Wanafunzi wa IFM fanyeni haya kama mnataka kuishi salaama

Mwanaweja

JF-Expert Member
Feb 8, 2011
3,575
523
Jana kama wengi wetu tuliamka salaama sana nakuenda kwenye mishe mishe za maisha kama kawaida. Lakini kunamdau alitupa taarifa ya kilichokuwa kinaendelea IFM. Tunashukuru kwa taarifa. Na baadaye niliona kwa macho kwenye ITV taarifa ya saa 2 usiku wanafunzi walivyokuwa wamefunga barabara na kuingia kwenye feri zaidi ya wanafunzi 600. Kweli ummoja ulinipa matumaini sana lakini cha ajabu ni pale nilipoona wanafunzi walipoanza kutembezewa mkong'oto na polisi hadi wengine kutemebelea magoti. Niliona ajabu sana tena nilitokwa na machozi hadi naandika hapa sijalala nikifikiria jinsi ya kuwasaidia hawa wadogo zetu aka waliokimbia hand education nakuingia kwenye soft education. fuatilia post zangu hapa

kwanini nasema hawa jamaa walikimbilia kwenye soft education kwa kuwa wao akili zao zinawaza sana kuwa karibu na fedha ndio maisha. Lahasha mimi siamini, lakini cha ajabu zaidi hawa wataalam wa balance sheet akili zao zote nazani zimekaa kubalance zaidi nje ya kufikiria nini cha kufanya hata kwenye jambo ambalo ni ngumu kwenye maisha yao. Pengine naungana na mbunge wa Iringa mjini Mchungaji Msingwa wameruhusu akili ndogo kuongoza akili kubwa. Hii halina ubishi kwa chuo kama IFM chukulia jana tu walivyokuwa wameng'ang'ania kwenye feri zaidi ya wanafunzi 600 lakini bila kujua kuwa mbele au feri ilkuwa kwenye maji (bahari).Je kweli waliona madahara ambayo yange wapata? na matokeo yake shemeji zao aka polisi waliwakamua kama hawana akili nzuri maana hawakuwa na pakukimbilia.

kwa nini nasema hivyo? Je, wazazi walio na watoto wao wakiume/wakike wanao rawitiwa, kubakwa, na pengine kupigwa nondo unazani wanajisikiaje kusikia matukio kama haya? Je, IFM hakuna wazazi walio olewa/kua. hakuna wachumba wanaosoma pale wakiwa na wenza wao nje ya chuo? Je, akisikia kuna mambo kama haya je, jamii inawachukuliaje? sipendi kuamini kama mimi hapa nilivyo na huzuni ila ninaimani ni wengi sana tena mamia ya watanzania wanahuzuni kama mimi hapa kutokana na nilichokiona jana na kukisika masikioni mwangu. Swali, Je, tunaandaaa jamii ya aina gani on the future?

mimi sio mwanataalum wa uandishi naomba niende kwenye point. Kwanza kabla sijaja kwenye nini kifanyike naomba tu kama kuna mzazi/mlezi/mchumba/mme/mke/kaka/dada/mjomba nk. humu anamtoto yuko IFM basi kuna haja ya kuniunga mkono wale watoto walitakiwa kuchapwa viboko kama sio kibao. Kwa nini nasema hivyo? Chukulia sisi tulikuwa tunasoma Mbeya Technical college (MTC) miaka ya nyuma huko leo hii Mbeya University of Science and Technology (MUST). Sikuweza kuona ujinga kama huu, hata pale UDSM, sijawahi sikia ujinga kama huu. sikatai vibaka wapo sawa kila sehemu ya nchi yetu kama si Afrika kwa ujumla.Mwanataluma nijuavyo mimi ni askari kwa akili aliyonayo anaweza fanya upeleleza, anaweza kujilinda yeye kama yeye, anaweza fundisha jamii kutoka na taaluma yake? Je, kwa kinachotokea IFM twaweza pata nini sisi wanajamii? ni maadili au? sinakumbukumbu sana kama sijakosea hata mwezi haujapita nilisikia redioni watoto wakike wanaandamana kupinga kuzuiliwa kuvaa nguo fupi sijui ni IFM au nichuo kingine lakini kumbukumbu zangu ni kama IFM leo hii ndio wanakuja na ujinga kama huu kuna haja yakubaidilika kabisa kiakili, maadili hata kimuonekano.

Sisi kipindi kile tunasoma pale MTC tulikuwa na ummoja wa hali ya juu sana ninaimani kama kuna wanaMTC humu watakubaliana na mimi haswa wa miaka ya nyuma sio leo. Chuo cha MTC kiko kama 4km kutoka Inyunga barabara ya mbeya Tunduma nakiko nje ya mji yaani kwa kifupi naweza sema ni porini. lakini sijawahi sikia mwanafunzi kapingwa nondo, kabakwa, karawitiwa. wizi wa kuibiwa kwenye mabweni ulikuwa wa nadra sana tena wezi walikuwa wanashiirkiana na wanafunzi wenzetu. Lakini ninakwambia hata kama suruali au kiatu kimeibiwa zaid ya mwezi kilikuwa kinapatiaka kwa njia nitakazo zitaja hapo mbeleni.
 
Sasa bandugu unatoa ushauri au unauliza maswali?
au ndo ushauri kwa njia ya maswali.
 
kwanza napenda nitoe historia ya MTC kidogo MTC ni chuo kilichokuwa kinaundwa na kozi zifuatacho: Mechanical, Electrical, Civil, na Architecture engineering japo ilikuwa ni elimu ya Fundi mchundo lakini ilikuwa nielimu ya Chuo kikuu kwa 75%. kwanini nasema hivyo? kwa sababu wanafunzi walikuwa huru sana hatukuwa na uniform za kuvaa tulikuwa tunaishi maisha ya raha mastarehe kama kufikwa (kuleta mwamke/msichana) ilikuwa ni ruksa na ilikuwa ni fahari kwa mkuu wetu wa chuo kipindikile Mzee Zuberi. Masomo yalikuwa magumu sana na tulikuwa tunaandaliwa sikuendelea na shule bali kwenda kufanya kazi. Maana kipindikile kwenda Chuo Kikuu bila na kuwa na B ya mathematics na at least masomo yako wastani wake lazima uwe C huwezi pata. Nje ya hapo kuapata hata cheti ilikuwa ngumu umesoma miaka yako 3 kwa kuruka viunzi kila term na mitihani yake ukifail nyumbani na mwishoni sasa unakusanya material yote ya mwaka wa kwanza unafanyia mtihani wa kwa masaa 3. Si hivyo tu ukipata "A" 5 kati ya masomo 6 ukafail moja hupati cheti na ukirudia mtihani ukafail mara 2 basi cheti hupati milele, ilikuwa ni bora kupata "D" zote iliuweze kuchukua cheti. Lakini istoshe kuipata hata 'D" haikuwa rahisi maana range yake D=(50-69), C=(70-79) B=(80-89) A=( 90-100)haikuwa rahisi sana wadau kuweza kuendelea na chuo kikuu au hata elimu ya juu
 
MTC tulikuwa nasehemu takatifu aka "KIZOTA" yaani sehemu iliyokuwa free kuongea kitu chochote na point zilikuwa zinachukuliwa na mwenyekiti wa siku ile ya kikao na muunganiko wa mawazo yetu yalikuwa yana heshimika sana na majina tuklikuwa hatuitani bali tulikuwa tunatumia "MJUMBE" kwa hiyo katika hili lilitusaidia sisi kufahamiana idadi yetu ilikuwa kama 150 tu. lakini tulikuwa nauumoja ambao sijawahi uona kwenye vyuo hadi leo

Nasema hivyo kutokana na matukio kadhaa tuliyoyafanya. natoa mifano michache tu 1. mwenzetu akionewa haijalishi ninani kamuonea na wapi iwe kwenye elimu, (academic issue), kwenye usafiri, (hiace), mitaani, Chuoni, polisi, tulikuwa tunaunganika au kukusanyika KIZOTA mara moja bila kuajili ni muda gani, usiku mchana, tuko kwenye mitihani, tuko darasana, na nani anafundisha, na njia tuliyokuwa tunatumia ni kipenga tu mwenye taarifa anapiga kipenga wote walioko mabwenini, madarasani kila kona wanakimbia kwenda KIZOTA na na aliyepuliza Kipenga anatoa maada (Tatizo) haraka wajumbe wanachangia hoja zinazopita zinafanyiwa analysis nakuja na nini kifanyike na kwa wakati gani

Nakumbuka tulikuww na na dhali/tifu na polisi wa mkoa wa mbeya kipindi kile RCO alikuwa Sanya alikuja chuoni tulimkatalia kututanguliza kuingia wanafunzi ndio yeye aje nyuma yetu kwenye bwalo. Ilibidi aingie yeye kwanza na polisi wenzake ndio sisi tukaja nyuma yake na tulikaa mlangoni.wao walikuwa mbele chochote kikitokea tutoke kabla yao. Na ungomvi ulikuwa wawanawake ilionekana polisi walikuwa wanazidiwa na wanafunzi kuchukua madem mitaani wakaanzisha ungomvi na wanachuo. huo ungomvi ulipelekea kuleta fujo tuliamua kwenda kuwatoa wenzetu kitu cha polisi Iyunga kwa kuvamia nakuwatoa ninaimani kama kuna mwana MTC humu atakubaliana na mimi movie tulizokuwa tunazifanya zilikuwa za 99% katika ufanisi sikupiga daladala haswa wale madreva na makonda wakorofi, vibaka, nk.
IFM jana walichokuwa wanakifanya walistahili kipingo maana walikuwa wametangulizwa na polisi mbele yao kulikuwa na bahari angalia huu ujinga kwa hiyo polisi walijua hawa sio wanataluma hawajui hata jinsi ya kujinasua kwa hilo tu IFM mlionyesha udhaifu wa hali ya juu sana. mwanajeshi anapopambana sehemu yeyote kitu cha kwanza kujiuliza ni je kama nikishinwa nitakimbilia wapi. Nyie hizo akili ua wazo hilo hamkuwa nalo kabisa ndio maana polisi waliwapigisha kwata kama wototo wadogo hadi kutembelea magoti ni aibu, chukulia mchumba wako, mke wako, baba yako anakuona unatembelea magoti kiasi kile inatia huruma sana na inaleta fedheha kwenye jamii mmezalilisha fani yenu sana jana acheni usister du, brothermen kwenye mambo ya muhimu natumieni akili kukabiliana na majnga kama hayo

ushauri wangu kwa wana IFM: Naomba kwanza muanzie ndani ya jamii yenu kusaka wale wanaowasaliti kwa kuleta kibaka kwa nini nasema hivyo haiwezekani taasisi ya watu 600 isumbuliwe na vibaka wa wachache kiasi kama hicho.Inamaana kunawenzenu wanwasliti ndani kwa kushirikiana na vibaka.
2. Jamani mbona mnakuwa kama sio watoto wa jiji? kamateni vibaka wote kwenyemitaa yenu watawaeleza tu nani anafanya ujinga kama huo weka selo hapo kwenu hostel na kamuani kama hamna akili nzuri watasema tu ukweli. Na kuwakamata hao vibaka ni rahisi mno tafuteni waschana hata wanaume weka kielf tano tu mahali peupe lakini hapo muwe mmezanga mitaani kwa wingi kila sehemu ili tu kibaka akikwapua anzeni naye. hapa lazima muwe mnajua nje ya hapo mtapigana nyie kwa nyie inabidi muwe na lugha mmoja aun neno mmoja la kuwatambulisha kama sisi tulikuwa tunatumia "MJUMBE"
3. hakikisheni mnafanya ulinzi wa kila aina nayeyote anayeingia kwenye chuo chenu lazima afahamike nani kamleta hapo au kafuata nini na hii ni rahisi tu mkiwa na lugha mmoja ukimwita kwa mfano "MJUMBE" yuko kimya utajua huyu ni mamluki kwa hiyounaanza kumfuatilia anaingia kwa nani na nichumba gani.
4. Siri ni kingizezo muhimu sana kataka mafanikio hata nyie kuweni wasiri katika yote mnayoyafanya
5. Msikimbilie polisi, polisi ndio hao hao wanaokula pamoja na vibaka, polisi watakuja kuwatafuta nyie mtakapo kuwa mmesurubu mmoja wa vibaka hao. kweli ninamengi ila naomba niishie hapa kwa maswali uliza niotajibu na nitatoa njia mbandala. Asnte sana na poleni kwa yaliowapata na masomo mema
 
Mbona hayo uliyotaka wafanye hayaonekani au ulipitiwa? Je wafanye yepi hayo ili wafanikiwe?
Jana kama wengi wetu tuliamka salaama sana nakuenda kwenye mishe mishe za maisha kama kawaida. Lakini kunamdau alitupa taarifa ya kilichokuwa kinaendelea IFM. Tunashukuru kwa taarifa. Na baadaye niliona kwa macho kwenye ITV taarifa ya saa 2 usiku wanafunzi walivyokuwa wamefunga barabra na kuingia kwenye feri zaidi ya wanafunzi 600. Kweli ummoja ulinipa matumaini sana lakini cha ajabu ni pale nilipoona wanafunzi walipoanza kutemezewa mkong'oto na polisi hadi wengine kutemebelea magoti. Niliona ajabu sana tena nilitokwa na machozi hadi naandika hapa sijalala nikifikiria jinsi ya kuwasaidia hawa wadogo zetu aka waliokimbia hand education nakuingia kwenye soft education. fuatilia post zangu hapa
 
boring & pointless! topic yako hujaipangilia vizuri. halafu mazingira uliyosomea na mazingira ya huko Kigamboni mbona ni tofauti! pia nyakati ni tofauti - kipindi wewe unasoma na kipindi hiki cha hao wanachuo wa IFM. things are dynamic, they are not static as you think! so try to be dynamic...
 
boring & pointless! topic yako hujaipangilia vizuri. halafu mazingira uliyosomea na mazingira ya huko Kigamboni mbona ni tofauti! pia nyakati ni tofauti - kipindi wewe unasoma na kipindi hiki cha hao wanachuo wa IFM. things are dynamic, they are not static as you think! so try to be dynamic...
si kila kinachoandikwa humu utakipenda na si kila unachokipenda kitaandikwa humu
 
boring & pointless! topic yako hujaipangilia vizuri. halafu mazingira uliyosomea na mazingira ya huko Kigamboni mbona ni tofauti! pia nyakati ni tofauti - kipindi wewe unasoma na kipindi hiki cha hao wanachuo wa IFM. things are dynamic, they are not static as you think! so try to be dynamic...

unaongelea mazigira gani ambayo yako kigamboni? ina maana hata wewe unashabikia ujinga waliufanya jana hawa jamaa? inakuwaje mnakaa kwenye feri bila kuwa na tahadhari ya kuwa polisi wanaweza kubadilikia na kuwapa kichapo na je, munaweza kujinasua kwa njia ipi? hilo nalo linahitaji uende chuo kikuu? kufanya ulinzi kwenye mabweni yao au mazingira yanayo wazunguka nayo inabidi waende kozi? tusiwe wavivu au washabiki wakusahabikia ujinga bila kuja na nini kifanyike
 
Usitetee uzezeta. Kichwa cha habari na habari yenyewe kifo na usingizi ukiachia mbali kujikanyaga. Kuna nini la lipi hapa gumu la kutafuniwa. Jaribu kupitia maoni yote uone ulivyochemsha hata kama uking'aka vipi mwanangu Mwanaweja.
umesoma post zangu na kuzielewa au? mbona mnapenda kuatafuniwa kila kitu?
 
tulikuwa na mwizi mwanafunzi pale MTC alikuwa akiitwa Onesmo, wale wa 1992 to 1995 watakuwa wanamkumbuka. Hizi redio, nguo viatu ndo zilikuwa zake kuiba. Sasa kuna siku alikamatwa pale block 7, kilichotokea ni kichapo mpaka alipokuja kuokolewa na polisi. The point is si kila kinachoibiwa vyuoni kinaibiwa na mtu toka nje ya chuo, wezi wengine wamo vyuoni humo humo. Wale wa nje wanapata ushirikiano toka kwa hao wa ndani ya chuo. Anzeni na wezi wa ndani, na hao ni rahisi kuwajuwa na kuwakamata. Si mnaishi nao...
 
unaongelea mazigira gani ambayo yako kigamboni? ina maana hata wewe unashabikia ujinga waliufanya jana hawa jamaa? inakuwaje mnakaa kwenye feri bila kuwa na tahadhari ya kuwa polisi wanaweza kubadilikia na kuwapa kichapo na je, munaweza kujinasua kwa njia ipi? hilo nalo linahitaji uende chuo kikuu? kufanya ulinzi kwenye mabweni yao au mazingira yanayo wazunguka nayo inabidi waende kozi? tusiwe wavivu au washabiki wakusahabikia ujinga bila kuja na nini kifanyike

binafsi nakuunga mkono kwa point yako ya kupinga hao wanachuo kujazana kwenye kivuko kwa lengo lao la kushinikiza madai yao. uko sahihi kabisa. tatizo langu topic yako iko vipande vipande...ungeiweka pamoja katika para. pili sioni kama ni sawa kulinganisha mazingira ya Mbeya na Dar...mazingira na watu ni tofauti katika maeneo hayo mawili. otherwise concern yako ni sawa!
 
kaeleza mengi tu. ila kwa kifupi anahubiri sera ya jino kwa jino!

mkuu yaani kwa kifupi hao jamaa walitakiwa kutembeza kichapo cha mbwa mwizi kwa vibaka katika maeneo yao hata wao wakiona kibaka anakuja mitaa yao wanamwambia unatutafutia balaa. Lakini hii ya kufunga barabara na matokeo yake wanatolewa kamasi na polisi tena kwa aibu kubwa jamani fuatilieni taarifa ya ITV ninaimani hii asubuhi watarudia muone walivyokuwa wanatembelea magoti ni huruma usister du, ubrothermen wote ulukuwa umeishatea ghafla
 
tulikuwa na mwizi mwanafunzi pale MTC alikuwa akiitwa Onesmo, wale wa 1992 to 1995 watakuwa wanamkumbuka. Hizi redio, nguo viatu ndo zilikuwa zake kuiba. Sasa kuna siku alikamatwa pale block 7, kilichotokea ni kichapo mpaka alipokuja kuokolewa na polisi. The point is si kila kinachoibiwa vyuoni kinaibiwa na mtu toka nje ya chuo, wezi wengine wamo vyuoni humo humo. Wale wa nje wanapata ushirikiano toka kwa hao wa ndani ya chuo. Anzeni na wezi wa ndani, na hao ni rahisi kuwajuwa na kuwakamata. Si mnaishi nao...
safi sana wewe mkuu angalia mziki tuliokuwa tunaufanya pale MTC mwizi au kibaka akimatwa lazima ateje aliemleta pale chuoni na kama hajataja kichapo kama kawaida na baadaye tulikuwa tunawapeleka polisi lakini ameshalowa jiti kama kawaida na hata akitaja lazima akirudi mitaani anaalama za MTC kichwani kwa kutumia nyembe kichwa kinaandikwa MTC
 
Back
Top Bottom