoji akaonyesha kujikanyaga na akaishi kituo cha polisi pale UDSM.

Tatizo ni kuwa huko vyuoni siku hizi hatuna utaratibu wa kuuliza nani ni nani. Na hii imeenda hadi kwenye level ya taifa. Zamani mgeni akiingia tu kijiji chochote, mara moja taarifa zishafika kunakohusiku, siku hizi haya mambo hayapo. Ni mpaka walawitiwe ndo wanaanza kujazana kwenye feri..... Shame
 
Issue si kwamba sijui kusoma. Utawekaje habari in piecemeals utegemee watu wapoteze muda kufuata mparaganyiko wako? Kama unaona wewe ni bingwa wa matatizo basi nenda kawasaidie badala ya kupayuka tu. Right?
acha uzezeta na ukichwa maji, wewe usiyejua kusoma maana inaonekana hauna utofauti na hao jamaa walikuwa wamejaa kwenye feri bila kujua nini kitatokea mbeleni
 
Issue si kwamba sijui kusoma. Utawekaje habari in piecemeals utegemee watu wapoteze muda kufuata mparaganyiko wako? Kama unaona wewe ni bingwa wa matatizo basi nenda kawasaidie badala ya kupayuka tu. Right?
Ni kweli jamaa kakosea kuweka post yake kivipande vipande, lakini makosa yake hayawezi kuyafanya makosa yako yawe sawa. Nashauri 'ukonsentreti' kwenye kilichomo badala ya jinsi kilivyo. Na uliyeianzisha mada hii nawe wakati mwingine tuwekee mambo yako kwenye post moja badala ya vipande vipande. M'barikiwe nyote....
 
Hakuna la maaana uliloandika zaid ya kujisifia uliza sababu na ujue undan wake c kuropoka tu huna point kajipange
 
hueleweki we nyangumi, wakusanye familia yako sebuleni kwako then uwasomee huu upumbavu wako labda hao ndio watakuelewa..!!!
 
mtoa mada kagawanya mada yake kwenye posts tofauti, hiyo post yake ya mwisho hapo juu inaelezea ushauri wake....
 
Nimejaribu kupitia post zako nikaona mtzamo ulionao kwa bahat mbaya niliangalia tbc ambao wako biased cna sana suala la polis kupiga watu walio kwenye panton si la kushabikia hata kidogo inawezekana hata watu wasio wanafunzi wakaangukia majini,suala la
kuwashikisha adabu vibaka nakubali kabisa ila tahadhari ni kua mara nyingi mkaz wa eneo akiuwawa unatokea uhasama mkubwa wa kuendeleza mauaji mfano refer wanakjj wa changanyikeni na chuo kikuu mzumbe miaka ile,na mwisho mkuu inabidi uanze kufuta kale ka ideology ka u pcm na u pcb kwa kua ugumu wa elimu si kipimo cha mafanikio, katka lyfe kila
zama zina wakat wake ni hayo tu.
 
Wanafunzi wapo kuxoma na c kulpiza visasi kwa Raia na ndo maana kuna Police kuwalinda ni jukumu lao nawapongeza kwa uamuz waliofanya na c kuchukua sheria mkononi fikirin kabla ya kuandika
 
ya Kigamboni ni magumu kuliko unavyofikiri: kigamboni ni nchi isiyo na serikali, hata raia wa kawaida hubakwa na kuporwa mali zao mchana kweupe bila kupata msaada wowote sembuse hawa watoto wa "chips na broiler?".
 
unaongelea mazigira gani ambayo yako kigamboni? ina maana hata wewe unashabikia ujinga waliufanya jana hawa jamaa? inakuwaje mnakaa kwenye feri bila kuwa na tahadhari ya kuwa polisi wanaweza kubadilikia na kuwapa kichapo na je, munaweza kujinasua kwa njia ipi? hilo nalo linahitaji uende chuo kikuu? kufanya ulinzi kwenye mabweni yao au mazingira yanayo wazunguka nayo inabidi waende kozi? tusiwe wavivu au washabiki wakusahabikia ujinga bila kuja na nini kifanyike

fujo inasemekana wanafunzi walienda polisi wakati kina kova wanataka waende uwanja wa machava ndio shughuli ya kuwaondoa kituoni kuwa hamishia machava ndio iliyotokea..
 
binafsi nakuunga mkono kwa point yako ya kupinga hao wanachuo kujazana kwenye kivuko kwa lengo lao la kushinikiza madai yao. uko sahihi kabisa. tatizo langu topic yako iko vipande vipande...ungeiweka pamoja katika para. pili sioni kama ni sawa kulinganisha mazingira ya Mbeya na Dar...mazingira na watu ni tofauti katika maeneo hayo mawili. otherwise concern yako ni sawa!

hili la kivuko walikuja wakavuka au kuna wengine walibaki kivukoni kweli au ndio TBC habari ilipoishia..
 
safi sana wewe mkuu angalia mziki tuliokuwa tunaufanya pale MTC mwizi au kibaka akimatwa lazima ateje aliemleta pale chuoni na kama hajataja kichapo kama kawaida na baadaye tulikuwa tunawapeleka polisi lakini ameshalowa jiti kama kawaida na hata akitaja lazima akirudi mitaani anaalama za MTC kichwani kwa kutumia nyembe kichwa kinaandikwa MTC

hawa wa siku hizi walivyo nyoro nyoro,wataweza kweli,maana wamelegea mpaka basi
 
maisha magumu kweli unapewa bum bado unavamiwa wanakupeleka had ATM wanatoa hela zako zote Kwny ATM hakuna walinzi uktoa taarifa police unaambiwa tutafatilia unategemea nn hapo kk

Wanachuo acha kuwa legelege hasa nyie wa kiume, acha usingizi polisi wameshindwa kuwalinda jipangie zamu ninyi kwa ninyi njilinde wakati mnatafuta suluhu ya usalama wenu. Kipindi sisi tunasoma tulikuwa nusu askali aingii mtu kichwa kichwa chuoni, tulijilinda wanyewe.
 
kwanza napenda nitoe historia ya MTC kidogo MTC ni chuo kilichokuwa kinaundwa na kozi zifuatacho: Mechanical, Electrical, Civil, na Architecture engineering japo ilikuwa ni elimu ya Fundi mchundo lakini ilikuwa nielimu ya Chuo kikuu kwa 75%. kwanini nasema hivyo? kwa sababu wanafunzi walikuwa huru sana hatukuwa na uniform za kuvaa tulikuwa tunaishi maisha ya raha mastarehe kama kufikwa (kuleta mwamke/msichana) ilikuwa ni ruksa na ilikuwa ni fahari kwa mkuu wetu wa chuo kipindikile Mzee Zuberi. Masomo yalikuwa magumu sana na tulikuwa tunaandaliwa sikuendelea na shule bali kwenda kufanya kazi. Maana kipindikile kwenda Chuo Kikuu bila na kuwa na B ya mathematics na at least masomo yako wastani wake lazima uwe C huwezi pata. Nje ya hapo kuapata hata cheti ilikuwa ngumu umesoma miaka yako 3 kwa kuruka viunzi kila term na mitihani yake ukifail nyumbani na mwishoni sasa unakusanya material yote ya mwaka wa kwanza unafanyia mtihani wa kwa masaa 3. Si hivyo tu ukipata "A" 5 kati ya masomo 6 ukafail moja hupati cheti na ukirudia mtihani ukafail mara 2 basi cheti hupati milele, ilikuwa ni bora kupata "D" zote iliuweze kuchukua cheti. Lakini istoshe kuipata hata 'D" haikuwa rahisi maana range yake D=(50-69), C=(70-79) B=(80-89) A=( 90-100)haikuwa rahisi sana wadau kuweza kuendelea na chuo kikuu au hata elimu ya juu

tulikandamizwa, sikuhizi unaendelea tu na masomo hata kama una 'F'
 
Wanamitindo na wasanii ndo wamejazana vyuoni kazi kula chips na yale makuku ya kisasa basi wamekuwa lainiiii!!unapigwa mti kihasara hasara mtoto wa kiume?
 
binafsi nakuunga mkono kwa point yako ya kupinga hao wanachuo kujazana kwenye kivuko kwa lengo lao la kushinikiza madai yao. uko sahihi kabisa. tatizo langu topic yako iko vipande vipande...ungeiweka pamoja katika para. pili sioni kama ni sawa kulinganisha mazingira ya Mbeya na Dar...mazingira na watu ni tofauti katika maeneo hayo mawili. otherwise concern yako ni sawa!
kwa hili hakuna kujitetea kwa kusema "mazingira hayafanani" basi kama ni hivyo nyie hamfai kuwa wapiganaji, kwa mpiganaji hakuna cha mazingira. mimi nilikuwa Tanga Technical zamani, tulikuwa tunapaita Kiungani, hapakuwa na askari wa kulinda shule lakini eneo la shule hakatizi mtu, anaweza kufa, na mabweni hayafungwi mulango tukiwa madarasani.
 
Back
Top Bottom