ebu cheki hayo majina yenye nyekundu,hivi viongozi wa chadema lazima wawe watu wa maeneo yenye majina hayo! yani hapo chadema ndo inapoharibu na hicho ndo kitawamaliza kabisa! anyway hongereni pia kwa kupata watoto 300 maana kwenye hicho chuo kuna wanachuo zaidi ya elfu so kupata watoto 300 si haba!na Grace Macha, Lushoto
HARAKATI za Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) za kujiwekea ngome kwenye vyuo vya elimu hapa nchini zimezidi kushika kasi baada ya wanachuo wa Chuo Kikuu cha Tumaini cha Sebastian Kolowa (SEKUCO) zaidi ya 310 kujiunga na chama hicho.
Wanachuo hao walikabidhiwa kadi za CHADEMA juzi na mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho ambaye pia ni mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, wakati wa hafla ya uzinduzi wa tawi la chama hicho iliyofanyika eneo la Bondeni nje ya chuo hicho.
Katika hafla hiyo ambayo pia ilihudhuriwa na Katibu wa CHADEMA mkoani Tanga, Benson Mramba, mwenyekiti wa chama hicho wilayani Kinondoni, Henry Kilewo, na aliyekuwa mgombea ubunge wa jimbo la Arumeru Mashariki kwenye uchaguzi mkuu uliopita, Nasari Joshua, wakazi wa maeneo ya jirani waliomba nao kupatiwa kadi za chama hicho.
CHADEMA tayari imeshafungua matawi kwenye vyuo vikuu mbalimbali vikiwemo vile vya Dar es Salaam (UDSM), Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Chuo cha Mipango Dodoma, Chuo cha Maadili Dodoma, Chuo Kikuu cha Mt. Augustine (SAUT), Chuo Kikuu cha Arusha (UOA) na wako mbioni kufungua matawi kwenye Chuo Kikuu cha Meru, Chuo cha Maendeleo Tengeru na Chuo cha Uhasibu Arusha ( IAA).
Lema aliwataka wanachuo hao kuhakikisha wanakuwa jasiri katika kudai haki zao pamoja na jamii inayowazunguka na wasikubali kuburuzwa kwa namna yoyote na badala yake wajenge tabia ya kuhoji pale wanapoona mambo hayaendi sawa.
Mbunge huyo wa Arusha Mjini aliwaeleza wanachuo hao kuwa watumie muda mwingi kuhamasishana kushiriki mijadala ya kisiasa na kujadili changamoto mbalimbali zinazoikabili jamii kwenye maeneo mbalimbali nchini, jambo alilosema litasaidia kwa kiasi kikubwa kuwaamsha wananchi wengine.
NAUNGA MKONO KAZI NZURI YA KIJANA GODBLESS LEMA.
KAZA BUTI KITAELEWEKA TUU.
Dah!! mkuu acha uwoga bana!!Ukizitambua haki zako utaweza kuzitetea so kitu wanacho fanya CHADEMA ni kumfanya kila mwananchi aujue wajibu na haki anazo stahili.Duh another smell of sad story from CCM...yaani kama hii inshu ni kweli basi nawashauri CHADEMA msifunguie matawi kwenye mashule ya sekondari, bora hukohuko vyuoni coz ikitokea CCM wakajua kwamba kuna sekondari ina tawi la CDM nadhani madent watafanya kusikia tu abt University, sidhani kama kuna pua itagusa chuo.
sawa bwana diwani!mapambano yanaendelea,,Hadi kieleweke
na Grace Macha, Lushoto
HARAKATI za Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) za kujiwekea ngome kwenye vyuo vya elimu hapa nchini zimezidi kushika kasi baada ya wanachuo wa Chuo Kikuu cha Tumaini cha Sebastian Kolowa (SEKUCO) zaidi ya 310 kujiunga na chama hicho.
Wanachuo hao walikabidhiwa kadi za CHADEMA juzi na mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho ambaye pia ni mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, wakati wa hafla ya uzinduzi wa tawi la chama hicho iliyofanyika eneo la Bondeni nje ya chuo hicho.
Katika hafla hiyo ambayo pia ilihudhuriwa na Katibu wa CHADEMA mkoani Tanga, Benson Mramba, mwenyekiti wa chama hicho wilayani Kinondoni, Henry Kilewo, na aliyekuwa mgombea ubunge wa jimbo la Arumeru Mashariki kwenye uchaguzi mkuu uliopita, Nasari Joshua, wakazi wa maeneo ya jirani waliomba nao kupatiwa kadi za chama hicho.
CHADEMA tayari imeshafungua matawi kwenye vyuo vikuu mbalimbali vikiwemo vile vya Dar es Salaam (UDSM), Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Chuo cha Mipango – Dodoma, Chuo cha Maadili –Dodoma, Chuo Kikuu cha Mt. Augustine (SAUT), Chuo Kikuu cha Arusha (UOA) na wako mbioni kufungua matawi kwenye Chuo Kikuu cha Meru, Chuo cha Maendeleo – Tengeru na Chuo cha Uhasibu –Arusha ( IAA).
Lema aliwataka wanachuo hao kuhakikisha wanakuwa jasiri katika kudai haki zao pamoja na jamii inayowazunguka na wasikubali kuburuzwa kwa namna yoyote na badala yake wajenge tabia ya kuhoji pale wanapoona mambo hayaendi sawa.
Mbunge huyo wa Arusha Mjini aliwaeleza wanachuo hao kuwa watumie muda mwingi kuhamasishana kushiriki mijadala ya kisiasa na kujadili changamoto mbalimbali zinazoikabili jamii kwenye maeneo mbalimbali nchini, jambo alilosema litasaidia kwa kiasi kikubwa kuwaamsha wananchi wengine.
NAUNGA MKONO KAZI NZURI YA KIJANA GODBLESS LEMA.
KAZA BUTI KITAELEWEKA TUU.
Ndiyo CDM!! kuna tetesi ambazo sio rasmi nimezisikia mahali nataka wana JF mwe makini kuzichunguza na kuzitafutia tiba iwapo na endapo kweli zitakuja kutimia. tetesi zenyewe ni juu ya matokeo ya mtihani wa kidato cha sita uliofanyika Februari 2011, inasemekana kuwa serikari ya CCM ina mpango wenye nia mbaya wa kupunguza ufaulu wa wanafunzi eitha kwa kuficha matokeo ama kuwafelisha wanafunzi kwa kiwango cha kutisha! Adhima na sababu iliyopo nyuma ya kusudi hili ni kwamba Vijana wengi wakijiunga na vyuo vikuu na vyuo vingine moja kwa moja wanaenda kuongeza idadi ya wafuasi wa CDM ambapo upinzani wao dhidi ya CCM unakuwa ni upinzani uliopevuka kiakili na kifikra. Hivyo wana JF natoa tahadhari mapema ili endapo hii hali ikitokea tujue jinsi ya kuwatetea wadogo zetu na wenzetu wa CDM, sio taarifa rasmi lakini inaleta hisia ya kujiweka tayari kwa sababu CCM sa ivi imeamua kuingiza siasa katika maslahi yanayomhusu mwananchi moja kwa moja kama njia mojawapo ya kutaka kujitetea dhidi ya shubiri inayotolewa na CDM. Tusifikiri kwamba ccm wamenyamaza tu kuona vijana wengi vyuoni wakijiunga na CDM na bado matawi yakifunguliwa vyuoni kwa kasi hivi!! CDM tuwe makini!