Waliokufa Loliondo wamsikitisha mchungaji

Serikali ya CCM imekataza watu kwenda uko ili walalahoi wanaougua wasipate tiba toka kwa Babu, wafe idadi ya Watanzania walalahoi ipungue.
 
baada ya serikali kushindwa kuboresha maisha ya mtanzania katika chakula na matibabu .... wananchi wamemwomba mungu akawaletea tiba ya bure sasa serikali imeamua kufanya mauaji kwa kuisitisha tiba iliyoletwa na mungu kwa watu wake ..... mungu ataionyesha serikali kidole chake kama alivyoleta tiba hii....!

eee mwenyezi mungu toa fundisho kwa serikali hii ya kidhalimu
 
Serikali ya CCM imekataza watu kwenda uko ili walalahoi wanaougua wasipate tiba toka kwa Babu, wafe idadi ya Watanzania walalahoi ipungue.

wao wameshakunywa.....na nyie wengine mkinywa mkipona,maNGO yanayoshughulikia maswala ya UKIMWI yatakosa kazi za kufanya kama wagonjwa watapona wote na pia hela za misaada zitapungua.....ama kweli TZ kufa kufaana
 
hehehe,labda wameona wanakosa mapato ktk hospitali zao binafsi that why wamesitisha tiba
 
wao wameshakunywa.....na nyie wengine mkinywa mkipona,maNGO yanayoshughulikia maswala ya UKIMWI yatakosa kazi za kufanya kama wagonjwa watapona wote na pia hela za misaada zitapungua.....ama kweli TZ kufa kufaana

Kaazi kweykwey!!!!
Ni ya kweli haya PRETA
 
Babu katoa angalizo kwa wale vibosile wote waliofika kwake kwa njia za panya na kupata kikombe bila kufuata utaratibu wa kupanga foleni hivyo basi dawa haitafanya kazi dhidi yao.
 
Yaani serikali sijui kwa nini imeamua kufanya hivyo wakati kuna watu wengi tu walikuwa kwenye foleni wakisubiri tiba na wengi wao hali zao zilikuwa mbaya..
 
Colleagues,

Nimesikitishwa na tamko la Serikali kufungwa kwa mda kwa huduma ya mchungaji huyo huko Loliondo. Ukweli ni kwamba kama serikali ingekuwa makini vya kutosha ingekuwa tayari imetoa matokeo ya uchunguzi wake kwa wananchi juu ya dawa hiyo. Hapa nilipo nimeona ktk picha msululu wa magari mengi ya serikali yakiwa huko. Watumishi hawa tayari walisha pata dawa na hivyo wamekuwa tayari kutoa tamko wakiwa wameishahudumiwa. Nionavyo mimi and I would stand for my vision:

Serikali itoe tamko la uchunguzi wa dawa hiyo haraka ili huduma ziendelee au zisitishwe. Kama haiwezi kufanya hivyo haraka basi iache hali hiyo ya ki-IMANI iendelee kama ilivyokuwa huko nyuma. Itoe ulinzi na resources nyingine za kumwezesha mchungaji huyo kutoa huduma hiyo. Kama serikali haiwezi, Kanisa linaweza kufanya hivyo kwa utukufu wa Mungu mwenyewe.
 
Hapana humu Jf Great thinkers ni wachache mno, na walio wengi ni malimbukeni na washabiki sana ambao kwenye isue nyingi huwa hawaoneshi hata chembe ya uzalendo.

Hivi unafahamu maana ya neno "limbuleni" au?Una siku 15 tu tangu ujiunge hapa JF lakini umeshaanza kuwa judgemental!
 
Wakubwa walishakunywa wote, nyie wengine mkiosa si vibaya. Ila ni laana jkuwa kwa maamuzi ya kinyama kama haya:rain:
watu wako pale kwa nauli ya kukopa na sasa hawapati tiba, nini kitatokea na bado ajalipa deni la nauli?
 
Ninashangazwa na wanaofanya utafiti wa dawa ya babu, yeye anageuza dawa ya miti shamba kuwa damu ya yesu bwana na mwokozi wetu, ina maana siku moja serikali itaunda pia tume kuangalia kuwa ekaristi ni kweli mwili na damu ya yesu!!!!!!!!!!!
 
Serikali ya CCM imekataza watu kwenda uko ili walalahoi wanaougua wasipate tiba toka kwa Babu, wafe idadi ya Watanzania walalahoi ipungue.
Kuwakataza utakuwa ni ujinga yaani wao waende wakanywe dawa kwa babu halafu wananchi walala hoi wazuiwe!?...
 
wao wameshakunywa.....na nyie wengine mkinywa mkipona,maNGO yanayoshughulikia maswala ya UKIMWI yatakosa kazi za kufanya kama wagonjwa watapona wote na pia hela za misaada zitapungua.....ama kweli TZ kufa kufaana
niajabu kweli...Mkwere,Lowasa,Magufuli na vigogo wengine wameshaenda kunywa dawa leo, watu wengine wakatazwe...hao polisi watakao endenda kuwazuia watapigwa mishale ohhhhhhhhhhhhhh
 
Hata kama dawa yake haifanyi kazi mbona kuna watu kibao waganga wa kienyeji wameachiwa wanauza dawa ambazo twajua hazifanyi kazi? Wamwache mzee wa watu atibu wagonjwa wasio na matumaini hata kama binafsi siiamini tiba yake.
 
Nasubiri Tamko la Viongozi wangu wa Dini,maana Loliondo unatoa 500 kwa babu.300 kwa ajili ya ujenzi wa Kanisa na 200 kwa ajili ya babu.
Sasa kwann nistoe 200 tu??? wapi Tamko????
 
Hapana humu Jf Great thinkers ni wachache mno, na walio wengi ni malimbukeni na washabiki sana ambao kwenye isue nyingi huwa hawaoneshi hata chembe ya uzalendo.
mnafki mkubwa wewe umejiunga juzi tuu umeanza kujudge the book by its cover hebu tuliza akili then ujue mambo yanendaje humu sio kuingia tu na kutupia upupu wako hapa
 
Back
Top Bottom