Waliokuwa Mawaziri Watiifu wa JPM Kumgeuka Sasa inaashiria Nini?

Chakaza

JF-Expert Member
Mar 10, 2007
39,801
71,226
Tumemsikia Waziri wafedha Mwigulu akitamka kuwa asemayo mama Samia kuhusu ukusanyaji kodi ni sahihi kabisa kwani utumiaji wa ubabe na hila sio njia nzuri (kama alivyokuwa anaunga mkono utendaji wa JPM), na Kigwangalla naye amepingana wazi leo na kauli alizokuwa anaziunga mkono kwa bidii kuhusu Nyungu na kujifukiza kuwa ni njia primitive zisizo na utafiti wa kisayansi tofauti kabisa na vigelegele walivyopiga kwa JPM. Funga kazi ni Nape Nnauye aliyefyatuka na kusema utawala wa sasa ni mzuri sana tofauti na uliopita.

Jee mawaziri hawa wa zamani na sasa wanataka kutupa ujumbe gani? Walikuwa wanaburuzwa na Jiwe au walikuwa wanamnafikia tuu?
Au kuna nini humo ndani ya chungu?
 
Hatari
 
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…