Chuo kipo Shirati-rorya Mara,ni mji mdogo na umechangamka kwa sana kibiashara...nauli ni 5000 kutoka Tarime na 1000 kwenda mpakani mwa kenya(mihuru bay) ni pembezoni mwa ziwa victoria.
Wanaishi wajaluo kwa sana...Gharama za maisha ni za kawaida...chakula 1000--1500/sahani..
Chuo kina hospital inaitwa RAO, mkuu wa chuo anaitwa Dr PZ Makoyo(MD,PhD)
Jirani pia kuna hospitali ya wilaya inaitwa Shirati KMT Hosp. Na inatumiwa sana na wanachuo wa RAO pia kuna chuo cha uuguzi hapohapo..
Hostel zipo ila ni option kuishi hostel/kitaa
Shule iko vizuri pale ijapokuwa madakitari wengi wamerudi shule kufanya masters.
Ada jiandae maana sio pungufu ya M3 (hakuna huduma za chakula)
Hutajuta kuwa pale ila kuwa makini kuna maambukizi UKIMWI sana.
Karibu kwa maswali..