Walioharibu Uchaguzi 2020, Watubu

Hamatan

JF-Expert Member
Nov 10, 2020
3,183
7,645
Sasa tunaongelea maridhiano, tunaongelea uponyaji wa Taifa, lakini unaliponya vipi Taifa bila kuyatambua majeraha? Kwa nini tusifuate mfano ule wa Afrika Kusini?

Waliotenda makosa, walitakiwa kujitokeza, walitakiwa kueleza uhusika wao katika maovu, kisha walikutanishwa na waathirika, waliomba msamaha, na mwisho walipewa hati ya kinga ya kutoshtakiwa kwa makosa waliyoyatubia.

Hapa kwetu, washiriki wote wa uharibifu wa uchaguzi wa 2020, wangejitokeza na kuweka wazi ushiriki wao.

Waliompoteza Ben Sanane, Azory, Kanguye, waliomshambulia Lisu, walioharibu uchaguzi wa ndani ya CCM kuwapata wagombea wa ubunge, waliowatengenezea watu kesi za uhujumu uchumi, waliopora pesa iliyoporwa toka kwa walioitwa wahujumu uchumi, n.k. Wote wangetakiwa kueleza kwa uwazi juu uhusika wao. Na wale ambao wasingejitokeza au kuficha ugusika wao, wangefikishwa mahakamani kama wahalifu.

Zoezi hili mwishowe lingewaacha huru, watuwaovu kama Sabaya, na watuhumiwa wengine kama Makonda, Mambosasa, Kalemani, Siro, Goodluck na wenzake, na wale majaji wa mchongo aliowatengeneza marehemu na kuwaingiza mahakamani kwa lengo maalum. Kwa sasa watu hawa, hakuna uhakika wa wao kutoshtakiwa siku moja kwa jinai wanazotuhumiwa.

Rais Samia, ufanye mchakato wa maridhiano kuwa halisia.
 
Zoezi hili mwishowe lingewaacha huru, watuwaovu kama Sabaya, na watuhumiwa wengine kama Makonda, Mambosasa, Kalemani, Siro, Goodluck na wenzake, na wale majaji wa mchongo aliowatengeneza marehemu na kuwaingiza mahakamani kwa lengo maalum. Kwa sasa watu hawa, hakuna uhakika wa wao kutoshtakiwa siku moja kwa jinai wanazotuhumiwa.
Ila kusema kweli kulikuwa na haja ya kuangalia ma- Judge wasio na ethics za kazi ili waweze kuondolewa ktk kazi hizi kwani wameharibu kabisa heshima ya majaji nchini
 
Sasa tunaongelea maridhiano, tunaongelea uponyaji wa Taifa, lakini unaliponya vipi Taifa bila kuyatambua majeraha? Kwa nini tusifuate mfano ule wa Afrika Kusini?

Waliotenda makosa, walitakiwa kujitokeza, walitakiwa kueleza uhusika wao katika maovu, kisha walikutanishwa na waathirika, waliomba msamaha, na mwisho walipewa hati ya kinga ya kutoshtakiwa kwa makosa waliyoyatubia.

Hapa kwetu, washiriki wote wa uharibifu wa uchaguzi wa 2020, wangejitokeza na kuweka wazi ushiriki wao.

Waliompoteza Ben Sanane, Azory, Kanguye, waliomshambulia Lisu, walioharibu uchaguzi wa ndani ya CCM kuwapata wagombea wa ubunge, waliowatengenezea watu kesi za uhujumu uchumi, waliopora pesa iliyoporwa toka kwa walioitwa wahujumu uchumi, n.k. Wote wangetakiwa kueleza kwa uwazi juu uhusika wao. Na wale ambao wasingejitokeza au kuficha ugusika wao, wangefikishwa mahakamani kama wahalifu.

Zoezi hili mwishowe lingewaacha huru, watuwaovu kama Sabaya, na watuhumiwa wengine kama Makonda, Mambosasa, Kalemani, Siro, Goodluck na wenzake, na wale majaji wa mchongo aliowatengeneza marehemu na kuwaingiza mahakamani kwa lengo maalum. Kwa sasa watu hawa, hakuna uhakika wa wao kutoshtakiwa siku moja kwa jinai wanazotuhumiwa.

Rais Samia, ufanye mchakato wa maridhiano kuwa halisia.
Wa 'Kutubu' kabisa ameshalala 'Mazima' tangia tarehe 17 Machi, 2021.
 
Sasa tunaongelea maridhiano, tunaongelea uponyaji wa Taifa, lakini unaliponya vipi Taifa bila kuyatambua majeraha? Kwa nini tusifuate mfano ule wa Afrika Kusini?

Waliotenda makosa, walitakiwa kujitokeza, walitakiwa kueleza uhusika wao katika maovu, kisha walikutanishwa na waathirika, waliomba msamaha, na mwisho walipewa hati ya kinga ya kutoshtakiwa kwa makosa waliyoyatubia.

Hapa kwetu, washiriki wote wa uharibifu wa uchaguzi wa 2020, wangejitokeza na kuweka wazi ushiriki wao.

Waliompoteza Ben Sanane, Azory, Kanguye, waliomshambulia Lisu, walioharibu uchaguzi wa ndani ya CCM kuwapata wagombea wa ubunge, waliowatengenezea watu kesi za uhujumu uchumi, waliopora pesa iliyoporwa toka kwa walioitwa wahujumu uchumi, n.k. Wote wangetakiwa kueleza kwa uwazi juu uhusika wao. Na wale ambao wasingejitokeza au kuficha ugusika wao, wangefikishwa mahakamani kama wahalifu.

Zoezi hili mwishowe lingewaacha huru, watuwaovu kama Sabaya, na watuhumiwa wengine kama Makonda, Mambosasa, Kalemani, Siro, Goodluck na wenzake, na wale majaji wa mchongo aliowatengeneza marehemu na kuwaingiza mahakamani kwa lengo maalum. Kwa sasa watu hawa, hakuna uhakika wa wao kutoshtakiwa siku moja kwa jinai wanazotuhumiwa.

Rais Samia, ufanye mchakato wa maridhiano kuwa halisia.
AMEN, AMEN, AMEN
Huu NDIO utakuwa ni mwanzo mpya na mwema wa kulijenga upya TAIFA letu. Tunahitaji kujitafakari na kutibu vidonda na majeraha mengi yaliyopo, Ili kuanza kuliponya na hatimae kulitibu Taifa hili. AMEN
 
Sasa tunaongelea maridhiano, tunaongelea uponyaji wa Taifa, lakini unaliponya vipi Taifa bila kuyatambua majeraha? Kwa nini tusifuate mfano ule wa Afrika Kusini?

Waliotenda makosa, walitakiwa kujitokeza, walitakiwa kueleza uhusika wao katika maovu, kisha walikutanishwa na waathirika, waliomba msamaha, na mwisho walipewa hati ya kinga ya kutoshtakiwa kwa makosa waliyoyatubia.

Hapa kwetu, washiriki wote wa uharibifu wa uchaguzi wa 2020, wangejitokeza na kuweka wazi ushiriki wao.

Waliompoteza Ben Sanane, Azory, Kanguye, waliomshambulia Lisu, walioharibu uchaguzi wa ndani ya CCM kuwapata wagombea wa ubunge, waliowatengenezea watu kesi za uhujumu uchumi, waliopora pesa iliyoporwa toka kwa walioitwa wahujumu uchumi, n.k. Wote wangetakiwa kueleza kwa uwazi juu uhusika wao. Na wale ambao wasingejitokeza au kuficha ugusika wao, wangefikishwa mahakamani kama wahalifu.

Zoezi hili mwishowe lingewaacha huru, watuwaovu kama Sabaya, na watuhumiwa wengine kama Makonda, Mambosasa, Kalemani, Siro, Goodluck na wenzake, na wale majaji wa mchongo aliowatengeneza marehemu na kuwaingiza mahakamani kwa lengo maalum. Kwa sasa watu hawa, hakuna uhakika wa wao kutoshtakiwa siku moja kwa jinai wanazotuhumiwa.

Rais Samia, ufanye mchakato wa maridhiano kuwa halisia.
NI maigizo tupu
 
Wa 'Kutubu' kabisa ameshalala 'Mazima' tangia tarehe 17 Machi, 2021.
Yeye hukumu yake ipo mbele ya mahakama kuu kuliko zote, Mahakama ya Mungu.

Lakini wapo alioshirikiana nao, tunao mitaani, hawa ndio tunawaongelea kwa sasa, Sabaya alikwishasema kuwa alikuwa akitumwa kutenda uovu ule. Ametusaidia tu kufahamu kuwa uovu ulikuwa unaratibiwa na Rais, na ulikuwa na baraka za makamuwa Rais wa sasa, Dr Mpango,lakinihiyo haimwondoi kwenye hatia.
 
Bwashee, hiyo toba inamhusisha na yule jamaa aliyewaambia wenzake kuwa sumu haionjwi kwa ulimi? Tuanzie hapo kwanza
 
Back
Top Bottom