Wanafunzi wa IFM fanyeni haya kama mnataka kuishi salaama

Nikushauri tu mwandishi.jaribu kuandika lengo la andiko lako kabla ya kufanya masimulizi ya wapi ulisoma n.k,Utangulizi wako hauendani na andiko zima.
 
Jana kama wengi wetu tuliamka salaama sana nakuenda kwenye mishe mishe za maisha kama kawaida. Lakini kunamdau alitupa taarifa ya kilichokuwa kinaendelea IFM. Tunashukuru kwa taarifa. Na baadaye niliona kwa macho kwenye ITV taarifa ya saa 2 usiku wanafunzi walivyokuwa wamefunga barabara na kuingia kwenye feri zaidi ya wanafunzi 600. Kweli ummoja ulinipa matumaini sana lakini cha ajabu ni pale nilipoona wanafunzi walipoanza kutembezewa mkong'oto na polisi hadi wengine kutemebelea magoti. Niliona ajabu sana tena nilitokwa na machozi hadi naandika hapa sijalala nikifikiria jinsi ya kuwasaidia hawa wadogo zetu aka waliokimbia hand education nakuingia kwenye soft education. fuatilia post zangu hapa

kwanini nasema hawa jamaa walikimbilia kwenye soft education kwa kuwa wao akili zao zinawaza sana kuwa karibu na fedha ndio maisha. Lahasha mimi siamini, lakini cha ajabu zaidi hawa wataalam wa balance sheet akili zao zote nazani zimekaa kubalance zaidi nje ya kufikiria nini cha kufanya hata kwenye jambo ambalo ni ngumu kwenye maisha yao. Pengine naungana na mbunge wa Iringa mjini Mchungaji Msingwa wameruhusu akili ndogo kuongoza akili kubwa. Hii halina ubishi kwa chuo kama IFM chukulia jana tu walivyokuwa wameng'ang'ania kwenye feri zaidi ya wanafunzi 600 lakini bila kujua kuwa mbele au feri ilkuwa kwenye maji (bahari).Je kweli waliona madahara ambayo yange wapata? na matokeo yake shemeji zao aka polisi waliwakamua kama hawana akili nzuri maana hawakuwa na pakukimbilia.

kwa nini nasema hivyo? Je, wazazi walio na watoto wao wakiume/wakike wanao rawitiwa, kubakwa, na pengine kupigwa nondo unazani wanajisikiaje kusikia matukio kama haya? Je, IFM hakuna wazazi walio olewa/kua. hakuna wachumba wanaosoma pale wakiwa na wenza wao nje ya chuo? Je, akisikia kuna mambo kama haya je, jamii inawachukuliaje? sipendi kuamini kama mimi hapa nilivyo na huzuni ila ninaimani ni wengi sana tena mamia ya watanzania wanahuzuni kama mimi hapa kutokana na nilichokiona jana na kukisika masikioni mwangu. Swali, Je, tunaandaaa jamii ya aina gani on the future?

mimi sio mwanataalum wa uandishi naomba niende kwenye point. Kwanza kabla sijaja kwenye nini kifanyike naomba tu kama kuna mzazi/mlezi/mchumba/mme/mke/kaka/dada/mjomba nk. humu anamtoto yuko IFM basi kuna haja ya kuniunga mkono wale watoto walitakiwa kuchapwa viboko kama sio kibao. Kwa nini nasema hivyo? Chukulia sisi tulikuwa tunasoma Mbeya Technical college (MTC) miaka ya nyuma huko leo hii Mbeya University of Science and Technology (MUST). Sikuweza kuona ujinga kama huu, hata pale UDSM, sijawahi sikia ujinga kama huu. sikatai vibaka wapo sawa kila sehemu ya nchi yetu kama si Afrika kwa ujumla.Mwanataluma nijuavyo mimi ni askari kwa akili aliyonayo anaweza fanya upeleleza, anaweza kujilinda yeye kama yeye, anaweza fundisha jamii kutoka na taaluma yake? Je, kwa kinachotokea IFM twaweza pata nini sisi wanajamii? ni maadili au? sinakumbukumbu sana kama sijakosea hata mwezi haujapita nilisikia redioni watoto wakike wanaandamana kupinga kuzuiliwa kuvaa nguo fupi sijui ni IFM au nichuo kingine lakini kumbukumbu zangu ni kama IFM leo hii ndio wanakuja na ujinga kama huu kuna haja yakubaidilika kabisa kiakili, maadili hata kimuonekano.

Sisi kipindi kile tunasoma pale MTC tulikuwa na ummoja wa hali ya juu sana ninaimani kama kuna wanaMTC humu watakubaliana na mimi haswa wa miaka ya nyuma sio leo. Chuo cha MTC kiko kama 4km kutoka Inyunga barabara ya mbeya Tunduma nakiko nje ya mji yaani kwa kifupi naweza sema ni porini. lakini sijawahi sikia mwanafunzi kapingwa nondo, kabakwa, karawitiwa. wizi wa kuibiwa kwenye mabweni ulikuwa wa nadra sana tena wezi walikuwa wanashiirkiana na wanafunzi wenzetu. Lakini ninakwambia hata kama suruali au kiatu kimeibiwa zaid ya mwezi kilikuwa kinapatiaka kwa njia nitakazo zitaja hapo mbeleni.

Wewe mleta mada unajua unachangia hoja za enzi za ujima, jiulize kama wewe na elimu yako hiyo leo hii ulawitiwe kisawasawa yaani ndembendembe utapata kuandika hizo ngonjera zako?
 
binafsi nakuunga mkono kwa point yako ya kupinga hao wanachuo kujazana kwenye kivuko kwa lengo lao la kushinikiza madai yao. uko sahihi kabisa. tatizo langu topic yako iko vipande vipande...ungeiweka pamoja katika para. pili sioni kama ni sawa kulinganisha mazingira ya Mbeya na Dar...mazingira na watu ni tofauti katika maeneo hayo mawili. otherwise concern yako ni sawa!

Kwa sehemu kubwa sana ninaungana na mwanaweja katika maoni na ushauri wake juu ya kadhia hii ya IFM.

Hapo kwenye red; Hiyo ni kujidanganya na ndio sababu ya kuendelea kuibiwa kila mara na kama haitoshi sasa jamaa wameamua kuwafumua tigo watoto wa kiume, hiyo ni dharau kubwa sana na kitendo hicho kilitosha kuwafanya wanafunzi wa IFM kuonyesha hasira zao halisi kivitendo.

Talking of mazingira ya dar na mbeya ni tofauti ni kweli lakini vitendo wanavyofanyiwa hao wanafunzi wa IFM havitofautiani sana na hivyo vilivyokuwa vikifanyika mbeya tech.

Nitakupa mfano wa matukio kama hayo, ya wizi yalikuwa yakitokea sana DIT. Kila mara watu walikuwa wanaibiwa nguo, viatu, simu na vitu vingine vya thamani, na pale jirani ya chuo upande wa hospitali ya regency kulikuwa na police post. Sasa maajabu ni kwamba wizi ulikuwa unafanyika zaidi block 5 ambalo liko karibu kabisa na police post.

Sasa tulipoazimia kuanzisha msako kwa wezi na vibaka tulikuja kubaini kwamba wezi na vibaka waliokuwa wakituibia walikuwa wanatoka nje ya chuo lakini walikuwa wanaletwa na wenyeji wao ambao walikuwa ni wanafunzi wenzetu. Katika saka saka hiyo tulimkamata mwanafunzi mwenzetu akishirikiana na hao wezi tena alikuwa ni muajiriwa wa jeshi la polisi, alikuwa ni constable wa police ndipo tulibaini ni kwanini police walio jirani yetu hawachukui hatua za kuimarisha ulinzi chuoni kwetu pamoja na kuwa wako jirani sana lakini tunaibiwa kila mara. Baada ya kumtembezea kichapo cha kueleweka ndipo akatuomba sana msamaha na kufichua mbinu zao za wizi na muda wanaokuja kuiba. Walikuwa wanavizia muda ambao wanafunzi wengi kama sio wote tuko madarasani.

Baada ya kupata taarifa hiyo tukaanza kuweka mitego na haukupita muda mrefu tukamnasa mwizi akiwa juu ghorofa ya tatu block five amekusanya viatu milangoni na anataka kusepa, nakumbuka siku hiyo tulikuwa tunafanya mitihani ya kumaliza mhula na baadhi yetu tulikuwa tunafanyia mitihani dinning hall. Ziliposikika kelele za mwizi watu wote wakakimbilia blok 5 na baada ya muda mfupi yule kibaka akawa ametoka mjengoni anakimbia kuparamia ukuta jirani na dinning hall na block five. Bila kutarajia watu walikurupuka kutoka chumba cha mtihani na kumvamia kibaka yule alipigwa katika kipindi kifupi sana kadri ya dakika 5 hadi 10 alikuwa ameshapoteza uhai. Wale polisi waliposikia purukushani na kuja kuona kulikoni walikuta maiti tu huku wanafunzi tukiwa tumeshatawanyika kuendelea na mitihani na wengine kuendelea na shughuli zao.

Na siku nyingine baada ya muda tena aliuawa kibaka mwingine jioni jioni akiwa ameiba vitu mbalimbali block 4 alipigwa na kufariki papo hapo. Tangia hapo hadi naondoka DIT takribani miaka miwili baadae hakukuwahi kutokea wizi tena katika hosteli zetu. Kwahiyo kwa ufupi anachoshauri Mwanaweja ndio njia pekee ya kupambana na hao vibaka wanaowavamia kila siku huko kigamboni. Kwa uzoefu wangu wa kuishi kigamboni polisi wanashirikiana na wahalifu na sishangai kusikia kwamba pamoja na kutoa ripoti kila mara kituo cha kigamboni bado ocd ameshindwa kuwajibika kutekeleza wajibu wake wa kuwapatia ulinzi ninyi wenyewe na mali zenu.
 
Last edited by a moderator:
umesoma post zangu na kuzielewa au? mbona mnapenda kuatafuniwa kila kitu?
Mkuu nimekusoma, usiwajibu wale wote watakao kuwa wanauliza maswali ya ku'kuprovock'. Jibu maswali/ hoja zenye mlengo wa kutaka kueleweshwa tu!
 
kaeleza mengi tu. ila kwa kifupi anahubiri sera ya jino kwa jino!

Mkuu umoja na ushirikiano wa namna hii aliouleza Mwanaweja ndiyo hasa umewasaidia waendesha pikipiki wengi nchini. Kipindi cha nyuma kulikuwa na ajali nyingi zinazohusisha waendesha pikipiki. Ni kweli baadhi ya ajari hizi zilikuwa zinatokana uelewa mdogo wa sheria za barabarani kwa madereva wa pikipiki. Lakini ni ukweli usiopingika kuwa waendesha pikipiki walikuwa wanaonewa na madereva wa magari ndiyo maana ajari zilikuwa nyingi sana.

Sasa hivi mgonge au msababishie ajari kwa makusudi mwendesha pikipiki uone tifu/kichapo utakachoshushiwa na maderava wa pikipiki. Siku hizi ajari zimepungua kiasi kutokana na umoja na ushirikiano wao.
 
Last edited by a moderator:
kwa hili hakuna kujitetea kwa kusema "mazingira hayafanani" basi kama ni hivyo nyie hamfai kuwa wapiganaji, kwa mpiganaji hakuna cha mazingira. mimi nilikuwa Tanga Technical zamani, tulikuwa tunapaita Kiungani, hapakuwa na askari wa kulinda shule lakini eneo la shule hakatizi mtu, anaweza kufa, na mabweni hayafungwi mulango tukiwa madarasani.
kwaa kusema mazingira ya mbeya na Dar ni tofauti sijamaanisha kwamba wanachuo wa IFM hawapaswi kujiwekea mfumo wa ulinzi. nina maana tofauti kabisa. hebu rudia kusoma topic ya mhusika na comment yangu, utaelewa!
 
Zuberi, hahahaa, Zee jinga sana hili..... Hihihiii. Mzee Mtu wa Tanga, matusi kama mbeba zege. Namfahamu akiwa TCA.

Kuna siku alikuwa akimpiga Mkwara Matron wa bweni la Wasichana "Matron, unahangaika na hawa wa nini? Wote hawa bikira walishapoteza siku nyingi sana. Kama huamini twende sasa hivi tukahakikishe....." Sasa sijui alitaka kuhakikisha vipi?

Siku nyingine akatoa nyingine mpya akimwambia Mzee Issa Mushi kuwa "Mwalimu, sishangai vitanda hivi vya wanafunzi vinaharibika haraka. Ikifika weekend, pale getini wanapita Wasichana wazuri, mmmmmhhh Wazuri jamani, mhh mhh mhh wazuri hao. Sasa hapo vitanda kweli vitadumu?" Watu hawana mbavu.

Kuna sherehe akaalikwa kama Mgeni Rasmi kufungua party na akaja bila mwanamke na akatupa kali ya mwaka "mnaniona mie mwalimu hapa, NINA UKAME..... hivyo inabidi mnipe mtu wa kucheza naye....." lohhhh. Nasikia akiwa Mbeya akaanza kuchukua Mke wa mwalimu mwenzake, kuna ukweli hapo? Hadi leo nina picha yake sehemu fulani kama sikosei.

Mzee Zuberi, mhandisi wa Ujenzi na Viroja viingi.
kwanza napenda nitoe historia ya MTC kidogo MTC ni chuo kilichokuwa kinaundwa na kozi zifuatacho: Mechanical, Electrical, Civil, na Architecture engineering japo ilikuwa ni elimu ya Fundi mchundo lakini ilikuwa nielimu ya Chuo kikuu kwa 75%. kwanini nasema hivyo? kwa sababu wanafunzi walikuwa huru sana hatukuwa na uniform za kuvaa tulikuwa tunaishi maisha ya raha mastarehe kama kufikwa (kuleta mwamke/msichana) ilikuwa ni ruksa na ilikuwa ni fahari kwa mkuu wetu wa chuo kipindikile Mzee Zuberi. Masomo yalikuwa magumu sana na tulikuwa tunaandaliwa sikuendelea na shule bali kwenda kufanya kazi. Maana kipindikile kwenda Chuo Kikuu bila na kuwa na B ya mathematics na at least masomo yako wastani wake lazima uwe C huwezi pata. Nje ya hapo kuapata hata cheti ilikuwa ngumu umesoma miaka yako 3 kwa kuruka viunzi kila term na mitihani yake ukifail nyumbani na mwishoni sasa unakusanya material yote ya mwaka wa kwanza unafanyia mtihani wa kwa masaa 3. Si hivyo tu ukipata "A" 5 kati ya masomo 6 ukafail moja hupati cheti na ukirudia mtihani ukafail mara 2 basi cheti hupati milele, ilikuwa ni bora kupata "D" zote iliuweze kuchukua cheti. Lakini istoshe kuipata hata 'D" haikuwa rahisi maana range yake D=(50-69), C=(70-79) B=(80-89) A=( 90-100)haikuwa rahisi sana wadau kuweza kuendelea na chuo kikuu au hata elimu ya juu
 
binafsi nakuunga mkono kwa point yako ya kupinga hao wanachuo kujazana kwenye kivuko kwa lengo lao la kushinikiza madai yao. uko sahihi kabisa. tatizo langu topic yako iko vipande vipande...ungeiweka pamoja katika para. pili sioni kama ni sawa kulinganisha mazingira ya Mbeya na Dar...mazingira na watu ni tofauti katika maeneo hayo mawili. otherwise concern yako ni sawa!
Lakini hawa IFM wanaojiita watoto wa mjini naona ndo wametumia mbinu za zamani halafu itakuaje mtoto wa mjini udhibitiwe kirahisi vilewangekuwa wa bush si wangekufa kabisa,hili la matukio ya kulawitiwakidogo ni gumu kulielewa mazingira gani huwa yanatokea haya mattizo labda watueleshe zaidi ili tuweze changia maada.Mtoa maada kanifurahisha inaonekana vijana wa MTC thinking ilikuwa kubwa maana mlijua kuwa mkitangulia tu kuingia ukumbini mgedhibitiwa kirahisi.Mwisho maada yake pia kuielewa inahitaji ufikiri kidogo ukitumia vionjo tu utaishia kusema sijaona kitu
 
Lakini hawa IFM wanaojiita watoto wa mjini naona ndo wametumia mbinu za zamani halafu itakuaje mtoto wa mjini udhibitiwe kirahisi vilewangekuwa wa bush si wangekufa kabisa,hili la matukio ya kulawitiwakidogo ni gumu kulielewa mazingira gani huwa yanatokea haya mattizo labda watueleshe zaidi ili tuweze changia maada.Mtoa maada kanifurahisha inaonekana vijana wa MTC thinking ilikuwa kubwa maana mlijua kuwa mkitangulia tu kuingia ukumbini mgedhibitiwa kirahisi.Mwisho maada yake pia kuielewa inahitaji ufikiri kidogo ukitumia vionjo tu utaishia kusema sijaona kitu

vijana wa siku hizi ni dot.com...unadhani kula chips zilizokaangwa kwa mafuta mixed na mafuta ya transformer na kuku walioteshwa kwa wiki tatu tu...nguvu ya mwili zitakuwa dhaifu pia! chakula ugali wa mahindi yasiyokobolewa (dona) ndo mpango mzima!
 
Back
Top Bottom