Wanafunzi 11 wapata ajali ya gari Usiku, wakitoka kupakia kuni za mwalimu

Pfizer

JF-Expert Member
Mar 25, 2021
304
518
Njombe

Wanafunzi 11 wa shule ya sekondari Kidegembye iliyopo katika halmashauri ya wilaya ya Njombe wamepata ajali kwenye gari wakitoka kupakia kuni za mwalimu majira ya usiku.
IMG-20231003-WA0005.jpg
Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Njombe kimefika katika hospitali ya mji wa Njombe (Kibena) ambako wanafunzi wanapatiwa matibabu na kutoa maelekezo kwa serikali kuandaa majibu juu ajali hiyo.

"Tumetoka kukagua utekelezaji wa Ilani na kupata taarifa kuwa kuna ajari wanafunzi wameumia Sasa madaktari wa zahanati pale Kidegembye wamekiri kupokea wanafunzi 11 lakini wengine walitibiwa na kuruhusiwa na sita waliletwa huku (Kibena)"amesema Julius Peter Katibu wa CCM mkoa wa Njombe

Aidha amesema kwa maelezo ya walimu,wanafunzi hao walipata ajari majira ya saa moja jioni wakiwa kwenye gari aina ya fuso wakati wakitoka kupakia kuni za mwalimu ambapo amesema wameielekeza serikali kutoa majibu ya hatua zinazoendelea dhidi ya aliyesababisha ajali.
 
Shule wamekuja kusoma au kuajiliwa vibarua.
Hii tabia shule za mikoani ndio tabia zao tena zile shule za kilimo.
Unalipa pesa ya chakula Cha kushangaza wanalimishwa wanafunzi
 
Njombe

Wanafunzi 11 wa shule ya sekondari Kidegembye iliyopo katika halmashauri ya wilaya ya Njombe wamepata ajali kwenye gari wakitoka kupakia kuni za mwalimu majira ya usiku.
View attachment 2770383
Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Njombe kimefika katika hospitali ya mji wa Njombe (Kibena) ambako wanafunzi wanapatiwa matibabu na kutoa maelekezo kwa serikali kuandaa majibu juu ajali hiyo.

"Tumetoka kukagua utekelezaji wa Ilani na kupata taarifa kuwa kuna ajari wanafunzi wameumia Sasa madaktari wa zahanati pale Kidegembye wamekiri kupokea wanafunzi 11 lakini wengine walitibiwa na kuruhusiwa na sita waliletwa huku (Kibena)"amesema Julius Peter Katibu wa CCM mkoa wa Njombe

Aidha amesema kwa maelezo ya walimu,wanafunzi hao walipata ajari majira ya saa moja jioni wakiwa kwenye gari aina ya fuso wakati wakitoka kupakia kuni za mwalimu ambapo amesema wameielekeza serikali kutoa majibu ya hatua zinazoendelea dhidi ya aliyesababisha ajali.
View attachment 2770382
...Sio kutoa Majibu TU, Bali kumchukulia Hatua Mwalimu anayesika na Kuni zake! Watoto tunawaleta Kusoma, Sio kubeba Kuni za Mwalimu....labda ziwe za jiko la Shule !!
 
Back
Top Bottom