Wanafunzi wa elimu ya juu wamehujumiwa kupiga kura?

amba.nkya

JF-Expert Member
Jan 7, 2010
446
131
Siku kadhaa zilizopita nilibahatika kumsikia Waziri mwenye dhamana na Elimu ya juu, Prof. Maghembe akitamka kupitia vyombo vya habari. Miongoni mwa mambo aliyotamka ni pamoja na kuwa "wanafunzi wa elimu ya juu wamefunga vyuo na hawaruhusiwi kurudi vyuoni hadi muda wa likizo utakapoisha, hivyo hawatashiriki kupiga kura kwenye vituo walivyojiandikisha wakiwa vyuoni". Pia Waziri huyo alibainisha kuwa "wanavyuo hao hawapaswi kujihusisha na siasa kwani jukumu lao ni kusoma tu".

My Take:
Kama serikali iliona wanavyuo hao hawastahili kupiga kura, kwanini waliruhusiwa kujiandikisha vyuoni? Aidha, serikali haioni kuwa imevunja Katiba kwa kuwanyima wanafunzi hao haki yao ya msingi ya kushikiriki kupiga kura 31.10.10? Nachelea kusema kwamba huu ni woga wa CCM kwani wana hofu kuwa wanafunzi wengi wataipa kura CHADEMA.
 
Hawajahujumiwa. Bali wanafunzi wanachotakiwa kujua ni kuwa HAKI siku zote hutafutwa kwa kujitolea. Wao wafanye kama Mwenyekiti wa NEC alivyosema. Waende katika vituo walivyojiandikishia wakapige kura. Wana muda wa kujiandaa kufanya hivyo ikiwa kweli wana nia thabiti ya kusaidia katika mageuzi ya kuiondoa nchi hii mikononi mwa CCM. Hali hii iliyotokea kwa kuahirishwa muda wa kufungua ingeweza tokea pia kwa chuo kufungwa kutokana na KUNJI kwa enzi zetu je tungesemaje??
 
Back
Top Bottom