Waliojenga kibanda cha Mlinzi kwa Tsh. Milini 11 wafikishwa Mahakamani

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,376
8,118
Watumishi hao ni Dkt. Zakayo Kyomo ambaye ni Kaimu Mkuu wa chuo cha VETA, Projestus Kabyemela (Mhasibu), Waziri Shaban Waziri (Mgavi) na Upendo Aidan Nindi (Afisa Ununuzi).

Watumishi hao wanashitakiwa kwa Matumizi Mabaya ya Mamlaka kinyume na kifungu cha 31 cha Sheria ya Uhujumu Uchumi sura ya 329 na Shitaka la pili ni kuisababishia Serikali hasara ya Tsh. Milioni 22.8 kinyume na kifungu 284 A (1) iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2022.

Washitakiwa walishindwa kupata wadhamini waliokidhi vigezo vilivyowekwa na kupelekwa Mahabusu, shauri hilo litatajwa tena Oktoba 13, 2022.

=======================

Watumishi wanne wa chuo cha Mamlaka ya Mafunzo ya Ufundi Stadi (Veta) mkoani hapa wamepandishwa kizimbani katika mahakama ya Hakimu mkazi mkoa wa Tabora wakikabiliwa na mashitaka mawili ya uhujumu uchumi.

Watumishi hao, Dk Zakayo Kyomo ambaye ni kaimu mkuu wa chuo hicho, Projestus Kabyemela (mhasibu), Waziri Shaban Waziri (mgavi) na Upendo Aidan Nindi (ofisa ununuzi), wamefikishwa mbele ya hakimu mkazi mwandamizi mkoa Tabora, Jovin Alphonce Kato leo Septemba 29.

Mashitaka yanayowakabili maofisa hao ni pamoja na shauri la uhujumu uchumi Namba 36 la mwaka 2022 yaliyosomwa na wakili wa Takukuru, Yunis Masalu.

Katika shauri hilo, watumishi hao wanashitakiwa kwa matumizi mabaya ya mamlaka kinyume na kifungu cha 31 cha Sheria ya Uhujumu Uchumi sura 329 na shitaka la pili ni kuisababishia mamlaka hasara ya Sh22.8 milioni kinyume na kifungu 284 A (1) iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2022.

Masalu amesema makosa hayo yamefanywa katika kipindi cha Februari 22, 2022 na Mei 25, 2022.

Wakili wa washitakiwa hao, Kelvin Kayaga amesema kwa kuwa dhamana iko wazi, atahakikisha wanadhaminiwa.

Mahakama imeweka masharti ya dhamana kwa washitakiwa wote kuwa na wadhamini wawili kila mmoja ambao watasaini nusu ya hasara huku mmoja wa wadhamini hao awe ni mtumishi wa Umma.

Hata hivyo, washitakiwa wameshindwa kupata wadhamini waliokidhi vigezo hivyo na kupelekwa rumande na shauri hilo litatajwa tena tarehe tena Oktoba 13 mwaka huu.

Kesi hiyo ni matokeo ya ziara ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa mkoani humo, ambapo alikagua ujenzi wa chuo hicho na kubaini ubadhirifu ukiwemo ujenzi wa chumba cha mlinzi kwa gharama ya Sh11 milioni na kumwagiza mkuu wa Takukuru kufanya uchunguzi na kuwachukulia hatua za kisheria wahusika.

MWANANCHI
 
Nchi hii ni ya hovyo. Kuna wale wizara ya fedha walikula mabilion mwaka jana tume ikaundwa ikaja na ushahidi wameweka kabatini.
Huu ni upuuzi kweli, ripoti ya CAG kila mwaka inaonesha ubadhirifu wa mabilion ya pesa na hakuna haktua zozote zinachukuliwa. Sasa ziara ya waziri mkuu kukagua kibanda cha mlinzi ndo haraka haraka watu wameshtakiwa kwa uhujumu uchumi, nchi ya ajabu sana.
 
Kesi nyingine bhana mpaka raha
Hawa wanashindwa kabla ya saa 4 asubuhi
 
Hakuna kesi hapo ni uzushi tuu wa kisiasa na watatoka vizuri tuu..

Kwani kibanda cha Mlinzi linatakiwa kuwa cha Bei gani?

Mwisho kumbe siku hizi makosa ya uhujumu uchumi huwa yanakuwa na dhamana?
Tatizo vitu vingi hamjui ila mnajitia kujua,

Economic case zote Zina dhamana, mfano ukishtakiwa kwa kosa ambalo thamani yake labda milion Mia, either umeitia hasara serikali au taasisi yoyote,
Basi kisheria dhamana inakuwa wazi ila lazima utoe au mtoe nusu ya fedha ambayo unatuhumiwa kuitia hasara hiyo taasisi au serikali,
Kama hauna fedha taslimu Basi Mali yenye thamani ya hiyo fedha ,haswa nyumba. Unaacha hati mahakamani,

Kwahiyo miaka yote hayo makosa yana dhamana,ila watu huwa wanakwama kwenye suala la kuacha fedha taslimu au hati ya mali,

Maana najua hapo unataka kusema wakati wa magufuli wenu hayo makosa yalikuwa hayana dhamana,

Makosa ambayo hayana dhamana ni murder case, money laundering, arm robbery, na uhaini,
 
Tatizo vitu vingi hamjui ila mnajitia kujua,

Economic case zote Zina dhamana, mfano ukishtakiwa kwa kosa ambalo thamani yake labda milion Mia, either umeitia hasara serikali au taasisi yoyote,
Basi kisheria dhamana inakuwa wazi ila lazima utoe au mtoe nusu ya fedha ambayo unatuhumiwa kuitia hasara hiyo taasisi au serikali,
Kama hauna fedha taslimu Basi Mali yenye thamani ya hiyo fedha ,haswa nyumba. Unaacha hati mahakamani,

Kwahiyo miaka yote hayo makosa yana dhamana,ila watu huwa wanakwama kwenye suala la kuacha fedha taslimu au hati ya mali,

Maana najua hapo unataka kusema wakati wa magufuli wenu hayo makosa yalikuwa hayana dhamana,

Makosa ambayo hayana dhamana ni murder case, money laundering, arm robbery, na uhaini,
Kwamba hao maafisa hawana mil.12 au mali za thamani hiyo? Sasa si unaona huo ni uonezi kama wakuu WA idara wamekosa hizo pesa wapi walipoiba?
 
Watumishi hao ni Dkt. Zakayo Kyomo ambaye ni Kaimu Mkuu wa chuo cha VETA, Projestus Kabyemela (Mhasibu), Waziri Shaban Waziri (Mgavi) na Upendo Aidan Nindi (Afisa Ununuzi).

Watumishi hao wanashitakiwa kwa Matumizi Mabaya ya Mamlaka kinyume na kifungu cha 31 cha Sheria ya Uhujumu Uchumi sura ya 329 na Shitaka la pili ni kuisababishia Serikali hasara ya Tsh. Milioni 22.8 kinyume na kifungu 284 A (1) iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2022.

Washitakiwa walishindwa kupata wadhamini waliokidhi vigezo vilivyowekwa na kupelekwa Mahabusu, shauri hilo litatajwa tena Oktoba 13, 2022.

=======================

Watumishi wanne wa chuo cha Mamlaka ya Mafunzo ya Ufundi Stadi (Veta) mkoani hapa wamepandishwa kizimbani katika mahakama ya Hakimu mkazi mkoa wa Tabora wakikabiliwa na mashitaka mawili ya uhujumu uchumi.

Watumishi hao, Dk Zakayo Kyomo ambaye ni kaimu mkuu wa chuo hicho, Projestus Kabyemela (mhasibu), Waziri Shaban Waziri (mgavi) na Upendo Aidan Nindi (ofisa ununuzi), wamefikishwa mbele ya hakimu mkazi mwandamizi mkoa Tabora, Jovin Alphonce Kato leo Septemba 29.

Mashitaka yanayowakabili maofisa hao ni pamoja na shauri la uhujumu uchumi Namba 36 la mwaka 2022 yaliyosomwa na wakili wa Takukuru, Yunis Masalu.

Katika shauri hilo, watumishi hao wanashitakiwa kwa matumizi mabaya ya mamlaka kinyume na kifungu cha 31 cha Sheria ya Uhujumu Uchumi sura 329 na shitaka la pili ni kuisababishia mamlaka hasara ya Sh22.8 milioni kinyume na kifungu 284 A (1) iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2022.

Masalu amesema makosa hayo yamefanywa katika kipindi cha Februari 22, 2022 na Mei 25, 2022.

Wakili wa washitakiwa hao, Kelvin Kayaga amesema kwa kuwa dhamana iko wazi, atahakikisha wanadhaminiwa.

Mahakama imeweka masharti ya dhamana kwa washitakiwa wote kuwa na wadhamini wawili kila mmoja ambao watasaini nusu ya hasara huku mmoja wa wadhamini hao awe ni mtumishi wa Umma.

Hata hivyo, washitakiwa wameshindwa kupata wadhamini waliokidhi vigezo hivyo na kupelekwa rumande na shauri hilo litatajwa tena tarehe tena Oktoba 13 mwaka huu.

Kesi hiyo ni matokeo ya ziara ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa mkoani humo, ambapo alikagua ujenzi wa chuo hicho na kubaini ubadhirifu ukiwemo ujenzi wa chumba cha mlinzi kwa gharama ya Sh11 milioni na kumwagiza mkuu wa Takukuru kufanya uchunguzi na kuwachukulia hatua za kisheria wahusika.

MWANANCHI
PM amewaonea tu hao watumishi waachwe wakapige kazi.
 
Tatizo vitu vingi hamjui ila mnajitia kujua,

Economic case zote Zina dhamana, mfano ukishtakiwa kwa kosa ambalo thamani yake labda milion Mia, either umeitia hasara serikali au taasisi yoyote,
Basi kisheria dhamana inakuwa wazi ila lazima utoe au mtoe nusu ya fedha ambayo unatuhumiwa kuitia hasara hiyo taasisi au serikali,
Kama hauna fedha taslimu Basi Mali yenye thamani ya hiyo fedha ,haswa nyumba. Unaacha hati mahakamani,

Kwahiyo miaka yote hayo makosa yana dhamana,ila watu huwa wanakwama kwenye suala la kuacha fedha taslimu au hati ya mali,

Maana najua hapo unataka kusema wakati wa magufuli wenu hayo makosa yalikuwa hayana dhamana,

Makosa ambayo hayana dhamana ni murder case, money laundering, arm robbery, na uhaini,
kwa hiyo hata rugemalila na seth walikosa fedha za kujidhamini?
 
Watumishi hao ni Dkt. Zakayo Kyomo ambaye ni Kaimu Mkuu wa chuo cha VETA, Projestus Kabyemela (Mhasibu), Waziri Shaban Waziri (Mgavi) na Upendo Aidan Nindi (Afisa Ununuzi).

Watumishi hao wanashitakiwa kwa Matumizi Mabaya ya Mamlaka kinyume na kifungu cha 31 cha Sheria ya Uhujumu Uchumi sura ya 329 na Shitaka la pili ni kuisababishia Serikali hasara ya Tsh. Milioni 22.8 kinyume na kifungu 284 A (1) iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2022.

Washitakiwa walishindwa kupata wadhamini waliokidhi vigezo vilivyowekwa na kupelekwa Mahabusu, shauri hilo litatajwa tena Oktoba 13, 2022.

=======================

Watumishi wanne wa chuo cha Mamlaka ya Mafunzo ya Ufundi Stadi (Veta) mkoani hapa wamepandishwa kizimbani katika mahakama ya Hakimu mkazi mkoa wa Tabora wakikabiliwa na mashitaka mawili ya uhujumu uchumi.

Watumishi hao, Dk Zakayo Kyomo ambaye ni kaimu mkuu wa chuo hicho, Projestus Kabyemela (mhasibu), Waziri Shaban Waziri (mgavi) na Upendo Aidan Nindi (ofisa ununuzi), wamefikishwa mbele ya hakimu mkazi mwandamizi mkoa Tabora, Jovin Alphonce Kato leo Septemba 29.

Mashitaka yanayowakabili maofisa hao ni pamoja na shauri la uhujumu uchumi Namba 36 la mwaka 2022 yaliyosomwa na wakili wa Takukuru, Yunis Masalu.

Katika shauri hilo, watumishi hao wanashitakiwa kwa matumizi mabaya ya mamlaka kinyume na kifungu cha 31 cha Sheria ya Uhujumu Uchumi sura 329 na shitaka la pili ni kuisababishia mamlaka hasara ya Sh22.8 milioni kinyume na kifungu 284 A (1) iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2022.

Masalu amesema makosa hayo yamefanywa katika kipindi cha Februari 22, 2022 na Mei 25, 2022.

Wakili wa washitakiwa hao, Kelvin Kayaga amesema kwa kuwa dhamana iko wazi, atahakikisha wanadhaminiwa.

Mahakama imeweka masharti ya dhamana kwa washitakiwa wote kuwa na wadhamini wawili kila mmoja ambao watasaini nusu ya hasara huku mmoja wa wadhamini hao awe ni mtumishi wa Umma.

Hata hivyo, washitakiwa wameshindwa kupata wadhamini waliokidhi vigezo hivyo na kupelekwa rumande na shauri hilo litatajwa tena tarehe tena Oktoba 13 mwaka huu.

Kesi hiyo ni matokeo ya ziara ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa mkoani humo, ambapo alikagua ujenzi wa chuo hicho na kubaini ubadhirifu ukiwemo ujenzi wa chumba cha mlinzi kwa gharama ya Sh11 milioni na kumwagiza mkuu wa Takukuru kufanya uchunguzi na kuwachukulia hatua za kisheria wahusika.

MWANANCHI
KESI HI WANASHINDA. kwa ushahidi upi kutoka serikalini? Itakwenda mpaka Court of Appeal na huko wataachiwa.
 
Siasa siasa siasa, tunatangaziwa kufikishwa mahakani, mwisho wa kesi haujulikani, mfano Mkurugenzi Temeke, Arusha na wengineo.
 
Back
Top Bottom