kifupi kirefu
JF-Expert Member
- Oct 29, 2018
- 539
- 3,507
Nimeona msimamo wa serikali dhidi ya watu wenye asili ya Burundi wanaoishi Mishamo na Katumba huko Katavi, nimeshtushwa na idadi aliyotaja Mh. Rais ya watu laki moja na sitini kuwa walipewa uraia wa Tanzania na ikanibidi nifuatilie kwenye mitandao kuhusu historia ya hao watu na walipewa lini Uraia.
Kupitia kumbukumbu za UNHCR zinataja kwamba Mh. Kikwete aliwahi kuutangazia umma na Dunia kwamba Tanzania imeamua kuwapa raia wa Burundi laki na sitini Uraia akiwa kwenye kikao cha UN. Lakini nikajiuliza Hawa watu ambao wanatoka kabila la Hutu laki na sitini kupewa Uraia na kuendelea kuishi Mishamo na Katumba siyo njia kweli imetengenezwa ya wao kuwa na utawala wao kuanzia Mbunge Hadi viongozi wengine wa kisiasa?
Kwanini tuliamua kuwapa Uraia watu wengi kiasi hiki na bila kuwachuja? Je Mhe Rais anaposema amesogeza jeshi karibu na eneo wanapoishi tafsiri yake ni kwamba Hawa bado ni raia wa Burundi yaani Wakimbizi au ni Watanzania? Kama Ni Watanzania kwanini wapewe ulinzi maaalumu au tayari wameanza chokochoko?
Serikali ipitie upya maamuzi yake na waombe pia mawazo ya wasomi mbalimbali kuhusu namna ya kuwaondoa hawa watu kutoka wanapoishi na wasambazwe maeneo mengine ya nchi. Kukaa pamoja siyo afya kwa Tanzania wala Burundi kwa sababu Kati ya watu laki moja na sitini watu mia tu wanaweza wakaanzisha vuguvugu na kuivuruga nchi yetu au asili yao.
Tukumbuke nao Ni binadamu na wanapenda kutawala siyo kuendelea kutawaliwa, Wana kiu ya kuwa viongozi na Wana haki ila Tanzania Kwanza.
Ahsante JPM kwa kuona tatizo nadhani ufumbuzi utapatikana bila kuathiri haki zao za kuishi na za kibinadamu.
Kupitia kumbukumbu za UNHCR zinataja kwamba Mh. Kikwete aliwahi kuutangazia umma na Dunia kwamba Tanzania imeamua kuwapa raia wa Burundi laki na sitini Uraia akiwa kwenye kikao cha UN. Lakini nikajiuliza Hawa watu ambao wanatoka kabila la Hutu laki na sitini kupewa Uraia na kuendelea kuishi Mishamo na Katumba siyo njia kweli imetengenezwa ya wao kuwa na utawala wao kuanzia Mbunge Hadi viongozi wengine wa kisiasa?
Kwanini tuliamua kuwapa Uraia watu wengi kiasi hiki na bila kuwachuja? Je Mhe Rais anaposema amesogeza jeshi karibu na eneo wanapoishi tafsiri yake ni kwamba Hawa bado ni raia wa Burundi yaani Wakimbizi au ni Watanzania? Kama Ni Watanzania kwanini wapewe ulinzi maaalumu au tayari wameanza chokochoko?
Serikali ipitie upya maamuzi yake na waombe pia mawazo ya wasomi mbalimbali kuhusu namna ya kuwaondoa hawa watu kutoka wanapoishi na wasambazwe maeneo mengine ya nchi. Kukaa pamoja siyo afya kwa Tanzania wala Burundi kwa sababu Kati ya watu laki moja na sitini watu mia tu wanaweza wakaanzisha vuguvugu na kuivuruga nchi yetu au asili yao.
Tukumbuke nao Ni binadamu na wanapenda kutawala siyo kuendelea kutawaliwa, Wana kiu ya kuwa viongozi na Wana haki ila Tanzania Kwanza.
Ahsante JPM kwa kuona tatizo nadhani ufumbuzi utapatikana bila kuathiri haki zao za kuishi na za kibinadamu.