Wana CHADEMA msitukane mamba kabla hamjavuka mto

Sijatumwa na mtu kusema haya. Nimejituma mwenyewe. Hapo natoa jibu la post ya kwanza kutoka kwa mashabiki wa CDM. Wala sijapokea bahasha kama kauli mbiu yenu humu isemavyo.

Najua kuwa, Viongozi wa CDM hasa Mnyika, ni watu makini sana. Wanajua nini wanafanya katika vita ya kumkomboa Mtanzania. Nawaunga mkono mia kwa mia. Sasa kimbembe ni kwa mashabiki wa chama, sina hakika kama wote wanaopiga kelele ni wanachama hai au la.

Lakini wanahitaji semina na ushauri nasaha, wapate mfundo wa kuacha hasira, jazba, chuki, hamaki, ukali na kejeli wanapoambiawa ukweli. Lazima watambue kuwa vyama navyo vina kifo, na vifo vingine hutokea ghafla kama kile cha CUF. Kwani walikuwaje wale jamaa? Sasa hivi wako wapi? Msibweteke na mafanikio ya chama kwa sasa!

Kumbukeni kuwa ndio kwanza bado kinatambaa. Wenzenu wanasherekea miaka 35, umri wa mtu mwenye mjukuu. Nyie je? Mingapi! Msitukane wakunga wakati uzazi bado ungalipo.

Kubalini ushauri, na kukosolewa pia. Mtu akikucheka, usimtukane. Jitazame kwani unaweza kuwa umejipakaza kinyesi. Na siku zote kichaa akikwambia "nyoka huyoo" usipuuze! Anaweza kuwa nyoka kweli kwani kichaa naye ana macho japo akili zake zimekaa upande...

Mbona mwenyewe unaonekana unajazba....punguza kwanza ndo ukemee wengine
 
Sijatumwa na mtu kusema haya. Nimejituma mwenyewe. Hapo natoa jibu la post ya kwanza kutoka kwa mashabiki wa CDM. Wala sijapokea bahasha kama kauli mbiu yenu humu isemavyo.

Najua kuwa, Viongozi wa CDM hasa Mnyika, ni watu makini sana. Wanajua nini wanafanya katika vita ya kumkomboa Mtanzania. Nawaunga mkono mia kwa mia. Sasa kimbembe ni kwa mashabiki wa chama, sina hakika kama wote wanaopiga kelele ni wanachama hai au la.

Lakini wanahitaji semina na ushauri nasaha, wapate mfundo wa kuacha hasira, jazba, chuki, hamaki, ukali na kejeli wanapoambiawa ukweli. Lazima watambue kuwa vyama navyo vina kifo, na vifo vingine hutokea ghafla kama kile cha CUF. Kwani walikuwaje wale jamaa? Sasa hivi wako wapi? Msibweteke na mafanikio ya chama kwa sasa!

Kumbukeni kuwa ndio kwanza bado kinatambaa. Wenzenu wanasherekea miaka 35, umri wa mtu mwenye mjukuu. Nyie je? Mingapi! Msitukane wakunga wakati uzazi bado ungalipo.

Kubalini ushauri, na kukosolewa pia. Mtu akikucheka, usimtukane. Jitazame kwani unaweza kuwa umejipakaza kinyesi. Na siku zote kichaa akikwambia "nyoka huyoo" usipuuze! Anaweza kuwa nyoka kweli kwani kichaa naye ana macho japo akili zake zimekaa upande...

Tuondolee ushuuzi wako hapa, Wataka kuwa mshauri wa CDM???
 
Upo sawa kabisa mkuu, m2 mwenye busara hua tayari kukosolewa. Kama walivyo viongozi we2 wa CHADEMA.

ndugu,lets agree to disagree,ivi uyu mtu analeta uongo tuache eti ni ushauri?haiwezekani...akosoe chama chake kwanza...badala ya kujadili mada zenye kujenga jamii eti anaishauri cdm? jana tu waziri wetu wa afya anadanganya bungen eti kcmc madaktari hawana mgomo apo apo leo madr wameendelea kugoma ata kukutana na mkuu wao,KKKT...Juzi mh pinda anadanganya taifa kuwa rais kasain
 
Kuna mzee mmoja aliniambia kwamba miaka ya 60 Samweli Sitta na wenzake wakiwa wanafunzi wa UDSM waliandamana wakiwa na mabango kuelekea ikulu kupinga mpango wa serikali kuwataka wanafunzi wa vyuo vikuu kupitia mafunzo ya JKT.Walikuwa hoja nyingi za msingi likiwemo hilo lakini katikati yao akachomekwa mtu wa usalama aliebeba bango linalokashfu serikali...na hiyo ikawapa serikali sababu ya kuwaaachia waingie ikulu na Mwalimu Nyerere akawalamba viboko.

Nachosisitiza hapa ni kuwa ni vizuri pia kusikiliza upande mwingine wa shilingi hata kama hoja hukubaliani nayo...lakini kinachonishtua ni namna watu wanaotoa maoni ya kukisaidia CDM wanavyoshambuliwa kwa maneno ya kejeli na dharau kana kwamba hiki ni chama cha watu wasiofanya makosa.....Na hili linanishawishi kuamini kuwa miongoni mwa watu wanaokisapoti kuna mamluki,ambao hutoa maneno ya kejeli kuonyesha wanakipenda chama kumbe wanakipaka sifa mbaya ya kukionyesha ni chama kisichokubali kukosolewa.

Haiwezekani iletwe hoja hapa halafu wanaokiunga mkono karibia wote watoe maneno ya kuponda tu bila kujadili hoja.Mtatuharibia chama na kikaonekana ni cha watu wasio kuwa na busara na wanaokurupuka.Hata miongoni mwa viongozi wa CDM wanatofautiana kwa mawazo na hoja lakini hatuwasikii wakipigana vijembe. Tafadhali viongozi muwe mnapita humu kusafisha hali ya hewa.

wewe una pumba nyingi na unataka kututeka kisaikolojia,DHAHIRI UMETUMWA NA UNA SIASA AMBAZO ZIMECHAKAA KAMA Mabalozi wa ccm.VIVA CDM
 
ndugu,lets agree to disagree,ivi uyu mtu analeta uongo tuache eti ni ushauri?haiwezekani...akosoe chama chake kwanza...badala ya kujadili mada zenye kujenga jamii eti anaishauri cdm? jana tu waziri wetu wa afya anadanganya bungen eti kcmc madaktari hawana mgomo apo apo leo madr wameendelea kugoma ata kukutana na mkuu wao,KKKT...Juzi mh pinda anadanganya taifa kuwa rais kasain

Inaonekana unasinzia sasa, pole sana kwa kazi za leo. Nimegundua tatizo lako, unataka kuniingiza kwenye ushabiki na malumbano ya kichama. Umekosea, waziri wa afya awe mwongo! Au asiwe mwongo, mimi hanihusu. Hanihusu kwa sababu mimi si mwanachama wa chama chochote, fuatilia thread na post zangu. Nakosoa vyama vyote. Nimejiweka mbali na vyama ili niwe na uhuru wa kutoa maoni bila mahaba ya kichama kama ulivyo wewe. Napiga kotekote, kwa maana rahisi, yaani sifungamani na upande wowote.
 
wewe una pumba nyingi na unataka kututeka kisaikolojia,DHAHIRI UMETUMWA NA UNA SIASA AMBAZO ZIMECHAKAA KAMA Mabalozi wa ccm.VIVA CDM

Duh, kipande hiki kinaniumiza kichwa. Kama nawe ni CDM, Basi chama kina wapiga kura kweli kweli!
 
Tuondolee ushuuzi wako hapa, Wataka kuwa mshauri wa CDM???

Haya Jumakidogo nafikiri utakuwa umenielewa vizuri zaidi.....Huwa nakutana na vijana wenzangu ambao kimsingi wanaipenda CDM na wangependa ku-share mambo ya msingi na wenzao ikiwemo kutoa ushauri ambao pengine kwa mtazamo wa wenzao wa humu jamvini ni "kutumiwa na magamba" ,lakini wakifikiria hayo na maneno ya hovyo watakayopata hawana hamu kuja hapa jamvini.

Kila jambo linaloibuka linavishwa joho la Chama, iwe mgomo wa madaktari au mijadala bungeni.Ukionekana una mawazo tofauti utabandikwa majina kibao ya ajabu na kashfa za kumwaga.

Nashauri kama mtu unaipenda CDM hebu njoo na hoja milioni 1 kuliko kuja na kejeli hata 1.Na pia Viongozi wa CDM na member wenye mtazamo chanya wakiona kuna thread ambayo ina mwelekeo wa kukikosoa au kukishauri chama haraka wajibu hoja kiukomavu au hata kukubaliana na ukosoaji. Hii itakuwa kama inatoa mwongozo kwa wale wenye haraka ya kujibu kutafakari kwanza.
 
ni bora kuitwa PANDIKIZI anayesaidia kuleta mageuzi ya kweli kuliko kuwa mshauri anayeua maendeleo...

Kujibu pumba, na utumbo ndo kuleta maendeleo? Mmetumwa ili CDM kionekane chama cha wapumbavu?
 
ndugu juma mi sawa nakubali kuitwa mbumbumbu au mbumbuka kwa vijineno vyako vya kumbumba ambavyo hata ktk aina za nyumbulisho wa kiswahili sanifu hakuna...tatizo ni kuleta ushauri hewa ...pia unajifanya mwema wakati ndo umejawa na kejeli na maneno ya ajabu...unasema hata ARV haziwatoshi waliokupinga,je waweza kudai unatumia akili kweli juma?...dawa ya moto ni moto...ukiongea vibaya utegemee kupata jibu baya...sorry we are ready to call a spade a spade and not a big spoon...ivo pokea haki yako kama ulivota
 
Haya Jumakidogo nafikiri utakuwa umenielewa vizuri zaidi.....Huwa nakutana na vijana wenzangu ambao kimsingi wanaipenda CDM na wangependa ku-share mambo ya msingi na wenzao ikiwemo kutoa ushauri ambao pengine kwa mtazamo wa wenzao wa humu jamvini ni "kutumiwa na magamba" ,lakini wakifikiria hayo na maneno ya hovyo watakayopata hawana hamu kuja hapa jamvini.

Kila jambo linaloibuka linavishwa joho la Chama, iwe mgomo wa madaktari au mijadala bungeni.Ukionekana una mawazo tofauti utabandikwa majina kibao ya ajabu na kashfa za kumwaga.

Nashauri kama mtu unaipenda CDM hebu njoo na hoja milioni 1 kuliko kuja na kejeli hata 1.Na pia Viongozi wa CDM na member wenye mtazamo chanya wakiona kuna thread ambayo ina mwelekeo wa kukikosoa au kukishauri chama haraka wajibu hoja kiukomavu au hata kukubaliana na ukosoaji. Hii itakuwa kama inatoa mwongozo kwa wale wenye haraka ya kujibu kutafakari kwanza.

Chama kikiwa na zaidi ya nusu ya wapiga kura wa aina ya hawa jamaa, kitageuka na kuwa hakifai kushika hatamu za uongozi. Chama kikiwa na wapiga kura zaidi ya nusu wa aina yako. Kitakuwa chama bora kabisa kushika hatamu za uongozi. Mnayo kazi nzito ya kutoa semina kwa aina hiyo ya wanachama. Vinginevyo, wana CDM wenye uchungu halisi mtavunishwa mabua na wanachama wa aina hii. Tusichoke, tuzidi kuwapa somo. Hata Roma haikujengwa kwa siku moja.
 
. Nimegundua tatizo... kuniingiza kwenye ushabiki na malumbano ya kichama......ok,kama huna upande wowote,unagunduaje kuwa upande una mapungufu?afterall a how does a third party have great concerns to un interested party? ivi unatumia akili gani kugundua kuwa uko katitaki?na katikati ni wapi?unaweza ukaisi ivi kumbe sio katkati bali mguu umegusa upande mmoja zaidi?tuachane na uchama tujenge taifa huru,..one who is not against anything,is one who is against everthing!
 
Kama ulivyojisemea mwenyewe kichaa akikwambia nyoka usipuuze, ahsante kichaa kwa ushauri wako. Lakini kwa mwenye uelewa makini huu sio muda mzuri wa kutoa ushauri huu. Inawezekana umechelewa au muda haukafika.
Umri wa CHADEMA na CCM sio hoja kwani sheria inayounda mfumo vyama vingi ilikuja baada ya CCM kuanzishwa.
Jaribu kusoma siasa za dunia za wakati huu, utakiona kifo cha CCM katika muda mfupi unaokuja.
Kifo cha CCM kinakuja karibuni bila matumizi ya nguvu wala pesa. Kuna mbinu moja ya kimuundo ambayo iko kwenye mchakato, sio busara kuijadili hapa inatosha sana kuimaliza CCM hata kabla ya uchaguzi mkuu wa 1215.

Wana CHADEMA hawajatukana mamba, wanajaribu kumfanya awe rafiki wao ili wavuke bila matatizo.
 
ndugu juma mi sawa nakubali kuitwa mbumbumbu au mbumbuka kwa vijineno vyako vya kumbumba ambavyo hata ktk aina za nyumbulisho wa kiswahili sanifu hakuna...tatizo ni kuleta ushauri hewa ...pia unajifanya mwema wakati ndo umejawa na kejeli na maneno ya ajabu...unasema hata ARV haziwatoshi waliokupinga,je waweza kudai unatumia akili kweli juma?...dawa ya moto ni moto...ukiongea vibaya utegemee kupata jibu baya...sorry we are ready to call a spade a spade and not a big spoon...ivo pokea haki yako kama ulivota

Sawa Mh Mbumbuka, najilazimisha sana kukusaidia ili uelewe lakini kila post yako naona unayumba huku na huko kama mlevi. Kuna faida ndogo sana wakati wa kumpigia mbuzi gitaa kwa kutegemea atakusikia na kukata mauno. Faida utakayopata ni kuongeza ujuzi tu wa kudonoa nyuzi za gitaa hilo. Ni muda wa kucheki mechi sasa, kwa heri kwa muda rafiki.
 
Kujibu pumba, na utumbo ndo kuleta maendeleo? Mmetumwa ili CDM kionekane chama cha wapumbavu?

kwani ndugu kuna mtu kataja kuwa yeye ni cdm au kwa woga wako unaona ucdm?ndo ivo kama unaogopa gizani ata ukiona mti unaanza kujiuliza kuwa ama umeona shetani,au muujiza au jini refu,ni uoga tu...hata usemeje,hautaweza kutarnish image ya cdm kwa kutuhusisha sisi na cdm,hata cdm ikifa leo bado tutazidi kupinga udhalimu...watoto wa wakulima tumepata elimu kwa tabu na hatutaacha
 
Chama kikiwa na zaidi ya nusu ya wapiga kura wa aina ya hawa jamaa, kitageuka na kuwa hakifai kushika hatamu za uongozi. Chama kikiwa na wapiga kura zaidi ya nusu wa aina yako. Kitakuwa chama bora kabisa kushika hatamu za uongozi. Mnayo kazi nzito ya kutoa semina kwa aina hiyo ya wanachama. Vinginevyo, wana CDM wenye uchungu halisi mtavunishwa mabua na wanachama wa aina hii. Tusichoke, tuzidi kuwapa somo. Hata Roma haikujengwa kwa siku moja.


Ni muhimu kuwa na chama ambacho kina sura zote za kiuongozi kuanzia kwa viongozi wenyewe na kwa wanachama pia kwa sababu Tanzania itaendelea kuwepo hata baada ya 2015.Inatakiwa wana-CDM wawathibitishie wenye mashaka ya kama wanaweza kushika na kudhibiti dola (ambao wako wengi) kwamba hiki ni chama kilichodhamiria kuleta mabadiliko chanya kwenye maisha yao baada ya uchaguzi.

Kwa fikra zangu hapa ni mahali pa ku-set ajenda na mitizamo chanya ya kukisaidia chama badala kuwa na mkusanyiko wa kutoa sifa kwa viongozi,maneno ya hovyo,taarifa mbaya za yanayowafika wapinzani wa CDM n.k
 
. Nimegundua tatizo... kuniingiza kwenye ushabiki na malumbano ya kichama......ok,kama huna upande wowote,unagunduaje kuwa upande una mapungufu?afterall a how does a third party have great concerns to un interested party? ivi unatumia akili gani kugundua kuwa uko katitaki?na katikati ni wapi?unaweza ukaisi ivi kumbe sio katkati bali mguu umegusa upande mmoja zaidi?tuachane na uchama tujenge taifa huru,..one who is not against anything,is one who is against everthing!

Hoja zako za kitoto sana. Dunia ya leo unaweza kweli kuuliza maswali haya? Eti kuku ana miguu miwi..........ngo'ombe ana miguu mi nn.........nne jumlisha nne sawa sawa na na..........Sasa unauliza nikiwa katiti ntasimama vipi. Nimekwambia sifungamani na upande wowote.
 
Back
Top Bottom