SautiYaMnyonge
JF-Expert Member
- May 13, 2018
- 439
- 742
Ikiwa ni miezi michache kabla ya uchaguzi mkuu wa udiwani, ubunge na urais Oktoba mwaka huu wanachama katika vyama mbalimbali vya siasa wamejitokeza kutaka kumrithi mbunge wa sasa James Francis Mbatia wa chama cha NCCR MAGEUZI.
Tangu kuanza kwa mara ya kwanza uchaguzi mkuu uliovihusisha vyama vingi vya siasa mwaka 1995, CCM imefanikiwa kuliongoza jimbo hilo mara moja mwaka 2005-2010 chini ya mbunge wake Mhe Aloyce Bent Kimaro.
1995-2000 Mhe James Francis Mbatia NCCR MAGEUZI.
2000-2005 Meja mstaafu Mhe Jeremiah Makundi kupitia TLP.
2005-2010 Mhe. Aloyce Bent Kimaro kupitia CCM.
2010-2015 Mhe Augustine Lyatonga Mrema kupitia TLP
2015-2020 Mhe James Francis Mbatia kupitia NCCR MAGEUZI.
2020-2025 nani kuliongoza jimbo hili?
Wafahamu makada 11 wanaotajwa kumrithi Mbatia Jimbo la Vunjo.
1. Mhe Dkt Charles Kimei mkurugenzi mstaafu wa CRDB. Huyu inaelezwa akijitokeza CCM inaweza kupita bila kupingwa katika jimbo hili.
2. Mhe Regina Chonjo Mkuu wa Wilaya Morogoro mjini mpaka sasa.
3. Mhe Crispin Theobald Meela aliyekuwa mgombea ubunge jimbo hilo mwaka 2010, akashindwa na Mhe Mrema. Baadae akateuliwa ukuu wa wilaya Rungwe na Babati kabla ya kutumbuliwa na Rais MAGUFULI.
4. Mhe Elias Nawera aliteuliwa kuwa mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Songwe katika awamu hii ya Rais MAGUFULI lakini alitumbuliwa kwa kuendekeza migogoro.
5. Mhe Innocent Meleck Shirima huyu ndiye alikuwa mgombea ubunge wa jimbo hilo mwaka 2015 na kushindwa vibaya na James Mbatia.
6. Mhe Peter Msaki kwa sasa ni Mjumbe wa kamati ya siasa mkoa wa Lindi.
7. Mhe Emanuel Mlaki huyu aliihama CCM mwaka 2011 na kujiunga na chadema akiwa kijana mtiifu wa Prof. Ndesamburo wakati huo akiwa mwenyekiti wa chadema mkoa wa Kilimanjaro na kanda ya Kaskazini ambapo aliweza kuwa katibu wa chadema wilaya Ya Moshi Vijijini. Baadae mwaka 2018 alitangaza kurejea CCM kwa ushawishi wa familia yake hususani Mama yake mdogo Rita Mlaki.
8. Mhe Laurent Mlaki huyu ni mtoto wa Toflo Mlaki na Rita Mlaki aliyewahi kuwa naibu waziri wa ardhi awamu ya kwanza ya Rais Kikwete.
9. Mhe Elinisaidie Msuri huyu kwa sasa ni mjumbe wa wa bodi ya TANROADS kipindi cha pili sasa. Huyu anatajwa kuwa na nafasi nzuri zaidi na kuwa mtu sahihi kwa sasa ili kumaliza siasa za makundi ndani ya CCM lakini anayeweza kuaminika kuingia serikalini.
10. Mhe Aloyce Bent Kimaro aliyewahi kuwa Mbunge wa Jimbo la Vunjo mwaka 2005-2010 na anatajwa ndiye mbunge anayeonekana kufanya kazi nzuri kuliko wengine tangu 1995-2020. Anapewa nafasi kubwa pia.
11. Mhe Gulatone MASIGA huyu alikuwa Mwenyekiti wa UVCCM wilaya ya Moshi Vijijini, Mgombea ubunge kura za maoni ndani ya CCM 2015, alikuwa moja ya washiriki wa timu ya kampeni za urais 2015 zilizomuingiza Rais MAGUFULI Ikulu. Anatajwa kuwa mwenye ushawishi mkubwa kwa makundi yote katika jimbo hilo japo anatajwa kutofahamika alipo kwa sasa.
Tangu kuanza kwa mara ya kwanza uchaguzi mkuu uliovihusisha vyama vingi vya siasa mwaka 1995, CCM imefanikiwa kuliongoza jimbo hilo mara moja mwaka 2005-2010 chini ya mbunge wake Mhe Aloyce Bent Kimaro.
1995-2000 Mhe James Francis Mbatia NCCR MAGEUZI.
2000-2005 Meja mstaafu Mhe Jeremiah Makundi kupitia TLP.
2005-2010 Mhe. Aloyce Bent Kimaro kupitia CCM.
2010-2015 Mhe Augustine Lyatonga Mrema kupitia TLP
2015-2020 Mhe James Francis Mbatia kupitia NCCR MAGEUZI.
2020-2025 nani kuliongoza jimbo hili?
Wafahamu makada 11 wanaotajwa kumrithi Mbatia Jimbo la Vunjo.
1. Mhe Dkt Charles Kimei mkurugenzi mstaafu wa CRDB. Huyu inaelezwa akijitokeza CCM inaweza kupita bila kupingwa katika jimbo hili.
2. Mhe Regina Chonjo Mkuu wa Wilaya Morogoro mjini mpaka sasa.
3. Mhe Crispin Theobald Meela aliyekuwa mgombea ubunge jimbo hilo mwaka 2010, akashindwa na Mhe Mrema. Baadae akateuliwa ukuu wa wilaya Rungwe na Babati kabla ya kutumbuliwa na Rais MAGUFULI.
4. Mhe Elias Nawera aliteuliwa kuwa mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Songwe katika awamu hii ya Rais MAGUFULI lakini alitumbuliwa kwa kuendekeza migogoro.
5. Mhe Innocent Meleck Shirima huyu ndiye alikuwa mgombea ubunge wa jimbo hilo mwaka 2015 na kushindwa vibaya na James Mbatia.
6. Mhe Peter Msaki kwa sasa ni Mjumbe wa kamati ya siasa mkoa wa Lindi.
7. Mhe Emanuel Mlaki huyu aliihama CCM mwaka 2011 na kujiunga na chadema akiwa kijana mtiifu wa Prof. Ndesamburo wakati huo akiwa mwenyekiti wa chadema mkoa wa Kilimanjaro na kanda ya Kaskazini ambapo aliweza kuwa katibu wa chadema wilaya Ya Moshi Vijijini. Baadae mwaka 2018 alitangaza kurejea CCM kwa ushawishi wa familia yake hususani Mama yake mdogo Rita Mlaki.
8. Mhe Laurent Mlaki huyu ni mtoto wa Toflo Mlaki na Rita Mlaki aliyewahi kuwa naibu waziri wa ardhi awamu ya kwanza ya Rais Kikwete.
9. Mhe Elinisaidie Msuri huyu kwa sasa ni mjumbe wa wa bodi ya TANROADS kipindi cha pili sasa. Huyu anatajwa kuwa na nafasi nzuri zaidi na kuwa mtu sahihi kwa sasa ili kumaliza siasa za makundi ndani ya CCM lakini anayeweza kuaminika kuingia serikalini.
10. Mhe Aloyce Bent Kimaro aliyewahi kuwa Mbunge wa Jimbo la Vunjo mwaka 2005-2010 na anatajwa ndiye mbunge anayeonekana kufanya kazi nzuri kuliko wengine tangu 1995-2020. Anapewa nafasi kubwa pia.
11. Mhe Gulatone MASIGA huyu alikuwa Mwenyekiti wa UVCCM wilaya ya Moshi Vijijini, Mgombea ubunge kura za maoni ndani ya CCM 2015, alikuwa moja ya washiriki wa timu ya kampeni za urais 2015 zilizomuingiza Rais MAGUFULI Ikulu. Anatajwa kuwa mwenye ushawishi mkubwa kwa makundi yote katika jimbo hilo japo anatajwa kutofahamika alipo kwa sasa.