Waliosoma Tosamaganga High School


Aisee Mama mingoi alikuwa analeta wali "mtamu" pia mpolee
 
mmenikumbusha mbali sana enzi hizo, mpishi mkuu Mlunza the great babu wa Sumu.
manesi ipamba unajifanya unaumwa ili uende kwa kimada tu.
zoooo...( iringa girls)
migomo ndo ilikuwa shidaaaaa
Mlunza nasikia kafukuzwa kazi mkuu
 
daaah pole yakee ila katumika pale kitambo....
alikuwa siku za jmosi tukienda kukata nyama anatupa nyama na viungo tunapika wenyewe basi siku hiyo tunakula sumu kiroho safiiiiiii kabisa
 
Sisi tuliosoma enzi miaka ya 2001 kulikuwa na kitu kinaitwa E.M.O kuna mzee mmoja nadhani alikuwa mhasibu wa shule anaenda mjini postal bank anakuja na majina ya waliopata EMO yanabandikwa pale staff kwa nje aisee ukiona jina unafurahi sana. EMO kwa saaa ndio hizi MPESA, Tigo Pesa etc. kweli mambo yanaenda kasi.
 

mkiona majina yamebandikwa mnaongezea na peni majina ya watu ambao kwao E.M.O ni ndoto [emoji3]
 
ni shule nzuri kwa majengo na kitaaluma ina mabweni kama ujamaa Mandela ni kama chuo kitaaluma inategemea management lakn 2006 kurudi nyuma enzi charwe ilikuwa inatoa TO cjui kwasasa kwakuwa should nyingi koñgwe za serikali zinapumulia machine
Mkuu Mandela bado ipo? Jengo la zamani sana lilikuwa ukitembea sakafu inatikisika unasikia mtetemeko na kudondosha vidongo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…