Hilo ulilosema ni kweli kaka ila wanaotuponza ni walimu wa shule za msingi na wengi kwa idadi hurubunika na hili husababishwa na wengi wa walimu wa msingi elimu ni ndogo, hawajui haki zao wanatshwa kila rahisi, wengine wanatumia vyeti vya marehemu, na wengine ni wake wa watumishi wa serikali na watawala huko so mgomo ni kama uasi kwa wenza wao. Mf mzuri ni deni la walimu lilikuwa bil 32 serikali ikalipa bil 18 tena asilimia kubwa kwa walimu wa msingi sekondari tukatoswa.Tatizo lingine ni mgawanyiko na propaganda zinazoendeshwa na viongozi wa CWT kati ya walimu wa sekondari na msingi kwa maslahi yao hutumia wingi wa walimu wa msingi kushinda chaguzi (Makatibu na wenyeviti wengi wa CWT ni walimu wa msingi ) na wanajali maslahi yao sio ya walimu.Mwaka huu tutafanikiwa kwanza kumekuwa na ongezeko la walimu wa msingi vijana wenye qualification kutoka vyo vya serikali na hivi vya private ambavyo vimeibuka kila mahali ka uyoga na huko nidhamu za ''kinyererenyerere'' hamna na kwa sababu ni vijana wenzetu tunamingle vizuri tu najua wale wazee wazee wa kusema ''enzi zetu sisi'' watakataa kugoma hao ndo tutawachapa bakora experience zetu za migomo chuoni tutazileta huku ktk field