Walimu Dodoma Wagoma

Walimu Dodoma Wagoma

libidozy

Member
Joined
Jul 16, 2009
Posts
56
Reaction score
3
Kule Dodoma leo walimu wa shule za msingi wamegoma na hivi sasa wapo viwanja vya Nyerere Square wakitoa malalamiko yao kwa afisa elimu mkoa juu ya kauli ya kifedhuli ya Mwantumu,yaani shule leo hakuna habari ndio hiyo!Kabla ya kufika hapo Nyerere Square,walimu pamoja na wanafunzi wao walifanya maandamano makubwa kuanzia mashuleni kwao hadi viwanjani hapo.Kumbuka kuwa viwanja vya Nyerere Square vipo karibu kabisa na makao makuu ya ccm ambapo hapo juzi walimaliza vikao vyao vya kuwashambulia na kuwabana watanzania.
 
Sasa Naibu Waziri Mahiza aende Dodoma akatoe kauli zile alizotoa kule Songea kukabiliana na mgomo basi!!!Aone jinsi atakavyoiacha CCM nnjia panda pale Mzakwe.
 
Naomba nijuzwe Mwantumu ametamka nini on this??
 
jamani huyu Mahiza ana nin tuhoji elimu yake maana hata wanafunzi muhimbili walishawahi kumtunishia misuli kwa ajili ya kaulizake.
mh kazii kwelikweli tutafika.
 
Nilimsikia Naibu Waziri wa Elimu Mh Mwantumu Mahiza akiongea na wanafunzi wa ualimu kule Songea (source TBC Taifa jana jioni).
Aliulizwa kuhusu mishahara midogo wanayolipwa walimu. Alijibu kuwa wale wanafunzi wasioridhika ni mishahara ya ualimu watafute kozi nyingine ili wapate hizo kazi zinazolipa zaidi. Na pia hata wale walimu wasioridhika na mishahara pia watafute kazi nyingine na sio kufanya migomo, kwani hata wao (mawaziri nafikiri) wakigoma itakuwaje?

Nilisikitika mno na kauli ile na nilijiulizi hivi
Serikali na wananchi tunalalamika sana kuhusu uhaba wa waalimu na pia mishahara midogo wanayolipwa hawa wachache ukiacha na haki nyingi wanazonyimwa. Je huyu Naibu Waziri anapata wapi kiburi cha kuwaambia walimu watafute kazi nyingine zitakazo walipa?
Alisema walimu wananzia kulipwa kama laki mbili hivi ambazo hazijakatwa kodi. Je huyu Naibu Waziri ameshafanya kautafiti kuona kuwa hiyo inawatosha kuwafanya wasilalamike?
Huyu ni Naibu Waziri wa ELIMU ambaye tunamtegemea asimamie vizuri Elimu yetu wa Tanzania iliyojaa matatizo. Badala ya kuwapa moyo walimu wanaoumia kwa kulitumikia Taifa kwa kujitolea, angalau kwa kuwaahidi kushughulikia matatizo ya Elimu, sasa anaongea kama mtu wa kijiweni.
Sijui CV ya huyu Naibu lakini nafikiri tunamatatizo makubwa na uwezo wa baadhi ya mawaziri wetu.
 
Tatizo hawa Mawazir wetu wengi wao wanapewa Wizara wasizo na taaluma zao, tunapeana wizara kwa kujuana tu. Nadhani kunahaja ya kuchaguwa waziri awekwe kwenye wizara ya taaluma yake hii kwakweli itasaidia sana tu man atajua shid n raha za wizara yake kwa undani zaidi na atakuwa radhi kushughulikia matatizo ya wizara yake kwa haraka zaidi maana machungu yake anayajua pia. Kweli safari ilio mbele yetu ni ngumu na hakuna rangi ambayo hatuta acha kuiona.
 
ndo mambo ya kuwa na mawaziri wa kuokota okota na kauli zao za hovyo hovyoo.huyu mama ni kweli ana kauli za kifedhuli sana,sasa waalimu waandamane kutaka ajiuzuru
 
Nilimsikia Naibu Waziri wa Elimu Mh Mwantumu Mahiza akiongea na wanafunzi wa ualimu kule Songea (source TBC Taifa jana jioni).
Aliulizwa kuhusu mishahara midogo wanayolipwa walimu. Alijibu kuwa wale wanafunzi wasioridhika ni mishahara ya ualimu watafute kozi nyingine ili wapate hizo kazi zinazolipa zaidi. Na pia hata wale walimu wasioridhika na mishahara pia watafute kazi nyingine na sio kufanya migomo, kwani hata wao (mawaziri nafikiri) wakigoma itakuwaje?

Nilisikitika mno na kauli ile na nilijiulizi hivi
Serikali na wananchi tunalalamika sana kuhusu uhaba wa waalimu na pia mishahara midogo wanayolipwa hawa wachache ukiacha na haki nyingi wanazonyimwa. Je huyu Naibu Waziri anapata wapi kiburi cha kuwaambia walimu watafute kazi nyingine zitakazo walipa?
Alisema walimu wananzia kulipwa kama laki mbili hivi ambazo hazijakatwa kodi. Je huyu Naibu Waziri ameshafanya kautafiti kuona kuwa hiyo inawatosha kuwafanya wasilalamike?
Huyu ni Naibu Waziri wa ELIMU ambaye tunamtegemea asimamie vizuri Elimu yetu wa Tanzania iliyojaa matatizo. Badala ya kuwapa moyo walimu wanaoumia kwa kulitumikia Taifa kwa kujitolea, angalau kwa kuwaahidi kushughulikia matatizo ya Elimu, sasa anaongea kama mtu wa kijiweni.
Sijui CV ya huyu Naibu lakini nafikiri tunamatatizo makubwa na uwezo wa baadhi ya mawaziri wetu.

Jamani tundondosheeni CV ya huyu mama. She is too avarage to the post!!!! Au alisoma vile vyuo vyenye utata!!! Si yeye yule alisema wanaume watakaowapa wanafunzi mimba wakatwe uume??? Hili siyo solution ya tatizo!!! Yaani hawezi hata dakika moja kukaa chini kutafakari majibu yake!!! Hii ndiyo mojawapo ya team ya awamu ya nne!!! Tutafika for the next 6 years to come??? Kuna fadhila gani hapa inalipwa kwa huyu mother!!!!!
 
ni mbunge wa viti maalumu toka tanga anategemea kugombea ubunge jimbo la mkinga hapo tanga kitaaluma ana cheti cha ualimu daraja la tatu katika elimu ya watu wenye mahitaji maalumu(walemavu) lakini hadi kufika hapo alipo ni chakula ya wazito muda mrefu.
 
Jamani tundondosheeni CV ya huyu mama. She is too avarage to the post!!!! Au alisoma vile vyuo vyenye utata!!! Si yeye yule alisema wanaume watakaowapa wanafunzi mimba wakatwe uume??? Hili siyo solution ya tatizo!!! Yaani hawezi hata dakika moja kukaa chini kutafakari majibu yake!!! Hii ndiyo mojawapo ya team ya awamu ya nne!!! Tutafika for the next 6 years to come??? Kuna fadhila gani hapa inalipwa kwa huyu mother!!!!!

wiki mbili zilizopita alisema:


Waziri aomba uume wa mwalimu aliyemjaza mimba mwanafunzi usifanye kazi
broken-heart.jpg
Na Juddy Ngonyani, Sumbawanga

NAIBU Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Mwantumu Mahiza amewataka wananchi wa kijiji cha Muze wilaya ya Sumbawanga mkoani Rukwa kumuombea dua mbaya aliyekuwa mwalimu wa shule ya sekondari Mazoka aliyempa mimba mwanafunzi wa kidato cha tatu katika shule hiyo.

Mahiza alisema taarifa ya shule ilimsikitisha na baadhi ya matatizo yaliyoainishwa yatashughulikiwa na serikali.

" Na hili la huyu bazazi, aliyemkatisha masomo mwanafunzi ni lazima tumuombee dua ili asisimame daima,uume wake uache kufanya kazi" alisema.

Alisema mwalimu ndiye kioo cha jamii, lakini mwalimu anapomkatisha masomo mwanafunzi ni lazima achukuliwe hatua kali za kisheria na kinidhamu na kwamba kwa vile alitoroka dua limfuate huko aliko.

Awali akitoa taarifa ya shule hiyo mkuu wa shule hiyo Anicent Mpemba alisema katika kipindi cha miaka mitatu hadi hivi sasa wanafunzi wanne wa kike walikatishwa masomo yao kutokana na ujauzito.

Hata hivyo wanaume watatu walikamatwa kwa tuhuma za kutunga mimba hizo, lakini mwanaume wa nne alitoroka. Mpemba alisema mwalimu huyo baada ya kupatikana na hatia alifanikiwa kutoroka kabla ya kukamatwa na juhudi za kumtafuta bado zinaendelea kwa lengo la kumfikisha katika vyombo vya sheria.
 
ni mbunge wa viti maalumu toka tanga anategemea kugombea ubunge jimbo la mkinga hapo tanga kitaaluma ana cheti cha ualimu daraja la tatu katika elimu ya watu wenye mahitaji maalumu(walemavu) lakini hadi kufika hapo alipo ni chakula ya wazito muda mrefu.

Akikabiliwa na hali ngumu huwa anakuwa hana majibu kwani huishia kulia.

http://nukta77.blogspot.com/2009/05/hili-ndilo-jengo-la-shule-ya-kutoa.html
Pichani ni Bweni la shue ya Sekondari Zingibari huko Mkinga linalohifadhi wanafunzi 25.
Alipolitembelea ghafla, Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi bi Mwantumu Mahiza hakuweza kujizuia kutodondosha machozi.
 
Mwantumu na mama Kikwete walifundisha pamoja Mbuyuni Primary School na pia alikuwa mwalimu wa michezo. Mwisho alikuwa headmistress wa JK Nyerere Nursery ya kina Ulimwengu
 
Anatutia kichefuchefu.
Tatizo ni hii sirikali yetu ya kubebana na kuleleyana
 
Mwantumu na mama Kikwete walifundisha pamoja Mbuyuni Primary School na pia alikuwa mwalimu wa michezo. Mwisho alikuwa headmistress wa JK Nyerere Nursery ya kina Ulimwengu
CV yake hiyo hapo
GENERAL
Salutation Honourable Member picture
mpcv.php


First Name: Mwantumu
Middle Name: Bakari
Last Name: Mahiza
Member Type: Special Seat
Constituent: No Constituency
Political Party: CHAMA CHA MAPINDUZI
Office Location: P.O.Box 9121, Dar es Salaam
Office Phone: +255 754 372918
Ext.:
Office Fax:
Office E-mail: mmahiza@parliament.go.tz

Member Status: Current Member
Start Date: 28 December 2005
End Date: 30 August 2010
Date of Birth 12 August 1954
EDUCATIONS
School Name/Location Course/Degree/Award Start Date End Date Level
Chang'ombe Teaching Training College Diploma 1986 1987 DIPLOMA
Korogwe Teaching Training College Certificate 1971 1972 CERTIFICATE
University of Oslo - Norway Teaching Course 1990 1990 DIPLOMA
Jerusalem College - Israel Curriculum Development Course 1997 1997 DIPLOMA
Beit Bel Teaching College - Israel Teaching College 1999 1999 DIPLOMA
EDEPA University College - New Delhi, India Diploma in Teaching, Admin & Management 2000 2000 DIPLOMA
Korogwe Secondary Secondary School Secondary Education 1967 1970 SECONDARY
Zingibari Primary School Primary Education 1962 1966 CERTIFICATE
CERTIFICATIONS
Certification Name or Type Certification No. Issued Expires
No items on list

EMPLOYMENT HISTORY
Company Name Position From Date To Date
Ministry of Education & Vocational Training Deputy Minister 2006
Primary School HeadTeachers' Union Chairperson (East Africa) 2005 2008
Primary School HeadTeachers' Union Chairperson (Dar es Salaam ) 2003 2005
Mwl. Julius K. Nyerere Primary School HeadTeacher 1997 2005
Agha Khan Primary School Sports Teacher 1993 1996
Netball Regional Party - Dsm Chairperson 1986 1993
Dar es Salaam City Teacher 1976 1993
Tanga Municipal Teacher 1972 1976
POLITICAL EXPERIENCE
Ministry/Political Party/Location Position From To
Chama Cha Mapinduzi - CCM Chairman of Economic Committee Kawe Branch 2001 2005
PUBLICATIONS
Description Published Date
No items on list

SPECIAL SKILLS
Skill Name or Description Years Experience Acquired Through Skill Level
No items on list

RECOGNITIONS
Recognition Type Recognition Date Reason Action Taken Issued by
No items on list


Source: http://www.bunge.go.tz/bunge/mpcv.php?vpkey=321
 
Nakumbuka Mheshimiwa akiwahi kuwa mwalimu. Kama yeye aliweza kuacha kazi na kuingia kwenye siasa ni wazi kuwa wako walimu wengi sana wana uwezo huo tena wa kuwa wanasiasa wazuri kuliko yeye. Kabla ya kutoa kauli hii pengine, ooh no ni lazima alipaswa kufikiria kama kweli walimu wote wataacha kazi nini basi utakuwa mustakabali wa taifa? Japo hakutamka bayana lakini kwakuwa ndo kazi aliyochagua baada ya kuacha ualimu bila shaka ndo inayolipa. Mheshimiwa sasa anaweza kusimama mbele ya umma na kutuambia kupitia hiyo kazi inayolipa taifa limefaidika vipi zaidi kauli zake kejeli? Anatufundisha nini hapa kwamba ukiwa na kazi inayolipa wajibu wako ni kukejeli wanaolalahoi kwa kulitumikia taifa hili? Halafu anajaribu kutuaminisha kwamba kunasiku mawaziri wanaweza kufikiria kugoma, thubutu! kwa lipi hasa? Aaaaaghrrrr kwa kweli bado sijamwelewa mahiza. Aliyemwelewa tafadhali anisaidie
 
Inawezekana kuwa ndio sifa iliyompa Ubunge na hatimaye uwaziri?

That's obviously! Yeye na Salma Kikwete ni mashoga toka enzi na walicheza pamoja netball so lazima "shemeji" ampe pande kwenye cabinet
 
Last edited:
Back
Top Bottom