sunguramjinga
Senior Member
- May 11, 2023
- 175
- 227
Ummy amesema “Gharama za kumpeleka Mgonjwa mmoja nje ya nchi ni shilingi milioni 250 wakati katika Hospitali hii ni shilingi milioni 70 tu, hivyo Hospitali imetumia shillingi milioni 770 na kama wangeenda nje ya nchi, Serikali ingetumia shilingi bilioni 2.75, hivyo jumla ya shilingi bilioni 1.98 zimeweza kuokolewa”
“Ili kuboresha huduma kwa Wagonjwa wenye matatizo ya ubongo na mishipa ya fahamu, Hospitali ya Taifa Muhimbili iliamua kuwahudumia wagonjwa hawa chini ya Hospitali ya Taifa Muhimbili - Mloganzila na kuwapangia kazi Madaktari bingwa na wabobezi wa fani hii, utaratibu huu wa kutoa huduma mahsusi chini ya Hospitali mahsusi na Mabingwa/ Wabobezi mahsusi ni msingi wa dhana ya Vituo vya Umahiri (Centres of Excellence) ambayo ndio dhana tunayoijenga kwa sasa katika utoaji wa huduma za kibingwa na kibobezi hapa nchini”