Walimu wanawadhalilisha watoto

Walimu wanawadhalilisha watoto

Walimu au watu kama hao wanatakiwa wachukuliwe hatua kwa kukiuka sheria ya mtandao ikiwa ni pamoja na kukiuka haki za watoto kwa sababu huo ni udharirishaji mkubwa kwa watoto ambao bado wana mengi ya kujifunza.
Udhalilishaji upo kwa wanasiasa tu, wengine sio watu.
 
Write your reply...HI NI TABIA YA MTU KUTOJALI AU KUHESHIMU KAZI YAKE NA PIA NA MADHARAU KWA WATOTO WA WENZIE.TCRA MPO NA WIZARA HUSIKA IPO WHY?MNAANGALIA TU HUO UPUUZI?
 
Hivi walimu wanavyodhalilishwa na wakuu wa wilaya na wa mikoa wewe huoni?? Acha upuuzi wewee
Kwa nini msiwadhalilishe wake au watoto wenu ndio mkarusha;kuna siku mtayakanyaga mawaya tu mumrushe mtoto wa mwehu mwenzenu awafurahishe
 
Habari wana jukwaa.

Hivi karibuni kumekuwa na mtindo wa walimu hasa wa shule za msingi kuwarekodi watoto na kisha kuzisambaza video hizo,

Binafsi nimefanikiwa kuona video 3 za walimu hao na zote zinaonesha si tu uelewa mdogo wa mwanafunzi bali pia ujinga wa aliyepewa dhamana ya kuuondoa ujinga wa mwingine.

Mwalimu anamuuliza mtoto kwanini hakuja shule? Mtoto anajabu hakuja kwa sababu alifariki. Kiswahili anachotumia mwalimu huyo na majibu ya mwanafunzi inaonesha kuna tatizo kubwa katika jamii.

Cha kujiuliza ni nini kinapelekea mtu kumrekodi mtu aliyepewa dhamana ya kumvusha toka alipo, halafu anamsambaza mitandaoni. Au ni stress za udogo wa mishahara?
Tunachagua watu walioshindwa kabisa katika vipimo vyetu vya mitihani kuwa walimu.

Unategemea nini?
 
Habari wana jukwaa.

Hivi karibuni kumekuwa na mtindo wa walimu hasa wa shule za msingi kuwarekodi watoto na kisha kuzisambaza video hizo,

Binafsi nimefanikiwa kuona video 3 za walimu hao na zote zinaonesha si tu uelewa mdogo wa mwanafunzi bali pia ujinga wa aliyepewa dhamana ya kuuondoa ujinga wa mwingine.

Mwalimu anamuuliza mtoto kwanini hakuja shule? Mtoto anajabu hakuja kwa sababu alifariki. Kiswahili anachotumia mwalimu huyo na majibu ya mwanafunzi inaonesha kuna tatizo kubwa katika jamii.

Cha kujiuliza ni nini kinapelekea mtu kumrekodi mtu aliyepewa dhamana ya kumvusha toka alipo, halafu anamsambaza mitandaoni. Au ni stress za udogo wa mishahara?
Una kadi ya kijani
 
Nimekuwa nikijiuliza sana, hivi unapomdhalilisha mtoto wa mwenzio unaona raha gani? Mwalimu anayejihusisha na udhalilishaji wa watoto mitandaoni atakuwa hajui wajibu wake wa kufundisha na kulea.
Huyo ni mwalimu wa MSHAHARA, sio wa WITO.
Kama anayefanya jambo hili sio mwalimu, basi ni mshamba wa matumizi ya mitandao ya kijamii.
Haki ya mtoto inakiukwa hapa. Serikali/TCRA iliangalie suala hili.
 
Nadhani waajiri wao wanapaswa kuwachukulia hatua...for sure huu ni uzalilishaji.
 
Inawezekana sio nia yako, ila kuendelea kuisambaza ni kuendelea kumdhalilisha huyo mtoto.
mkuu siku na nia hiyo....nimeshaifuta link.

Nawe

Futa tu hii comment uliyoniquote. ..automatic na hiyo link ya video itafutika...
kwa sababu bado ipo kwako.
 
Mwalimu kusambaza video za namna hiyo ni moja ya madhara ya kuchukua wanafunzi waliopata madaraja ya chini katika matokeo ya kidato cha 5 na 6 ndo wakasomee kozi ya ualimu. Mtu mwenye uelewe mzuri hawezi kufanya kitendo cha namna hiyo.
Uko sahihi brother, salute.
 
Positively mwenyew hcho kitu nimekiona na nikawaza kama mleta Uzi......ule ni uzaririshaji kabisa afu ni ukosefu wa weledi wa kazi
Kuandika tu, baadhi ya maneno hujui, 'uzaririshaji' sijui ndio nini!? Ndo ije kuwa huo weredi wako.
 
Kazi ya Mwalimu, licha ya kwamba anapaswa kumpa mtoto/mwanafunzi elimu ya darasani, haimaanishi asimpe elimu dunia (ya kufahamu mazingira yake). Sidhani kama endapo mtoto angejisaidia kwenye nguo zake angemchukua video na kuirusha mitandaoni.

Walimu (mnaofanya hivyo) badilikeni huo si uungwana na ni kinyume cha maadili ya kazi zenu
 
Back
Top Bottom