MwanaPekee
JF-Expert Member
- Jul 18, 2014
- 382
- 385
Upinzani wa Tanzania ni mgumu sana kuulewa maana hata hawaeleweki nini hasa wanakitaka. Wakati zoezi la kuandikisha wapiga kura lilipokuwa likiendelea, na serikali kutumia muda mwingi kuwaelimisha watu umuhimu wa wao kujiandikisha na kupiga kura, Upinzani ulishangilia na kuwaunga mkono wale ambao hawakujitokeza kujiandikisha.
Hata hivyo Serikali ilitumia juhudi kubwa kuhakikisha idadi kubwa ya watu inafikiwa. In short hakuna aliyelalamikia mchakato huo kwa upande wao kuwa ulikuwa na kasoro zozote za kikanuni, zaidi ya kuwaunga mkono wale ambao hawakujiandikisha.
Hatua ya pili ilikuwa ni kwa wagombea kuchukua forms na kuzijaza kwa mujibu wa Sheria na Kanuni zinazoongoza uchaguzi wa Serikali za mitaa. Katika hatua hii ndipo malalamiko yalipoanzia hasa baada ya wagombea wao wengi kuonekana wakikiuka Sheria na Kanuni hizo na hivyo kuenguliwa kwenye mchakato wa kugombea uongozi kwa nafasi mbalimbali.
Serikali imesikiliza kilio chao na kuamua kuwaruhusu wagombea wao wote waliochukua na kurejesha kushiriki katika uchaguzi huo licha ya kukiuka baadhi ya Sheria na Kanuni hizo, lakini bado wamekuja na hitaji la “Kuanza mchakato upya, yaani kuanzia uandikishaji wa wapiga kura”, la sivyo hawatashiriki.
Najiuliza kwanini hawakulalamikia mchakato wa uandikishaji wa wapiga kura toka mwanzo, na sasa wanataka turudi huko? Je, kwanini wanasema hawatashiriki hata baada ya malalamiko yao kusikilizwa? CCM, imepita bila kupingwa katika maeneo ambayo wao hawakuweka mgombea, sasa wao walitaka iwaje?
Ninachokiona mimi hapa ni kuwa hawa watu hawana shida na uchaguzi. Wao wanatengeneza mazingira ya kuonekana wanaonewa kila wakati. Itakuwa poa kama serikali itawachunguza watu wachache wanataka kuvuruga mchakato huo na kuwachukulia hatua kali za kisheria.
Na kuhusu uchaguzi, hakuna haja ya kuwabembeleza, vyama vilivyotangaza kujiondoa ni vitatu tu, lakini kuna vyama vingi tu (Almost 10) ambavyo viko tayari kuendelea na mchakato.
Tuache Maneno, Tuchape Kazi, Tulijenge Taifa Letu.
Hata hivyo Serikali ilitumia juhudi kubwa kuhakikisha idadi kubwa ya watu inafikiwa. In short hakuna aliyelalamikia mchakato huo kwa upande wao kuwa ulikuwa na kasoro zozote za kikanuni, zaidi ya kuwaunga mkono wale ambao hawakujiandikisha.
Hatua ya pili ilikuwa ni kwa wagombea kuchukua forms na kuzijaza kwa mujibu wa Sheria na Kanuni zinazoongoza uchaguzi wa Serikali za mitaa. Katika hatua hii ndipo malalamiko yalipoanzia hasa baada ya wagombea wao wengi kuonekana wakikiuka Sheria na Kanuni hizo na hivyo kuenguliwa kwenye mchakato wa kugombea uongozi kwa nafasi mbalimbali.
Serikali imesikiliza kilio chao na kuamua kuwaruhusu wagombea wao wote waliochukua na kurejesha kushiriki katika uchaguzi huo licha ya kukiuka baadhi ya Sheria na Kanuni hizo, lakini bado wamekuja na hitaji la “Kuanza mchakato upya, yaani kuanzia uandikishaji wa wapiga kura”, la sivyo hawatashiriki.
Najiuliza kwanini hawakulalamikia mchakato wa uandikishaji wa wapiga kura toka mwanzo, na sasa wanataka turudi huko? Je, kwanini wanasema hawatashiriki hata baada ya malalamiko yao kusikilizwa? CCM, imepita bila kupingwa katika maeneo ambayo wao hawakuweka mgombea, sasa wao walitaka iwaje?
Ninachokiona mimi hapa ni kuwa hawa watu hawana shida na uchaguzi. Wao wanatengeneza mazingira ya kuonekana wanaonewa kila wakati. Itakuwa poa kama serikali itawachunguza watu wachache wanataka kuvuruga mchakato huo na kuwachukulia hatua kali za kisheria.
Na kuhusu uchaguzi, hakuna haja ya kuwabembeleza, vyama vilivyotangaza kujiondoa ni vitatu tu, lakini kuna vyama vingi tu (Almost 10) ambavyo viko tayari kuendelea na mchakato.
Tuache Maneno, Tuchape Kazi, Tulijenge Taifa Letu.