Walimu Shule ya Msingi Mzinga Morogoro wanatesa wanafunzi

sinajinasasa

JF-Expert Member
Dec 10, 2013
2,989
4,129
Kilio hiki naomba kimfikie Waziri husika, hapa Morogoro kuna Shule ya Msingi ya Mzinga inatesa Wanafunzi wake, kwa vile Walimu wana hofu ya wanafunzi wa shule ya msingi wa darasa la saba na la nne kufeli mitihani, walimu hawa wamekuwa nyuki, wanawachapa sana wanafunzi viboko, yaani watoto wanalalamika sana kwa wazazi nyumbani.

Mtoto mdogo anaamka giza kabisa asubuhi anawahi shule, walimu wanawapa mitihani Watoto saa 12 asubuhi na asipofanya ni fimbo tu, kuna watoto wanatoka maeneo ya umbali hadi wa km 5 kwa miguu kuja shule, na wao wakichelewa ni fimbo tu hawajali kwamba mtoto anatoka mbali.

Wakati fulani hadi tunahisi labda watoto waache tu shule basi maana si kwa mateso hayo ya watoto.

Walimu badala ya kufundisha, wao wanawapigisha strori za udaku kwa watoto, yaani mwalimu anatumia dakika 40 za kipindi kuwalaani wazazi wa watoto eti hawana ushirikiano na walimu.

Sasa ninyi walimu nawauliza ushirikiano gani mnataka? Je, tuwape rushwa ili mfundishe watoto, matendo yote hayo tunaletewa na watoto wenyewe kama mashahidi. Walimu hawa wengi wanahangaika kutafuta wateja wa QNET badala ya kufundisha.
Naomba niwataje kwa majina yao;

Walimu wengine wao wana stress za kutapeliwa na qnet. Sasa hasira zao zinawaangukia watoto. Waziri wa elimu mama yangu okoa jahazi. Naomba mnisaidie kumtagi mhusika achukue hatua.

Mimi Mzazi.
 
Tuanzie hapa una uthibitisho wa walimu kupiga udaku dk 40 zote za kipindi?

Swala dogo Kama hili unataka waziri atatue? Umeshindwa kumfwata mkuu wa shule kumueleza haya?

Inaonekana wew n mtu wa kulialia Sana ndio sababu Hata mwanao anakuja kulia mbele yako kwa uzembe wako badala ya kuchukua hatua unakuja jf kulia.

Acha uoga Kama unauhakika nenda kwa mkuu wa shule kamueleze maafisa elimu pia wapo.
 
Baada ya kuminyana kwenye biashara yenu ya q net naona umeamua kuja kupiga kelele huku
 
Kama wewe ndiye mzazi basi huwatendei haki hao watoto. Waache wafundishwe, wewe wakati wako ulishapita, acha watoto watengeneze maisha yao ya baadaye. Hata sisi tuliofanikiwa tuliamka saa kumi na moja nakutembea zaidi ya km 30 kwenda shule, kumbuka hapo unatakiwa ubebe kuni, nyasi, maji etc.
 
Mwl. Mtete bado yupo hapo mzinga ?

Madame Stella.
Wewe unakaa unafanya kazi kiwandani au ?
pole. sana
 
Unaogopa mtoto akichapwa? Acha wakomae, wamelegea mno.

Mwaka fulani binti yangu akiwa fomu three hapo kiluvya alichapwa viboko kidogo afe.

Niliziba masikio kama sisikii anachoniambia.

Now she's good so good,

Usimnyime mtoto viboko hata Bible imeandika.
 
Kilio hiki naomba kimfikie Waziri husika, hapa Morogoro kuna shule ya msingi ya Mzinga inatesa wanafunzi wake, kwa vile walimu wana hofu ya wanafunzi wa shule ya msingi wa darasa la saba na la nne kufeli mitihani, walimu hawa wamekuwa nyuki, wanawachapa sana wanafunzi viboko, yaani watoto wanalalamika sana kwa wazazi nyumbani.

Mtoto mdogo anaamka giza kabisa asubuhi anawahi shule, walimu wanawapa mitihani watoto saa 12 asubuhi na asipofanya ni fimbo tu, kuna watoto wanatoka maeneo ya umbali hadi wa km 5 kwa miguu kuja shule, na wao wakichelewa ni fimbo tu hawajali kwamba mtoto anatoka mbali...
Qnet kama kweli mmewatapeli hawa waalimu milioni tano tano kila mmoja basi mlaaniwe!

Kwa kipato cha mwalimu 5m ni kubwa sana.
 
Walimu wana nia nzur tu kwa vile muda umekwenda wanataka wamalize silabasi mapema ili watoto wasifeli

Kuhusu kutumia dk 40 kupiga umbeya siwez liongelea kama wanafsnya hvyo waache

TUWAPE USHIRIKIANO WALIMU WAZAZ WENZANGU TUKOSOE KWA NAMNA INAYOFAA
 
Kutokana na maelezo yako nimegundua mtoto wako anasifa hizi:
_ Mchelewaji
_ Anafeli darasani
_ Muongo ( story za darasani wewe mzazi umezipataje?)
_ Hana nidhamu ( hupigwa viboko kila siku)

Acha walimu wafanye kazi yao.
 
Kama wewe ndiye mzazi basi huwatendei haki hao watoto. Waache wafundishwe, wewe wakati wako ulishapita, acha watoto watengeneze maisha yao ya baadaye. Hata sisi tuliofanikiwa tuliamka saa kumi na moja nakutembea zaidi ya km 30 kwenda shule, kumbuka hapo unatakiwa ubebe kuni, nyasi, maji etc.

Umenikumbusha kubeba nyasi dah🤣🤣🤣! A.k.a lipelele!
 
Back
Top Bottom