Wanaccm waanza kumchukia Magufuli, wadai asijidanganye alishinda kwa nguvu zake binafsi

ibesa mau

JF-Expert Member
Sep 17, 2015
2,109
1,697
Ninaposema wanaccm si maanishi mwanaccm anayeishi kijijini anayetembea bila ndala, si maanishi wanaccm wanaotembelea baiskeli. Ninamaanisha wana ccm wenye chama chao.

Kundi la wanaccm waliokosa vyeo ( uwaziri ) na ubunge ( wa kuteuliwa) . wapo wabunge waliojua fika lazima wapate uwaziri kutokana na kujiamini kwamba lazima wawepo, lakini baada ya uteuzi wa awamu ya kwanza kupita wakajipa moyo kwamba kwa kuwa uteuzi bado huenda wakaingia awamu ya pili, lakini baada ya awamu pili nayo kupita kuona hawapo wameanza vikao vya mikakati.

Lakini vilevile lipo kundi jingine lililojipa moyo kwamba wangepata ubunge wa kuteuliwa lakini mpaka sasa raisi kashateua nafasi 6 na bado nne hivyo wameshakata tamaa kupata hizo nafasi nne zilizosalia na kuamua kuungana na kundi la kwanza kuanza figisu figisu.

Lakini kundi la tatu ni lile la wabunge wa kawaida ambao wao hawakuwa na mategemeo ya kupata ubunge wao wanamwona kama magufuri ni mtu asiyetaka maridhiano na wabunge na wanamwona magufuri kama mtu anayejiona amepita kwa nguvu zake wakati wao ndio waliofanya kazi ya kupiga magoti kwa wananchi ili kuwaombea kura madiwani na raisi tena kwa gharama zao binafsi kuna baadhi ya majimbo hawakupata fedha ya chama kabisa , kundi hili linalalamikia kitendo cha boss kuwateua watu ubunge na kuwapa uwaziri watu ambao hawakufanya lolote wakati wa kampeni na kuwaacha watu waliojitoa usiku na mchana kukisaidia chama kushinda.

Tutegemee kuanza kujengeka kwa makundi makundi ndani ya ccm wakati kundi lenye nguvu kiasi kikubwa lipo nje, na kundi lililopo ndani halina nguvu ukimwacha nchemba , januari na Nape lakini wengine wote hawana nguvu ndani ya ccm . Makundi hayo yatajenga mpasuko ndani ya ccm . Kitendo cha kuzuia ziara za nje kwa wabunge na kitendawili kinachosubiri jibu cha kukopeshwa fedha za usafiri kwa wabunge kitaongeza msuguano mkubwa kama raisi atakataa kuwapa fedha walizoomba milioni 150
 
Basi uchaguzi urudiwe sasa hivi waone kama hatashinda?
Kama sio nguvu zake bunafsi lakini mwenyekiti wao ndio alimtengenezea mwenzake njia ngumu.
Sasa hivi Magu akalale chato asifanye kampeni.
 
Wao wamuunge mkono tu maana kwa sasa mwenzao yuko mbali sana........wakifanya mchezo atagombea binafsi na atashinda tena 2020
 
Kumbe ni kakikundi kasikozidi watu 100?
Go Magufuli go, ulipo tupo.
 
Last edited by a moderator:
Hahahahahaaaaaa! Baada ya kushindwa kwenye siasa za ushindani, sasa mnataka kumgombanisha Magufuli na wana CCM wenzake. Poleni sana. Ushindi 2020 ni lazima
 
WACHA WAISOMEEEE. MAGUFULI JIPU LINGINE KWA TANZANIA YA WAJUKUU WAKO HUKO MBELENI NI KATIBA YA WARIOBA. IRUDISHE KATIBA YA WARIOBA, PUNGUZA PAYE HAKIKA UTATAWALA HATA MISIMU MITANO. WANYoNYAJI WALICHOKIFANYA KINATOSHA USIWAPE MWANYA HATA KIDOGO
. WAKIKUANDAMA SANA HAMIA UKAWA NA UTASHINDA KWA KISHINDO HAPO SASA ITAKUWA NI KUWANYONGA KABISA.
 
At least we now know who are the real enemies of progress, and Dr Magufuli is not one of them so if he chooses to disband the Parliament we the people will deal with all those parliamentarians who tried to sabotage the President. We will vote them all out!!!
 
Fitna mnazo eneza humu ndani HAZITALETA MPASUKO NDANI YA CCM WALA NYUFA.BADALA YAKE CCM INAZIDI KUNGA'RA NA KUWA IMARA.UNADHANI CCM NI KAMA KILE CHAMA KILICHOKUWA KIMESHATEUA NI NANI NA NANI ATAKUWA NA CHEO HIKI NA IKAPELEKESHA WATU KUSHONA SUTI KABISA .NA WAPISHI WA FITNA CCM WAMETOKA WENYEWE BILA KUAMBIWA HAPA SASA HAMTOSHI
 
......we have to thanks lowassa!....
if not his wisdom of detach to ccm,we shouldnt have " precious dk.magufuri"
insteady off,THE ESCOBOR FAMILLY COULD CONTINUE LEAD!
 
WACHA WAISOMEEEE. MAGUFULI JIPU LINGINE KWA TANZANIA YA WAJUKUU WAKO HUKO MBELENI NI KATIBA YA WARIOBA. IRUDISHE KATIBA YA WARIOBA, PUNGUZA PAYE HAKIKA UTATAWALA HATA MISIMU MITANO. WANYoNYAJI WALICHOKIFANYA KINATOSHA USIWAPE MWANYA HATA KIDOGO
. WAKIKUANDAMA SANA HAMIA UKAWA NA UTASHINDA KWA KISHINDO HAPO SASA ITAKUWA NI KUWANYONGA KABISA.

ahamie ukawa tena ?? lowasa atakubali akatwe na magufuri?
 
Magufuli baada ya kusimamisha mafuriko kwa dole sasa nnaona waliokuwa wanampinga dole limewakolea wanalichekelea.
 
Kumbe ni kakikundi kasikozidi watu 100?
Go Magufuli go, ulipo tupo.

Wewe Wonderful hoja yako pia ni wonderful. Wanaomchukia MAGUFULIndani ya CCM ni watu wachache mno na kama ulivyosema sidhani kama wanazidi 100. WanaCCM wa kawaida na wananchi wengine wasio CCM wanampenda MAGUFULI. Siku CCM hawa wachache (na ambao nina hakika hivi sasa wanapanga na kula njama za kumuangusha MAGUFULI) wakikosea na kumsakama ndipo watakapojua nguvu ya umma ikoje. wasirogwe wakafanya hivyo.
 
Back
Top Bottom