From: Said Amour Arfi
<said_arfi@yahoo.com>
Date: November 22, 2013 3:45:47 PM
GMT+03:00
To: "mbowe2008@gmail.com"
<mbowe2008@gmail.com>
Cc: "slaa@chadema.or.tz.
zittokabwe@gmail.com"
<slaa@chadema.or.tz.
zittokabwe@gmail.com>
Subject: KUJIUZULU MAKAMU
MWENYEKITI (BARA)
Salaam,
Napenda kuwasilisha kwako taarifa ya
kujiuzulu nafasi ya Makamu
Mwenyekiti Bara kuanzia Leo Ijumaa
22 Novemba 2013 kwa kuchoshwa na
Unafiki unaoendelea ndani ya Chama.
Napenda ifahamike pia kwangu
maslahi ya Wapiga kura, Wakaazi na
wananchi wa Mpanda Mjini na Wilaya
ya Mpanda ni muhimu katika
kuwatumikia, hivyo basi sipo tayari
kuchaguliwa marafiki.
Kwa kipindi kirefu zimekuwepo
shutma dhidi yangu na kutiliwa
mashaka mahusiano yangu na Mhe
Pinda Waziri Mkuu pamoja na
kulijadili katika vikao kadha Mpanda
na Dar es Salaam bado yapo mashaka
kwa nini alipita bila kupingwa hayo
yalikua maamuzi ya Wanampanda
kwenu imekua ni tatizo lakin
hamsemi kwa nini Majimbo mengine
16 nchini yalipita bila kupingwa
mlikua wapi na nani alaaumiwe huu
ni Unafiki wa kupindukia.
Aidha mmechukizwa sana kwa nini
nilihoji kauli ya Muasisi wa Chama
Mhe Mtei kutuchagulia viongozi
naomba ifahamike wazi kwamba huu
ni mtazamo wangu na utabakia hivyo
siku zote kwa chama cha demokrasia
kutoruhusu uongozi wa kiimla kwa
kukidhi matakwa ya Waasisi ambao
huvigeuza vyama kuwa Mali binafsi
Kwa kusema ukweli na kusimamia
ukweli daima itabakia kuwa lengo
langu katika maisha yangu siku zote
hata kama itanigharimu maisha
yangu
Nawasilisha.
Said A Arfi (mb)
Nakala Vyombo vya Habari