Wanafunzi ni kundi kubwa lililopo katika hatari ya kupata maambukizi ya Corona kwa urahisi. Nashauri shule zifungwe

Afyayaakili

JF-Expert Member
Sep 12, 2012
903
1,175
WAZIRI WA ELIMU, NAOMBA TUOKOE HILI KUNDI NGUVU KAZI YA TAIFA YA KESHO.

Kwa hali inavooendelea huu ugonjwa kusambaa haikwepeki lakini ni lazima tupunguze namna ya ueneaji wake na katika jamii yetu ya Kitanzania na ulimwengu kwa ujumla kundi la wanafunzi lipo katika hatari kubwa ya kupata ugonjwa huu wa mlipuko.

Wanafunzi wanatumia karibia masaa nane (8) kwa siku kukaa katika mkusanyiko mmoja kiasi kwamba wakipata maambukizi ni rahisi kuyasambaza wanaporudi majumbani na mitaani kwao.

Naomba shule zifungwe libaki kundi la wanafunzi wanaojiandaa na mitihani kama kidato cha sita tu, wengine warudi tu maana hali ishakuwa tete.

Wenzetu miji kama San Fransisco shughuli zimesimama kwa wiki tatu ili kuzuia maambukizi yasisambae sana hii pia kwa Italy na Hispania inatisha wamepata maambukizi mapya 1,000 ndani ya saa 24 ni hatari aisee.

Tunaomba tuchukue maamuzi mapema kabla ya kuzidiwa, kutumia njia hizi sio kwamba tumekubali tumeshindwa na ugonjwa huu bali ni njia nzuri kuwa tunaweza kupambana na ugonjwa huu na tukaushinda.

Tukae salama kila mtu katika kipindi hiki kigumu cha mpito naamini kila kitu kitakuwa sawa soon.
 
Yaani wewe usiejua hata kuandika ndio wakushauri Wizara
Alichokiandika umekielewa au ndo hadi uugue utamwelewa?

Hivi huyo aliyeugua asingekuwa hajitambui angewaambukiza wangapi kabla ya serikali yenye kiburi kutoa matamko ya mihemko?

Darasani wanakaa watoto 70-100. Hivi kuna usalama?
 
Ukiangalia takwimu watu wanaokufa na huu ugonjwa wengi ni wa umri kuanzia miaka 60
Mpaka sasa hakuna mtoto wa chini ya miaka 10 aliyefariki.
 
Arusha shule zifungwe kwa wiki mbili kupunguza uwezekano wa maabukizi. Dereva teksi, wafanyakazi airport, wahudumu wa hotel aliyofikia wanaweza kuwa vyanzo vya maambukizi kwa familia zao.

Hao member wa familia wanaweza kuwa chanzo cha kuusambaza.

Shule zote zifungwe, mikusanyiko isiyo ya lazima, safari zisizo za ulazima zisitishwe.
 
Kama wewe ni mzazi unampenda mwanao mzuie kwenda shule, serikali haina mtoto watoto ni wajamii. Tamko litatoka hali imeisha kuwa mbaya.
 
HILI LA KUFUNGA MASHULE NAHISI LIFANYIKE KIMKAKATI ZAIDI..
LA SIVYO NI SAWA NA KUTOBOA MELI NA WEWE UPO NDANI

Kwa shule za Day sawa maana Atatoka nyumbn na maambukizi ataenda atasambaza shuleni and vice versa.

Ila Binafsi naona kwa shule za boarding HASA ZILE ZILIZOJITENGA NA MAKAZI YA WATU wafanyiwe vipimo.

Kama hakuna kiashiria chochote wabaki huko huko ndio salama zaidi, japo pia watengwe kwa madarasa au mabweni bila muingiliano mkubwa.

Akigundulika mmoja pia. Watengewe Karantini huko huko maana ndio hatari zaidi ukiwarudisha wote.

Kinyume na hapo ni kuwatoa watu salama sehemu salama na kuwapeleka sehemu hatarishi.

Au kutoa kundi kubwa la watu hatarishi kwenda kuongeza hatari.
 
Kama kutakuwa na ulazima wa kufunga Mashule.

Basi nadhani hili liwe kwa shule za Day tu.

Kwa hili naafiki kabisa.

Maana mwanafunzi Atatoka na maambukizi kwao atapeleka shuleni kwenye kundi kubwa la watu nao kila yule atarudi na maambukizi nyumbani atasambaza kwa wale wa majumbani.

Wanyumbani nao watasambaza sehemu zao za kazi na katika mizunguko ya mitaani.

Hivyo Tunaona WANAFUNZI ndio kundi hatari zaidi kuusambaza uginjwa huu, hasa ukizingatia ni kundi kubwa katika mkusanyiko mdogo.

Kwa shule za BOARDING Hasa zile zilizo Isolated na Makazi ya watu.
Wangepaswa kufanyiwa Uchunguzi wa vipimo.
Kama wapo salama (japo tunajua huwezi kua na uhakika 100%) Basi wabaki huko huko.

Lakini pia wakitengwa kutokana na madarasa au mabweni yao kuepuka mrundikano mkubwa.

Na kama Pia akagundulika mmoja ana maambukizi.
Wengine wasirudishwe makwao.
Wawekwe karantini huko huko (kwa mashuleni sehemu za kuwatenga sio shida).

Hii yote ni kuepuka kujaza hili lundo kubwa mtaani.

Kinyume na hapo Ni kutoa watu Wasio na maambukizi katika sehemu salama na kuwaleta sehemu hatarishi (yenye maambukizi).

Au kutoa watu wenye maambukizi (hatarishi) na kuwapeleka sehemu Salama.

Kwaio unaona by any means.
Shule za namna hii zikifungwa ni kuongeza hatari.
Haijalishi Walio salama wanaenda mtaani au walio na maambukizi wanayapeleka mtaani.
 
Uko sahihi kabisa. Huko bwenini ni Sawa Sawa na self isolation, ihakikishwe tu wafanyakazi kama wanaishi nje ya hapo, wasiwaletee wanafunzi maambukizi.
 
Wataambukizwa na walimu na wafanya kazi! Halafu wataambukizana wao kwa wao!
Au unazani huko boarding wanaishi peke ao bila raia?
 
Mkuu hapo unazungumzia shule za bweni za kishua ila hizi changanyikeni wanajichanganya sana kitaa. Mwanafunzi anaweza kutulia hata siku mbili na jimama kitaa na akarudi shuleni bila kugundulika.
 
Alichokiandika umekielewa au ndo hadi uugue utamwelewa?

Hivi huyo aliyeugua asingekuwa hajitambui angewaambukiza wangapi kabla ya serikali yenye kiburi kutoa matamko ya mihemko?

Darasani wanakaa watoto 70-100. Hivi kuna usalama?

Aandike vizuri kwanza
 
Mkuu hapo unazungumzia shule za bweni za kishua ila hizi changanyikeni wanajichanganya sana kitaa. Mwanafunzi anaweza kutulia hata siku mbili na jimama kitaa na akarudi shuleni bila kugundulika.
Mimi nafikiri mwanafunzi alieko shule ya bweni iliyoko huko maporini yuko salama zaidi akikaa huko, kuliko kumrudisha mjini. Ni kweli kuna muingiliano na watu wa nje lakini ni mdogo sana kulinganisha na huku mjini, na pia anaingiliana na watu ambao nao ni nadra sana kupata maambukizi.
 
Back
Top Bottom