Wamaasai wasikitishwa na mavazi aliyovaa Diamond

Ngongo

JF-Expert Member
Sep 20, 2008
18,930
31,169
WAMASAAI WAMESEMA MAVAZI ALIYOVAA *DIAMOND KATIKA TUZO HUKO BET NI MAVAZI YA KIKE

Urembo aliovaa shingoni kuanzia alioubana na ulioning'inia ni mavazi ya wanawake wanaovuka rika.

Pia nguo aliyovaa ni yakike na haivaliwagi kama khanga au taulo kama umetoka kuoga.

Kitu pekee alichobeba cha kiume ni Sime na Ngao

Kikao ndio tumekimaliza na kilisimamiwa na *Leigwanan Selevie
1624946393202.png
 
Alitakiwa awashirikishe wadau wenyewe wa kimasai bila shaka kabla ya kukurupuka yeye mwenyewe na wapambe wake, na kujipamba kama mwanamke aliyevuka rika!!
 
Kikao kimepisha adhabu ya fimbo 70 iwapo Diamond atakanyaga maeneo ya Wamaasai kwasababu ya kufedhehesha na kudharau mila.

Kikao kimepitisha kwa kauli moja kwamba mtu au kikundi kitakachotumia mavazi yao au kitu chochote kinachohusiana na mila zao kupata ushauri kabla vinginevyo viboko 70 vitahusika.
 
WAMASAAI WAMESEMA MAVAZI ALIYOVAA *DIAMOND KATIKA TUZO HUKO BET NI MAVAZI YA KIKE.
Urembo aliovaa shingoni kuanzia alioubana na ulioning'inia ni mavazi ya wanawake wanaovuka rika*
Pia nguo aliyovaa ni yakike na haivaliwagi kama khanga au taulo kama umetoka kuoga.
Kitu pekee alichobeba cha kiume ni Sime na Ngao

Kikao ndio tumekimaliza na kilisimamiwa na *Leigwanan Selevie
Ni kweli nadhani alishauriwa vibaya; alibeba ngao bila mkuki!
 
WAMASAAI WAMESEMA MAVAZI ALIYOVAA *DIAMOND KATIKA TUZO HUKO BET NI MAVAZI YA KIKE.
Urembo aliovaa shingoni kuanzia alioubana na ulioning'inia ni mavazi ya wanawake wanaovuka rika*
Pia nguo aliyovaa ni yakike na haivaliwagi kama khanga au taulo kama umetoka kuoga.
Kitu pekee alichobeba cha kiume ni Sime na Ngao

Kikao ndio tumekimaliza na kilisimamiwa na *Leigwanan Selevie
Ngongo Am sure wamasai wamekurupuka kwakuwa Mond hakuvaa kimasai bali alivaa kisanii.. Wakumbuke hayakuwa maonesho ya kitamaduni bali ya kisanii ya kugombea tuzo za kimziki...Vile vionjo vyote ni kwa ajili ya usanii zaidi kuliko utamaduni
 
Back
Top Bottom