Walimu wanawadhalilisha watoto

Walimu wanawadhalilisha watoto

Pyepyepye

JF-Expert Member
Joined
Jan 6, 2017
Posts
1,940
Reaction score
3,842
Habari wana jukwaa.

Hivi karibuni kumekuwa na mtindo wa walimu hasa wa shule za msingi kuwarekodi watoto na kisha kuzisambaza video hizo,

Binafsi nimefanikiwa kuona video 3 za walimu hao na zote zinaonesha si tu uelewa mdogo wa mwanafunzi bali pia ujinga wa aliyepewa dhamana ya kuuondoa ujinga wa mwingine.

Mwalimu anamuuliza mtoto kwanini hakuja shule? Mtoto anajabu hakuja kwa sababu alifariki. Kiswahili anachotumia mwalimu huyo na majibu ya mwanafunzi inaonesha kuna tatizo kubwa katika jamii.

Cha kujiuliza ni nini kinapelekea mtu kumrekodi mtu aliyepewa dhamana ya kumvusha toka alipo, halafu anamsambaza mitandaoni. Au ni stress za udogo wa mishahara?
 
Walimu au watu kama hao wanatakiwa wachukuliwe hatua kwa kukiuka sheria ya mtandao ikiwa ni pamoja na kukiuka haki za watoto kwa sababu huo ni udhalilishaji mkubwa kwa watoto ambao bado wana mengi ya kujifunza.
 
Last edited:
Its not right kabisa.

Kwanza ethics za kutumia simu shuleni zinaruhusu kweli?

Pia tuje kwenje exposure ya mtoto hivyo, sio sahihi.
 
Habari wana jukwaa.

Hivi karibuni kumekuwa na mtindo wa walimu hasa wa shule za msingi kuwarekodi watoto na kisha kuzisambaza video hizo,

Binafsi nimefanikiwa kuona video 3 za walimu hao na zote zinaonesha si tu uelewa mdogo wa mwanafunzi bali pia ujinga wa aliyepewa dhamana ya kuuondoa ujinga wa mwingine.

Mwalimu anamuuliza mtoto kwanini hakuja shule? Mtoto anajabu hakuja kwa sababu alifariki. Kiswahili anachotumia mwalimu huyo na majibu ya mwanafunzi inaonesha kuna tatizo kubwa katika jamii.

Cha kujiuliza ni nini kinapelekea mtu kumrekodi mtu aliyepewa dhamana ya kumvusha toka alipo, halafu anamsambaza mitandaoni. Au ni stress za udogo wa mishahara?
Mshahara Mdogo!Unatia uvivu kufundisha na mbaya zaidi unasikia wapuuzi fulani wako bungeni wanakula hela ya kutosha bila kutumia nguvu
 
Hii ni kutuonyesha wazi kuwa kazi tuliyowapa hawaifanyi, na mshahara wanakula na mikopo wanapata, na wataendelea kuuza ubuyu na asikilimu shuleni, hatuna cha kuwafanya, zaidi ya kushuhudia watoto wetu wakielea kwenye ujinga. Huyo mtoto hajui tofauti ya kufariki/kufa na kufiwa.... ilikuwa ni kazi ya mwalimu kumwelimisha. Huu ni mgomo wazi wa waalimu, sio lazima watangaze kugoma.
 
Mwalimu kusambaza video za namna hiyo ni moja ya madhara ya kuchukua wanafunzi waliopata madaraja ya chini katika matokeo ya kidato cha 5 na 6 ndo wakasomee kozi ya ualimu. Mtu mwenye uelewe mzuri hawezi kufanya kitendo cha namna hiyo.
 
Mwalimu kusambaza video za namna hiyo ni moja ya madhara ya kuchukua wanafunzi waliopata madaraja ya chini katika matokeo ya kidato cha 5 na 6 ndo wakasomee kozi ya ualimu. Mtu mwenye uelewe mzuri hawezi kufanya kitendo cha namna hiyo.
si kweli! analysis yako ipo chini sana ya kiwango endelea kufanya utafiti wako upya mkuu
 
Back
Top Bottom