Walimu kufutwa tuition wamkumbuka Kikwete

Walimu kufutwa tuition wamkumbuka Kikwete

bulabo

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2015
Posts
628
Reaction score
783
Walimu hasa hawa wa mijini sasa wanasikitika baada ya tuition kufutwa kwa sababu zifuatazo.

-Zilikuwa zinawapa ahueni ya maisha.

- Mikopo kukatwa iliwapa unafuu wa maisha.

- Maji ya chooni, walinzi, umeme, rim, mitihani ya asubuhi na weekend hasa jumamosi.

- Walimu waliipenda kazi
- Walimu waliweza kuishi na hiyo mishahara midogo
- Na mengine mengi ongezeeni.

WALIMU wakuu waliendesha shule hata kama serikali itachelewesha support.

Sasa wataisoma namba, wazazi watafurahi lakini wajue watoto nao watakosa mitihani ya wiki ili kuwafanya kuwa active. hiyo elfu 5000 ambayo wazazi walikuwa wakichanga iliwasaidia wanafunzi kupata vitu vingi kama uji kama usafi kama chalk kama umeme kama ukinzi kama karatasi za mitihani.

Niwaombe tu walimu wakubaliane na mabadiliko ya JPM na serikali itafidiaa hizo hela za umeme maji n.k kama zitacheleweshwa ndo kuisoma namba.

Mwisho mbadiliko huja na faida na hasara. Elimu burendiyo hiyo hata lowasa angefanya kama magu nvyofanya. kwa hiyo tumshukuru yale jk aliyafanya na tujifunge mkanda ambayo magu anakuja nayo baada ya miaka miwili tutaona matunda yake.

TANZANIA YETU SOTE
 
Hivi tamko limetolewa maana binti yangu kaniambia wametangaziwa shuleni kwamba hakuna kutoa tena pesa za michango elimu ni bure
 
tangazoo gazetini limetoka. ni maumivu kwa walimu aiaeee
 
Arudishe mfumo wa zamani basi. Alafu mfumo wa GPA kwa form IV na VI aufute tafdhari. BRN za kikwete kwenye elimu zimefeli kabisa. Apangue madudu ya kikwete yote. Mdogo mdogo tutafika tu!!!
 
Gazeti gani jamani,manake Leo mtotoangu amekuja na kusema walimu wamewambia waende na elfu tano(5)ya chakula siku wanafanya mtihani WA std 4
 
Hayo ndo mabadiliko, Magufuli ni mrithi halisi wa Mwl Nyerere!!
 
hahahaha! kucheka ruksa

Shida iko wapi kama serikali itaajiri walinzi kwa utaratibu uliokuwapo hapo awali, italipia umeme na maji na mengineyo. Kumbuka shule zinahitaji secretaries, watu wa masijala, makarani wa fedha, maboharia, walinzi, wapishi, maktaba na wakutubi, maabara na lab technicians. Hawa wote hajaajiriwa tangu miaka ya 90 kwa shule kongwe wapo wale ambao hawajastaafu au kuomba redundancy. Kwa shule za kata hakuna hata mmoja. Serikali iwaajiri na kupunguza wasio na kazi. Ndio mabadiliko. BRN haina lolote iondolewe walimu wafundishe kwa mujibu wa taratibu za kazi bila uzembe. Grading system iliyoanza 2014 ni nzuri isibadilishwe
 
Arudishe mfumo wa zamani basi. Alafu mfumo wa GPA kwa form IV na VI aufute tafdhari. BRN za kikwete kwenye elimu zimefeli kabisa. Apangue madudu ya kikwete yote. Mdogo mdogo tutafika tu!!!
Kwan wakitumia GPA au division tofauti yake ni nini.....fuatilia kwanza ndo ucomment
 
Watazoea taratibu. Ninachoofikiria. Serikali fungu inalopeleka kwenye kila shule lisicheleweshwe tu. kama tunavyojua oc zinamiaka baadhi ya maeneo hazijaja....kwa hiyo hali inaweza kuwa mbaya kwenye mambo kadhaa. Serikali wajipange tu
 
kati ya nipashe au mwananchi waliandika. sikumbuki vizuri
 
Watazoea taratibu. Ninachoofikiria. Serikali fungu inalopeleka kwenye kila shule lisicheleweshwe tu. kama tunavyojua oc zinamiaka baadhi ya maeneo hazijaja....kwa hiyo hali inaweza kuwa mbaya kwenye mambo kadhaa. Serikali wajipange tu

Kama sijasahau, JK ndo alipiga marufuku hizi habari za tuition kwa wanafunzi mwaka 2006. Ila naona walimu waliendelea na kutoa tuition tuu kama kawaida.
Kama ndivyo hivyo basi kunatatizo haswa katika usimamiaji wa maelekezo ya watendaji wakuu. Katika nchi yetu sidhani kama kunasheria ya Mwalimu kufundisha tuition achilia mbali remedial classes.
Tumepiga marufuku tena tuition, hapo sina shaka na ni hatua nzuri. Bado hii michango mingine kama speed test, chakula, mlinzi na nk, Je serikali inakuja kufidia hivyo na wanafunzi wataendelea kupewa chakula wakiwa shuleni kwa shule zote nchini!?

Mungu ibariki Tanzania, Mungu Mbariki Rais wetu aweze kufanya mambo kwa weledi na hekima zaidi kwa manufaa ya Watanzania wote
 
Asante!!Nashidwa kuelewa hii system ya tuition katika nchi hii.
 
Kama sijasahau, JK ndo alipiga marufuku hizi habari za tuition kwa wanafunzi mwaka 2006. Ila naona walimu waliendelea na kutoa tuition tuu kama kawaida.
Kama ndivyo hivyo basi kunatatizo haswa katika usimamiaji wa maelekezo ya watendaji wakuu. Katika nchi yetu sidhani kama kunasheria ya Mwalimu kufundisha tuition achilia mbali remedial classes.
Tumepiga marufuku tena tuition, hapo sina shaka na ni hatua nzuri. Bado hii michango mingine kama speed test, chakula, mlinzi na nk, Je serikali inakuja kufidia hivyo na wanafunzi wataendelea kupewa chakula wakiwa shuleni kwa shule zote nchini!?

Mungu ibariki Tanzania, Mungu Mbariki Rais wetu aweze kufanya mambo kwa weledi na hekima zaidi kwa manufaa ya Watanzania wote


kwani tuition ina matatizo gani?
 
ah kwahil sidhan kama rais wetu atafanikiwa kwa asilimia mia maana kwa shule hiz za kata tushen zinasaida watu kwa kiwango kikubwa katika swal la ufaulu
 
Hakuna lolote! kama tution ilikuwa inasaidia mbona kila cku elimu inazid kushuka? tution haisaidii chochote, zaman watu hatujasoma iyo tution na elimu ilikuwa juu kuliko hv sasa
 
Hakuna lolote! kama tution ilikuwa inasaidia mbona kila cku elimu inazid kushuka? tution haisaidii chochote, zaman watu hatujasoma iyo tution na elimu ilikuwa juu kuliko hv sasa

Jaribu kutofautisha mkuu zama ulizosoma ww uenda n zama baba wa taifa tution bado inaumuhim sana
 
Nınachojua tuition kuzikomesha itakuwa ngumu kwa wazazi wenyewe ndiyo wanaziratibu kwa hapa Dar.Ukidhibiti tuition za shule ambazo kimsingi nı cheap,watoto watatafuta za mtaani ambazo nı ghali na sio salama!
 
Back
Top Bottom