Zanzibar-ASP
JF-Expert Member
- Nov 28, 2013
- 12,151
- 44,078
Baadhi ya makada wa CCM katika jimbo la vunjo wameanza kususa kuendelea na kampeni za kuinadi CCM kuanzia nafasi ya Udiwani, ubunge na Urais kufuatia kitendo cha mgombea urais wa CCM, John Magufuli kufika jimbo la Vunjo na kuanza kumpigia kampeni Mrema wa TLP awe mbunge badala ya kumnadi mgombea wa ubunge wa CCM innocent Shirima. Kitendo hicho wamekitafsiri kama ni dharau na kuwadhalilisha wanaCCM wa Vunjo kwa kuwa kwa sasa wanaonekana kama watu wasiojitambua kwa kuwa wanachokipigania hakipo tena.
Baadhi ya wakazi wa vunjo wameanza kuwatania makada wa CCM kwa kuwaita "Misukule" baada ya magazeti yenye Picha na habari ya tukio kuzagaa kila mahali katika mkoa wa Kilimanjaro japokuwa tukio lenyewe limetokea Vunjo.
Baadhi ya wakazi wa vunjo wameanza kuwatania makada wa CCM kwa kuwaita "Misukule" baada ya magazeti yenye Picha na habari ya tukio kuzagaa kila mahali katika mkoa wa Kilimanjaro japokuwa tukio lenyewe limetokea Vunjo.