Waliofurahi na kucheza Bunge la Katiba ndio wanaolia leo na maamuzi ya CAF

aleesha

JF-Expert Member
Oct 17, 2016
776
1,121
1. Suala la CAF na taarifa ya jana ya kufutwa uanachama unadhirisha mambo mawili. Zanzibar ni nchi inayokubalika na mataifa zaidi ya hamsini barani Afrika iliopiyaliopigaga kura ya ndio miezi minne iliopita kutujumuisha nasi katika taasisi hii.

2. Kufutwa kwetu si kwa sababu ya Afrika kutokutukubali na kuyaona yanayotendekea ila kuna wakoloni waoga wengine wanaokhofia nao kupoteza makoloni walioyakalia kimabavu. Fikiri Umoja kama huu lakini kwa upande wa Ulaya majuzi imeikubalia uanachama kijimamlaka cha Gibraltar ambacho ni kimantik na kwa sheria zote ni sehemu ya Umoja wa Himaya ya Malkia wa Uingereza ikiwa na mamlaka yote ya kujiongeza yenyewe isipokuwa "Sovereignty" lakini ni mwanachama kamili. Tumefutiwa uanachama katika mkutano wa Moroco chini ya mamlaka ya Mwenyekiti mbuki, na ndio waliopiga kura ya hapana kutupinga uanachama tangu awali. Wameshindwa kuishawishi Afrika wamekwenda na ujecha, zaidi hakuna ridhaa baina ya "tuwaache walete waislam" na tunaotaka mabadiliko.

3. Kama mtafiti tazama tafauti za kijamii kwa kuzingatia wakati tukikubaliwa uanachama habari hizi zilikuwa na mvuto kwa nani na kusheherekewa na nani. Lakini halkadhalika wakati wa kufutwa mvuto ulikuwa wapi wa habari na masikitiko yalianzia wapi. Nikitegemea kabisa kwa mamlaka husika katika taarifa ya jana nao wangejitokeza pande zote mbili na kutoa maelezo na hatua za kuchukua ukizingatia sababu tulizokubaliwa kujiunga na kufutwa zina mchanganyiko mkubwa hasa katika masuala ya kisheria. Pande zote za mamlaka kimnya, hivi maraika na genge lake waliridhia au yalikuja bila ya kutegemea? Na kibatari chetu kimejaa moshi, hakifurukuti, wakti wa neema hauji kwa wasio na ridhaa ya uongozi. Tumegusa, tumenusa na kuonja ladha ya utambulisho na furaha ya kujulikana, ari izidi hasa mpaka tufike lengo, tunaweza.

4. La mwisho ni kuwa tuboreshe kwanza mfumo wa michezo visiwani na kuhakikisha tumesonga mbele. Nakumbuka kipindi cha Small Simba, Malindi, Kiski, Miembeni, Jamhuri nk. Hatukuwa na habari ya CAF lakini tulikuwa na mvuto mzuri wa masuala ya michezo. Nahisi hili la CAF ni Mungu tu kataka kuwadhihirishia samaki kwamba huwezi ukawa huku na kule na dunia ikutazame tu.

5. Njia ni moja tu nayo ni mabadiliko ya mfumo wa muungano utaotupa fursa kila upande wa kukubaliana kwa ridhaa zetu ya kushirikiana tunayoyataka na kutuacha tukiwa na utambulisho wa kifursa hasa katika masuala ya kimataifa na taasisi za kimataifa. Inafurahisha waliokata viuno Bunge la katiba, ndio wanaolia leo kwa msimamo wa CAF. Bila ya ridhaa ya waliokuchagua kuwaongoza, utafikia tu ukuta maana Mungu atakusuta tu kuanzia ndani ya nafsi na kwa matukio ya namna hii kwa sababu unafik hauna mwisho mwema. Mabadiliko yanakuja na yakifika tutarejesha heshima ya visiwa hivi vinavyofanyiwa juhudi kubwa kuwa manispaa isiojitambua. Hata uchaguzi tatizo si sisi wazanzibari kama tunavyoaminishwa, tatizo nafikiri kwa sasa linatambulikana.
 
kati ya vitu vilivyonifurahisha kuliko vyote jana ni kusikia zenji wamepigwa chini. wakubali tu kuwa wao sio nchi hata mataifa mengine yanajua hilo.
 
kati ya vitu vilivyonifurahisha kuliko vyote jana ni kusikia zenji wamepigwa chini. wakubali tu kuwa wao sio nchi hata mataifa mengine yanajua hilo.
ZANZIBAR KUVULIWA UANACHAMA CAF NI BISHARA NJEMA
Maswali yamekuwa mengi sana bila ya majibu, suala kubwa kwa nini Zanzibar ilipewa uanachama CAF? ukianza kuzitazama sheria kwa nini nchi inapewa uanachama mchakato mzima mpaka hatua ya upigaji kura utaona kama miujiza.
Hili si jambo la bahati mbaya Mungu amelileta kwa makusudi yake. Vyovyote mtu atakavoliona kuwa kubwa au dogo, linaumuhimu au halina, kuwa zito au jepesi kwangu nimelitafsiri kuwa lina maana pana kwa mustakbali wa Zanzibar.
Kubadilika kwa mwanaadamu hakutokani na jambo kubwa sana mfano; afe mzazi wake au kutokee vita kwenye nchi yake laa si hayo tu kwanza lazima tujue kuwa kabadilika kwa binaadamu kunataka sababu ndogo tu ambayo Mungu ameshataka kumbadilisha mja wake.
Wakati mwengine huwa tunasema mtu fulani kabadilika kwa jambo la "kipuuzi" tu naam tunaliona kuwa ni la kipuuzi lakini Mungu ametaka hiyo ndio iwe sababu ya kumuongoa mja wake amtakae. Mimi si muumini wa Visasi, Kebehi, Kejeli na tambo za KIBURI naipigania HAKI, naitetea haki, lakini kwa njia zile zile za haki.
Kwa imani kabisa naamini kama madogo (ukiyaacha makubwa yalio/yanayo isibu Zanzibar) yaliweza kuwaweka watu karibu wakaweka udugu wa kitaifa kwanza na tukafanikiwa kuvuka kizingiti kikubwa basi sina wasi wasi kwa moyo wenye imani, kupitia njia za amani na hili linalooneka kuwa ni dogo ukilinganisha na mengi yenye kumbukumbu mbaya yanayoendelea kusemwa huenda hapa ndipo ilipo heri ya mabadiliko.
Mwisho tuweke hakiba kwa kurejea tena hizi sio zama za visasi na nongwa tukaishia kubezana na kuchukiana. Mungu anakadari zake anaweza kuyaleta mabadiliko kwa kumtumia kuku hayawan aso na akili
 
Yanini kupindapinda?Si mseme kile kilicho mioyoni mwa wazanzibari hawataki muungano wa kuwageuza mkoa badala ya nchi.Hilo ndio tatizo
 
Aisee mtoa mada umetukumbusha jambo muhimu mno nahisi mada yako hii ndio mada bora kwa mwezi huu.

Stay blessed
 
Mleta mada analialia tu hasira zake analeta kwenye siasa.
Sioni tatizo ni suala la kujipanga na kwenda na hoja mpya na nzito zaidi,ikishindikana basi ZFA ivunjwe na katiba ya TFF ihusishe makamu na naibu kutoka upande mmoja na zanzibar iwe na sekretarieti itayoendesha soka huko
 
Kwa akili zenu mumeomba uanachama mashirka na taasisi za kimataifa kama nani? Ni sawa kabisa walichofanya CAF. Halafu kidogo munashangaza, linapokuja suala la haki zenu mnakuwa na vidomodomo sana ila mnapoona khatari mbele yenu haoooo; submission to Dodoma. Amueni moja mueleweke.
 
Mleta mada analialia tu hasira zake analeta kwenye siasa.
Sioni tatizo ni suala la kujipanga na kwenda na hoja mpya na nzito zaidi,ikishindikana basi ZFA ivunjwe na katiba ya TFF ihusishe makamu na naibu kutoka upande mmoja na zanzibar iwe na sekretarieti itayoendesha soka huko
Michezo sio suala la muungano; ndivyo zisemavyo "Articles of the Union".
 
Dah,mtoa mada nasikitika kukuambia kuwa andiko lako halieleweki,nimejaribu kusoma zaidi ya mara tatu narudia rudio lakini sioni urari na vina katika andiko lako,yani ni kama umeshtuliwa kutoka usingizini au unamhemko kiasi kwamba unaandika kisichoeleweka,point yako inaweza kuwa ni nzuri lakini uwasilishaji wako hapa jukwaani unamang'amung'amu .

Kama hutojali rudia tena kuandika hili bandiko lako ili lieleweke vema .
 
Michezo sio suala la muungano; ndivyo zisemavyo "Articles of the Union".
Kwani waliowatimua zanzibar ni serikali ya muungano au CAF?
Zanzibar imenyimwa uanachama kwa sababu walimuunga mkono ISSA HAYATOU,hilo lipo wazi aliengia amewatolea mbavuni.
Kinachotakiwa wajipange upya wapeleke hoja badala ya kulia lia na kusingizia Muungano.Ingawa zanzibar sio nchi yapo mazingira yanayoweza kufanya wakafikiriwa
 
Strong actions should be taken against all those who helped Zanzibar to violate the constitution of the United Republic

Cc:
John Magufuli, The President of the United Republic of Tanzania & Chairman of the ruling party

Prof. Palamagamba Kabudi
, Minister of Constitution & Legal Affairs

George Masaju
, Attorney General

Harrison Mwakyembe
, The Recently Minister of Information, Sports and Culture
 
Fikiri Umoja kama huu lakini kwa upande wa Ulaya majuzi imeikubalia uanachama kijimamlaka cha Gibraltar ambacho ni kimantik na kwa sheria zote ni sehemu ya Umoja wa Himaya ya Malkia wa Uingereza ikiwa na mamlaka yote ya kujiongeza yenyewe isipokuwa "Sovereignty" lakini ni mwanachama kamili

Acha kulinganisha Gibraltar na Zanzibar! Gibraltar ni nchi inayotawaliwa lakini Zanzibar ni sehemu ya Tanzania! Gibraltar inaweza kudai Jamuhuri, Zanzibar haiwezi kudai jamuhuri kwa kuwa itakuwa uhaini na uasi!
 
Sababu za Rais wa CAF kuifuta uanachama wa CAF Zanzibar kwa misingi ya kutokuwa mwanachama wa UN na AU naamini amekurupuka angeangalia Mashirikisho makubwa kama UEFA na FIFA wanachama wake wanavyopatikana mfano UNITED KINGDOM (England, Wales,Scotland na Northern Ireland ) ni mwanachama wa UN na EU (ambayo imejitoa karibuni).Hapa utaona ENGLAND, WALES, SCOTLAND & NORTHERN IRELAND si wanachama wa UN na EU lakini ni wanachama wa UEFA na FIFA. Kwahivyo hapa hakufanya maamuzi sahihi kwasabu ENGLAND sawa na ZANZIBAR wote wana bendera, wimbo wa Taifa, Bunge, Mahakama, Serikali pamoja na Wizara ya Michezo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom