Ni takribani wiki tatu sasa tangu katibu mkuu utumishi autangazie umma kuwa watumishi 450 waliokuwa wamekata rufaa wameshinda nà kutakiwa warudishwe kazini. Kwa masikitiko makubwa baadhi ya halmashauri hadi leo tarehe 1/8/2017 hazijawaandia watumishi hao barua za kurudishwa kazini. Ucheleweshwaji huo unazidi kuleta simanzi kubwa kwa waathirika kwani wameshadhalilika vyakutosha lakini baadhi ya maafisa utumishi hawalioni hilo. Kuna wasiwasi huenda hata mshahara wa mwezi wa nane wasiupate. Kutokana na hili msemo wa wahenga usemao mwenye shibe hamjui mwenye njaa unathibitika. Chondechonde Katibu Mkuu Utumishi liangalie hili ili waathirika hawa wapate mshahara wao wa mwezi wa nane na mishahara yao ya nyuma tangu wafukuzwe kazi.