Wamiliki wengi wa majokofu/friji wanauelewa mdogo juu ya utendaji kazi wake

Infopaedia

JF-Expert Member
Oct 28, 2011
1,231
1,487
Pia kama una AC, hapa panakuhusu.

Twende moja kwa moja kwenye mada. Watu wengi tunamiliki majokofu au friji lakini tunauelewa mdogo juu ya utendaji wa hichi kifaa. Kimsingi, kama mtumiaji hautakiwi kuwa na uelewa sana juu ya utendaji wa jokofu lako. Wataalamu au mafundi wanaohudumia jokofu lako wakati wa matatizo ndio wanatakiwa wawe na uelewa na wakupe miongozo mbalimbali juu ya kifaa chako. Kwa bahati mbaya sana, mafundi wengi wa majokofu hawana uelewa huo. Hapa ndipo tatizo linapoanzia na kukulazimu mmiliki wa jokofu uwe na ABC fulani juu ya kifaa chako, kitu ambacho si cha lazima sana. Na hapo ndipo nilipoona kuna haja ya kuleta kwenu uzi huu.

Kiini cha uzi huu ni kuhusu tatizo la ujazaji wa gesi kwenye majokofu yetu Pamoja na AC za majumbani kwetu.

Ili tuweze kuelewana vizuri, naomba nielezee jinsi mfumo wa upoozaji ndani ya jokofu unavyofanya kazi.

Kimsingi mfumo wa upoozaji kwenye jokofu lako una sehemu kuu kama tatu hivi. Yaani COMPRESSOR, CONDENSER, NA EVAPORATOR.

Compressor kazi yake ni kuisukuma gesi iweze kuzunguka kwenye mfumo wa upoozaji. Inaisukuma gesi kwenda kwenye EVAPORATOR, ikitoka kwenye EVAPORATOR inaenda kwenye CONDENSER na kurudi tena kwenye COMPRESSOR, mzunguko unaanza tena na kuendelea. CONDENSER na EVAPORATOR ni mirija au tube katika muundo wa zigizaga zilizotengenezwa kwa shaba au malighafi nyingine yoyote inayoweza kubadilishana jotoridi kwa wepesi kama kielelezo cha mchoro kinavyoonyesha hapo chini.

Friji3.png

Wakati gesi inafanya mzunguko au inazungushwa kati ya CONDENSER na EVAPORATOR ndipo inapofanya upoozaji. EVAPORATOR huwa iko ndani ya jokofu, yaani mule kwenye kabati ya baridi. CONDENSOR huwa nje ya jokofu upande wa nyuma. Gesi wakati inazunguka, ikipita kwenye EVAPORATOR inachukua lile joto na kwenda nalo nje kwenye CONDENSOR. Ikifika kwenye CONDENSOR inaliachia lile joto na gesi kuwa imepoa, inarudi tena kwenda kukusanya joto ndani ya jokofu na kulileta nje na kuliachia. Kwa gesi kufanya mzunguko huo na kazi ya kutoa joto ndani ya jokofu, ndani ya jokofu hubaki na ubaridi. Hapo chini kuna kielelezo cha picha
kikionyesha jinsi mpangilio wa COMPRESSOR, EVAPORATOR, na CONDENSER unavyokuwa kwenye jokofu.



Friji.png


GESI

Tumeona kwamba, gesi kwenye jokofu kazi yake ni kuzunguka, kuchukua joto ndani ya jokofu na kulileta nje na kuliachia. Inasukumwa kurudi ndani kuchukua tena joto kupitia EVAPORATOR, inakujanalo nje na kuliachia kupitia CONDENSER.

TAMBUA

Katika hali ya kawaida, gesi katika jokofu lako haitakiwi kuisha. Tumeona hapo juu jinsi gesi inavyofanya kazi ndani ya jokofu lako. Haiungui kama mafuta ya gari tuseme kwamba inaisha. Gesi ipo kwenye mzunguko wa mduara ambao umefungwa na hufanya kazi kupitia mirija kama tulivyoelezana hapo juu. Yaani unaweza ukazaliwa mpaka unazeeka, jokofu lako likawa linapoza kama kawaida. Na bahati mbaya sana mafundi wengi wa mifumo ya kupooza hawajui kwamba gesi haitakiwi kuisha katika hali ya kawaida.

Sababu moja kubwa ya kuisha gesi kwenye jokofu ni kuvuja kwa gesi. Pale ambapo kunakuwa na tundu kwenye mfumo wa mzunguko wa gesi na gesi kuanza kuvuja.

Kwanza fundi anatakiwa atatue tatizo la kuvuja kwa gesi ndipo ajaze gesi kwenye kifaa chako. Tofauti na hapo anakupa suluhu ya muda mfupi tu kwa kujaza gesi bila kuzuia kuvuja. Baada ya muda mfupi utamtafuta akujazie tena gesi. Kisheria huu ni wizi. Yawezekana wanafanya makusudi, inawezekana pia hawajui kwamba lazima kutakuwa na tatizo la gesi kuvuja sababu katika hali ya kawaida gesi haitakiwi kuisha. Pia inawezekana fundi anajua ila hataki kujisumbu. Au anajua ila anauhakika hutamlipa gharama za kutafuta leakage au panapovuja.

Kama una jokofu lako ambalo unajaza gesi kila baada ya muda Fulani, sasa ni wakati wa kulitengeneza na kuzuia kuvuja ili kuepuka gharama zisizo za lazima. Fundi anatakiwa atafute gesi inapovujia, adhibiti hiyo sehemu. Baada ya hapo atafanya majaribio ya kuhakiki kama mfumo hauna sehemu inayovujisha gesi. Jaribio hilo atalifanya kabla ya kujaza gesi. Na jaribio hilo la kuhakiki afya ya mfumo linaitwa ‘pressure test’. Baada ya kufanya pressure test na kujiridhisha afya ya mfumo wa upoozaji, atafanya ‘vacuum’. Hapa ataondoa hewa iliyoingia kwenye mfumo wa upoozaji. Sababu baada ya gesi kuvuja na kuisha, hewa ya kawaida huchukua nafasi na kuingia kwenye mfumo. Hii hewa haitakiwi. Endapo gesi itajazwa bila kutoa hewa iliyoingia, ufanisi wa gesi kupooza utapungua na utashangaa kwamba jokofu langu sikuhizi halipoozi vizuri. Ni kama mafuta ya gari uchanganye na kimiminika kingine. Lazima ufanisi wa mafuta utapungua. Ndani ya mfumo wa kupooza inatakiwa iingie gesi peke yake ili ifanye kazi kwa ufanisi wa juu.

Katika pitapita yangu na kukutana na mafundi wa mifumo ya kupooza, sikumbuki kumuona fundi ana ‘vacuum pump’. Yaani pump au kifaa cha kuondolea hewa kwenye mfumo wa kupooza wa jokofu au AC.

Nawatakia upambanaji mwema.



Wakatabahu

Infopaedia
 
Hongera mtoa mada

Ila kuna vitu umechanganya kidogo

Uhalisia ni kwamba

Gesi ikitoka kwenye compresor huwa inashika joto so direct inapitishwa kwenye condensor ili ipoozwe na hata ikipoozwa haiwi na ule ubaridi kabisa, ubarid unatokea kwenye expansion valve

Expansion valve inaletaje ubaridi?

Natolea mfano wa perfume, ukijipulizia perfume kuna kaubaridi fulan huwa unakapata na kale kaubaridi kanazalishwa na ile valve unavyoibonyeza pale ili kujispray, same same to refrigeration system expansion valve ndiyo inazalisha ubarid kwa kuspray freon gas kabla haijaingia kwenye evaporator.

Mengine upo sawa ila hapo tu ndo ulichanganya mtoa mada
 
Hongera mtoa mada

Ila kuna vitu umechanganya kidogo

Uhalisia ni kwamba

Gesi ikitoka kwenye compresor huwa inashika joto so direct inapitishwa kwenye condensor ili ipoozwe na hata ikipoozwa haiwi na ule ubaridi kabisa, ubarid unatokea kwenye expansion valve

Expansion valve inaletaje ubaridi?

Natolea mfano wa perfume, ukijipulizia perfume kuna kaubaridi fulan huwa unakapata na kale kaubaridi kanazalishwa na ile valve unavyoibonyeza pale ili kujispray, same same to refrigeration system expansion valve ndiyo inazalisha ubarid kwa kuspray freon gas kabla haijaingia kwenye evaporator.

Mengine upo sawa ila hapo tu ndo ulichanganya mtoa mada
Nashukuru kwa pongezi kaka. Wakati naandika huu uzi niliwalenga watumiaji wa majokofu. Hivyo sikutaka kuwachosha sana na habari za kitaalamu.

Mkuu Buzitata kazi ya Thermostatic expansion valve ni kuibadili gesi kutoka maji maji na kuwa mvuke. Hii gesi ikiwa katika mfumo wa mvuke ina tabia ya kufyonza joto, hata liwe kidogo italifyonza.

Yaani inatabia ya kuhitaji joto ikiwa kwenye mfumo wa mvuke ndani ya evaporator. Baada ya hapo ikipita kwenye compressor huwa imesharudia tena kwenye hali yake ya kimiminika.

Na ikiwa kwenye hali ya kimiminika, gesi ya Freon huwa na tabia ya kutoa joto. Yaani inakuwa kinyume na wakati ikiwa kwenye hali ya mvuke. Inakuwa inafyonza au inahitaji zaidi ubaridi. Baada ya hapo inapita tena kwenye expansion valve, expansion valve inaigandamiza na kui-spray ndani ya evaporator kuwa hali ya mvuke na mzunguko unaendelea.

Jokofu hutumia kanuni ya kuondoa joto ili kupata ubaridi. Nikupe mfano wa giza na mwanga. Kwa asili dunia ni giza. Taa au jua likiwaka ndio hulizidi giza japokuwa wakati wote giza lipo. Kinachotokea ni kwamba mwanga unalizidi uwiano giza, basi giza halionekani.

Na kwa habari ya joto na baridi ni hivyo hivyo. Dunia yetu ni baridi isipokuwa msuguwano ndio husababisha joto na kuja kuiondoa baridi, japo baridi wakati wote ipo ila uwiano na joto au jotoridi huegemea upande wa joto hivyo tunahisi joto zaidi. Ama jotoridi ikiegemea upande wa baridi tunasema kuna baridi.

Kwahiyo jokofu hutumia kanuni ya kuliondoa joto, kinachobaki ni ubaridi. Hakuna kitu kinachotengeneza ubaridi kwenye jokofu.
 
Kwa kuongezea. Kwa sasa tuna aina 2 za Compresors. Kuna (1.)non Invetors ( karibia hizi Used zote toka Nje na friji/AC zenye zaidi ya miaka 4 ) 2. Invetors Compresors- hizi Friji/AC zinauzwa sambamba na Non Invetors Friji na AC. Inventor Compressor Friji/AC ulaji wake wa Units za Umeme ni mdogo mno zipo zinazotumia Units za Umeme wa kuanzia laki 3 kwa mwaka mzima (360 Days-Ikiwa ON siku zote hizo bila Kuzimwa). Ili kuondokana na kazia ya kuzima friji usiku- utamaduni wa watanzania wengi😁 Nunua Friji yenye inventor compresor System. Mafundi wengi hapa Tanzania ukiwapeleka dead invetor Compresor Refigirator wana tabia ya kuondoa hii system na kukufungia compresor ya kawaida so kuwa makini sana na hilo
 
Nashukuru kwa pongezi kaka. Wakati naandika huu uzi niliwalenga watumiaji wa majokofu. Hivyo sikutaka kuwachosha sana na habari za kitaalamu.
Mkuu Buzitata kazi ya Thermostatic expansion valve ni kuibadili gesi kutoka maji maji na kuwa mvuke. Hii gesi ikiwa katika mfumo wa mvuke ina tabia ya kufyonza joto, hata liwe kidogo italifyonza. Yaani inatabia ya kuhitaji joto ikiwa kwenye mfumo wa mvuke ndani ya evaporator. Baada ya hapo ikipita kwenye compressor huwa imesharudia tena kwenye hali yake ya kimiminika. Na ikiwa kwenye hali ya kimiminika, gesi ya Freon huwa na tabia ya kutoa joto. Yaani inakuwa kinyume na wakati ikiwa kwenye hali ya mvuke. Inakuwa inafyonza au inahitaji zaidi ubaridi. Baada ya hapo inapita tena kwenye expansion valve, expansion valve inaigandamiza na kui-spray ndani ya evaporator kuwa hali ya mvuke na mzunguko unaendelea.
Jokofu hutumia kanuni ya kuondoa joto ili kupata ubaridi. Nikupe mfano wa giza na mwanga. Kwa asili dunia ni giza. Taa au jua likiwaka ndio hulizidi giza japokuwa wakati wote giza lipo. Kinachotokea ni kwamba mwanga unalizidi uwiano giza, basi giza halionekani.
Na kwa habari ya joto na baridi ni hivyo hivyo. Dunia yetu ni baridi isipokuwa msuguwano ndio husababisha joto na kuja kuiondoa baridi, japo baridi wakati wote ipo ila uwiano na joto au jotoridi huegemea upande wa joto hivyo tunahisi joto zaidi. Ama jotoridi ikiegemea upande wa baridi tunasema kuna baridi.
Kwahiyo jokofu hutumia kanuni ya kuliondoa joto, kinachobaki ni ubaridi. Hakuna kitu kinachotengeneza ubaridi kwenye jokofu.
Sawa mtoa mada, ila lengo langu nilitaka ujue kitu unachokichanganya, i hope hii kitu umeitoa darasani ila haya mambo kila siku huwa nadili nayo.

Ubaridi unazalishwa kwenye expansion valve hapa inabidi ukubali tu mtoa mada hata kama huelewi wewe meza kama lilivyo.

Kuna mengi kwenye hizi system
 
Sawa mtoa mada, ila lengo langu nilitaka ujue kitu unachokichanganya, i hope hii kitu umeitoa darasani ila mm hii mimi haya mambo kila siku nacheza nayo.

Ubard unazalishwa kwenye expansion valve hapa inabd ukubali tu mtoa mada hata kama huelewi ww ameza kama lilivyo.

Kuna mengi kwenye hizi system
Asante mkuu. Kuna kitu nimejifunza pia.
 
Uzi umekaa vizuri

Utajuaje kama freezer ina tatizo la gas
Kiujumla tatizo lolote likitokea kwenye gesi basi jokofu hupoteza ufanisi wake wa kupoza. Japo tatizo la kutopooza linaweza kusababishwa na kadhia anuwai tofauti na gesi. Ila nahisi kama vile unataka kujua utajuwaje kama gesi inavuja. Ni vigumu kujua kama gesi inavuja mpaka pale madhara au matokeo ya kuvuja yanapo jitokeza. Madhara yakijitokeza ndipo sataalamu wanaweza kufanya vipimo na kugundua. Lakini kwa mtumiaji kujua kabla ya madhara ni ngumu kidogo.
 
Kwa kuongezea. Kwa sasa tuna aina 2 za Compresors. Kuna (1.)non Invetors ( karibia hizi Used zote toka Nje na friji/AC zenye zaidi ya miaka 4 ) 2. Invetors Compresors- hizi Friji/AC zinauzwa sambamba na Non Invetors Friji na AC. Inventor Compressor Friji/AC ulaji wake wa Units za Umeme ni mdogo mno zipo zinazotumia Units za Umeme wa kuanzia laki 3 kwa mwaka mzima (360 Days-Ikiwa ON siku zote hizo bila Kuzimwa). Ili kuondokana na kazia ya kuzima friji usiku- utamaduni wa watanzania wengi Nunua Friji yenye inventor compresor System. Mafundi wengi hapa Tanzania ukiwapeleka dead invetor Compresor Refigirator wana tabia ya kuondoa hii system na kukufungia compresor ya kawaida so kuwa makini sana na hilo

Hivi friji ukiliacha tu liwake kila siku kuna shida?
 
Back
Top Bottom