David Goliath
JF-Expert Member
- May 16, 2018
- 929
- 1,798
Aisee jana nimeponea chupuchupu kuzirusha na Walinzi wa SUMA JKT, ipo hivi mimi ni dereva Bajaj sasa kuna abiria wangu huwa nampeleka ofisini na kumfata, jana akaniambia kapata dharura haendi kazini ila akanipa laptop nipeleke ofisini kwao na namba ya muhusika ambaye anatakiwa kupelekewa hiyo laptop akanipa, nilipofika pale nikampigia simu akaniambia ametoka kidogo hiyo laptop niwaachie Walinzi hapo getini nilivyo maliza kuongea na simu kuna mlinzi wa kike akaniuliza kasemaje?
Nikamjibu kasema niwaachie nyie Walinzi anakuja kuichukulia hapa aisee yule mdada akaanza wewe usirudie tena kutuita Walinzi, nikauliza nyie ni wakina nani?
Akawa ananiambia uwe na heshima usitake kubishana na mimi tukazozana pale wale wengine nao wakaingilia nikawaambia nyie ni Walinzi kama hamfanyi kazi ya ulinzi ondokeni hapa mmoja akamwambia wenzake eti huyu ni wakumpa materials za kijeshi Ili atuelewe nikawaambia hilo haliwezekani mkitaka kuhatarisha ajira yenu mniguse kisa nimewaita Walinzi nikawasha zangu Bajaj nikaondoka.
Nilishangaa sana hawa jamaa sijui ndivyo wanavyoambiwa huko na wakubwa zao au ni uelewa mdogo.
Nikamjibu kasema niwaachie nyie Walinzi anakuja kuichukulia hapa aisee yule mdada akaanza wewe usirudie tena kutuita Walinzi, nikauliza nyie ni wakina nani?
Akawa ananiambia uwe na heshima usitake kubishana na mimi tukazozana pale wale wengine nao wakaingilia nikawaambia nyie ni Walinzi kama hamfanyi kazi ya ulinzi ondokeni hapa mmoja akamwambia wenzake eti huyu ni wakumpa materials za kijeshi Ili atuelewe nikawaambia hilo haliwezekani mkitaka kuhatarisha ajira yenu mniguse kisa nimewaita Walinzi nikawasha zangu Bajaj nikaondoka.
Nilishangaa sana hawa jamaa sijui ndivyo wanavyoambiwa huko na wakubwa zao au ni uelewa mdogo.