Wana JF tusaidiane

Wana JF tusaidiane

BabaMorgan

JF-Expert Member
Joined
Dec 18, 2017
Posts
5,149
Reaction score
14,205
Licha ya JamiiForums kuwa Home of Great Thinkers pia ni forum ambayo member wengi utoa ya moyoni. Wengi humu tunatumia ID ambazo sio rahisi kufahamiana kitu ambacho upelekea mtu kufunguka hata yale ambayo hawezi kuyanena mbele ya jamii iliyomzunguka.

Kwa observation yangu ya nyuzi nazozisoma humu JF na comments za baadhi ya members zinajieleza wazi kuwa kuna tatizo ambalo mhusika anapitia yaweza kuwa kiuchumi, kitaalamu, na hata pia kisaikolojia. Tusisubiri mpaka member mwenzetu akafika katika hatua mbaya ndo tuweze kumsaidia. Unaposoma uzi wa mtu na ukagundua ana changamoto ni vizuri kumsaidia sio lazima pesa hata mawazo yako yanaweza kumpa mwanga.

Usishangae kukuta kuna members humu nyuzi zao zilionyesha wanahitaji msaada wa kisaikolojia wakakosa na kufikia hatua ya kujiua. Mimi ningependa kukumbusha tu JF MEMBERS TUSAIDIANE humu kuna members ni waalimu, madaktari, wachumi, wanasaikolojia na wengine wengi wenye taalamu mbalimbali tusaidiane unapoana nyuzi inahitaji msaada usisite kuutoa.

Fanya dunia kuwa sehemu salama.
 
Ahsante sana kwa post yenye ujumbe mzuri ni kweli humu kuna watu wana moyo mzuri sana wa kutoa msaada na wengi ni wakatisha tamaa. Yaani mtu kapost jambo akiwa anaomba ushauri afu jitu linakoment ujinga.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kiukweli huwa naogopa kutangaza shida/tatizo humu jf maana watatokea wa kukujeli hadi ujute kwanini umesema, mtu unaishia kufa ndani kwa ndani.
Sina moyo wa kuvumilia kejeli

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu, Hiyo ni kweli lakn si wote wata-comment pumba kunawatu wako very smart umu jf japo si kwa kutoa mchango wa pesa hapana ila mawazo very brilliant japo unatakiwa kujiaanda kiakil kwa kejer but be free take as if nobody know u.
 
Yeah...sure!

Lakini humu kuna baadhi watatumia Shida yako Kuchekesha watu Wengine Wenye huzuni kwa Wakati huo( Kupitia Joke's Comment).
 
yaaap take your time thinking but stil ujue Kuna watu watakuwa na ww bega to bega ukiwa tayal kufunguka jf ni Zaidi ya ndugu more than a friend
Si kweli. Unamdanganya huyu binti.. msaada hauombwi huja automatically.
Akieleza shida zake humu sana ataishia kuzodolewa wengine wata take advantage ya shida zake ili kumpata.
Bora ubaki na shida zako kuliko kuzianika mitandaoni..to the strangers
 
Si kweli. Unamdanganya huyu binti.. msaada hauombwi huja automatically.
Akieleza shida zake humu sana ataishia kuzodolewa wengine wata take advantage ya shida zake ili kumpata.
Bora ubaki na shida zako kuliko kuzianika mitandaoni..to the strangers

Behind the keyboard, who is there to guess kwamba huyu ana shida hii au yule ana shida gani?

Tatizo la JF lina watu wengi (could be more than 70) ni losers, so, ikitokea mmoja anatangaza shida, inakuwa kama relief kwa wengi wetu humu kwa kuona kwamba tuko wengi.

Tena wengine wako likely kumlabel mtu kama tapeli ili tu hata wale waliokuwa wamejitolea kusaidia wafe moyo.

Watu wanahitaji kubadilika.
 
Kiukweli huwa naogopa kutangaza shida/tatizo humu jf maana watatokea wa kukujeli hadi ujute kwanini umesema, mtu unaishia kufa ndani kwa ndani.
Sina moyo wa kuvumilia kejeli

Sent using Jamii Forums mobile app
Mimi huwa sioni tabu kueleza shida popote ili mradi sivunji sheria. Mungu amenikutanisha na watu wengi humu jf ambao nisingewapatavkwingine. Pamoja na kuwa wapo wenye kejeli ila wakusaidia pia wapo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi ni mtu wa utani
Sana, Ila linapofika suala la matatzo au inshu yyt serious utani naweka kandoo, km siwezi kutoa msaada napita kimyaa.
Tunaumiza wengi sana humu ila tunachukulia poa tuu..
Nashukuru sijui mara ya mwisho kukwaruzana na member ni lini humu..
Na hua ikitokea hivyo huyo mtu namwomba msamaha kwenye wall na namfuata PM..
 
Si kweli. Unamdanganya huyu binti.. msaada hauombwi huja automatically.
Akieleza shida zake humu sana ataishia kuzodolewa wengine wata take advantage ya shida zake ili kumpata.
Bora ubaki na shida zako kuliko kuzianika mitandaoni..to the strangers
Hahaha wanasema "Kula Uliwe ndio mwendo wa sasa".

Vijana wanasema "hata akiibana haileti interest na hazitaongezeka kuwa mbili, bora aitumie tu imsaidie anapokuwa nashida".
That is not me, nime copy.
 
Mimi ni mtu wa utani
Sana, Ila linapofika suala la matatzo au inshu yyt serious utani naweka kandoo, km siwezi kutoa msaada napita kimyaa.
Tunaumiza wengi sana humu ila tunachukulia poa tuu..
Nashukuru sijui mara ya mwisho kukwaruzana na member ni lini humu..
Na hua ikitokea hivyo huyo mtu namwomba msamaha kwenye wall na namfuata PM..
Kweli hiyo ndo maana halisi ya ustaarabu.
 
Back
Top Bottom