Wana jamvi ninaomba msaada wa mawazo.

akatanyukuile

JF-Expert Member
Sep 13, 2019
314
308
Mimi ni mhitimu wa chuo fani ya ualimu. Nilimaliza mwaka 2015 kwa mchepuo wa arts. Hivo mimi ni mhanga wa ajira mpya.

Nilivoona maisha yamekwama kijijini nililazimika kujitosa jijin Dar es Salaam kusaka maisha. Nilibahatika kupata kazi ya kufundisha shule moja ya binafsi, baada ya miaka miwili figisu zilikuwa nyingi nikaamua kuachana nao.

Ila kwa muda huo wote nimebahatika kupanga vyumba vyangu viwili na kuhakikisha nimeweka kila kitu kinachotakiwa, na pia nilikuwa ninasevu kapesa kidogo kidogo ambapo kwasasa nina milion 3 benki.

Changamoto inakuja nifanye nini na hizo milioni tatu. Nilinunua pikipiki ikaibwa hivyo sitaki kurudi kwenye maumivu ya pikipiki

Tafadhari mwenye uelewa wa biashara anisaidie nifungue nini ili niweze endeleza kapesa hako ambako ninako. Kwasasa sina kazi nipo tu ninawaza cha kufanya. Nipo Tegeta kwa ndevu hapa.

Msaada tafadhali.
 
HONGERA MKUU KWA KWA KUWA NA NIDHAMU YA PESA, JAPO UNAPATA KIDOGO ILA UNAJITAHIDI KUWA NA AKIBA
Cha kukushauri kwanza kama uko nyumba ya gharama sana hamia ile ya bei nafuu ili kupata nafasi ya kujipanga kwanza.
 
Ushauri wangu nenda kijijini ulipotoka angalia wana kijiji nini wanahitaji sana kutoka mjini au nje kabisa. Itumie hii fursa kuwaletea wanacho kihitaji, shida kwao fursa kwako hii ndio njia ya biashara. Usikurupike kufanya mpaka ufanye tasmini ya mahitaji,mauzo na malipo.


Ndukiiiii🏃‍♂️🏃‍♂️🏃‍♂️
 
Tafuta sehemu kaanga chip's na kuku au mishkaki, tegeta hapo mbona biashara kibao za kufanya, au omba kaeneo hapo karibu na stend ya kwenda bunju au yakwendea mwenge, au popote ila karibu na barabarani, weka kajibanda kadogo,, fuata matunda temeke stirio au buguruni kauze hapo tegeta,, matunda yana faida sana, parachichi la Mia mbili we unakuja kuuza efu moja, tikiti la efu mbili, we utakuja kuuza efu tano, na ukiyakata vipande ndo faida Kubwa zaid pia,,

Jaribu hii biashara hutojuta,usione aibu tu na usiwe mvivu wa kudamka kufuata matunda
 
Pamoja na changamoto ulio nayo kwa sasa, binafsi naomba nikupongeze sana kwa kuwa na nidhamu ya pesa, na pia kwa kuthamini kile kidogo ulichokuwa ukikipata.

Ukweli ninakutofautisha sana na vijana wengi ambao wanapenda kuomba pasipo kuwaza kwamba hata kidogo wanacho kipata wanaweza wakakitunza hata kikawa kikubwa.

Ungelikuwa Dodoma, ningelikupa ushauri wa nini ufanye na hata pengine ningekuonesha wapi ukafanye nini na ungepata faida.
 
Mimi ni mhitimu wa chuo fani ya ualimu. Nilimaliza mwaka 2015 kwa mchepuo wa arts. Hivo mimi ni mhanga wa ajira mpya.

Nilivoona maisha yamekwama kijijini nililazimika kujitosa jijin Dar es Salaam kusaka maisha. Nilibahatika kupata kazi ya kufundisha shule moja ya binafsi, baada ya miaka miwili figisu zilikuwa nyingi nikaamua kuachana nao.

Ila kwa muda huo wote nimebahatika kupanga vyumba vyangu viwili na kuhakikisha nimeweka kila kitu kinachotakiwa, na pia nilikuwa ninasevu kapesa kidogo kidogo ambapo kwasasa nina milion 3 benki.

Changamoto inakuja nifanye nini na hizo milioni tatu. Nilinunua pikipiki ikaibwa hivyo sitaki kurudi kwenye maumivu ya pikipiki

Tafadhari mwenye uelewa wa biashara anisaidie nifungue nini ili niweze endeleza kapesa hako ambako ninako. Kwasasa sina kazi nipo tu ninawaza cha kufanya. Nipo Tegeta kwa ndevu hapa.

Msaada tafadhali.
Hapo kwa ndevu huwa kuna biashara,tafuta kafrem weka bidhaa anza kupiga mzigo baadaye jiunge na group moja hv la watsup unaunganishwa na watu wapo China unaagiza mzigo toka huko moja kwa moja.
 
Back
Top Bottom