VIKWAZO
JF-Expert Member
- Apr 9, 2011
- 1,899
- 580
HALMASHAURI ya Manispaa ya Sumbawanga, mkoani Rukwa imekubali walimu wake 40 kwenda likizo baada ya kushindwa kuwalipa walimu wapya 40 wa shule za sekondari za Serikali zaidi ya Sh milioni 60.
Hizo ni fedha za malimbikizo ya mishahara yao kwa miezi minne iliyopita wanayoidai manispaa hiyo.
Tayari walimu hao wameuomba uongozi wa manispaa hiyo kuwaruhusu kurudi nyumbani na kwamba watakuwa tayari kurudi pindi halmashauri itakapokuwa na uwezo kifedha.
Walimu hao ambao wanatoka mikoa mbalimbali nchini wanadai kuwa hawajalipwa mishahara yao tangu mwezi Januari mwaka huu walipoajiriwa na halmashauri hiyo na kuanza kazi kwenye vituo vyao vipya.
Kwa mujibu wa walimu hao ambao walikuwa wamekusanyika kwenye ofisi za halmashauri hiyo jana mchana, kwamba Kaimu Mkurugenzi James Biseko amewataka kila mmoja wao amwandikie barua Mkuu wake wa Shule ya kuomba ruhusa kurudi walikotoka kwa kuwa
halmashauri hiyo haina uwezo wa kuwalipa mishahara yao wanayodai kwa sasa.
Tangu halmashauri hii ituajiri Januari mwaka huu hadi hii leo hatujalipwa mishahara yetu. Leo (jana) tumekutana na Kaimu Mkurugenzi huyo wa Manispaa hapa ofisini kwake tukampatia mapendekezo yetu mawili,......watulipe malimbikizo ya mishahara yetu yote ya miezi minne tunayodai, lakini amedai kuwa hilo haliwezekani kwa kuwa eti halmashauri haina pesa ya kutulipa.
"Basi tukamwambia (Kaimu Mkurugenzi) kwa kuwa hana pesa za kutulipa mishahara yetu yote kwa sasa atuwezeshe na atupe ruhusa turudi kwetu tulikotoka hadi hapo watakapokuwa na uwezo wa kutulipa ...ndipo Kaimu Mkurugenzi huyo alipokubali kutupatia ruksa hiyo ila kwa sharti kuwa kila mmoja wetu aandike barua yake binafsi akiomba ruhusa kwa Mkuu wa Shule tunakofundisha, alisema mmoja wa walimu hao aliyejitambulisha kama Clever Moses.
Kwa mujibu wa walimu hao wamekataa kuendelea kukopeshwa kiasi cha Sh 100,000 na Manispaa hiyo, ili wajikimu kimaisha hadi pale itakapokuwa na uwezo wa kuwalipa malimbikizo hayo ya mishahara yao wanayodai.
Tumekuja hapa kwa hiari yetu kama wahitimu wa Chuo Kikuu ngazi ya mshahara kwa mwezi ni Sh 400,000, sisi tumeajiriwa na halmashauri hii na tayari tumeanza kufundisha kwenye vituo vyetu vipya vya kazi tangu Januari mwaka huu hadi leo hii lakini hatuna mshahara.
Maisha kwetu ni magumu tuna madeni lukuki, ikiwemo malipo ya kodi la pango huku tukiwa hatarini kufukuzwa kwenye nyumba ambazo tumepanga, alisema Fadhili Sanga, mmoja wa walimu hao wapya.
Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Sumbawanga, James Biseko alikiri kuwa halmashauri hiyo haina uwezo wa kifedha kwa sasa wa kulipa malimbikizo hayo ya mishahara ya walimu hao wanayodai.
"Ni kweli hawa walimu ni waajiriwa wetu tangu Januari mwaka huu....tumekuwa tukiwakopesha Sh 100,000- siku zilizopita ili wajikimu, lakini mpaka sasa hatuna hiyo pesa ya
kuwalipa. Sasa kama hatuna mie nifanyeje sina la kufanya....mshahara wa mwalimu mpya kwa mwezi baada ya makato yote ni Sh 380,000.
habari leo
MAONI: ni lini serikali itakili kufulia na kupunguza matumizi yake ili kuleta unafuu kidogo kwa wafanyakazi wake wa chini walau kuwalipa mishahara
Hizo ni fedha za malimbikizo ya mishahara yao kwa miezi minne iliyopita wanayoidai manispaa hiyo.
Tayari walimu hao wameuomba uongozi wa manispaa hiyo kuwaruhusu kurudi nyumbani na kwamba watakuwa tayari kurudi pindi halmashauri itakapokuwa na uwezo kifedha.
Walimu hao ambao wanatoka mikoa mbalimbali nchini wanadai kuwa hawajalipwa mishahara yao tangu mwezi Januari mwaka huu walipoajiriwa na halmashauri hiyo na kuanza kazi kwenye vituo vyao vipya.
Kwa mujibu wa walimu hao ambao walikuwa wamekusanyika kwenye ofisi za halmashauri hiyo jana mchana, kwamba Kaimu Mkurugenzi James Biseko amewataka kila mmoja wao amwandikie barua Mkuu wake wa Shule ya kuomba ruhusa kurudi walikotoka kwa kuwa
halmashauri hiyo haina uwezo wa kuwalipa mishahara yao wanayodai kwa sasa.
Tangu halmashauri hii ituajiri Januari mwaka huu hadi hii leo hatujalipwa mishahara yetu. Leo (jana) tumekutana na Kaimu Mkurugenzi huyo wa Manispaa hapa ofisini kwake tukampatia mapendekezo yetu mawili,......watulipe malimbikizo ya mishahara yetu yote ya miezi minne tunayodai, lakini amedai kuwa hilo haliwezekani kwa kuwa eti halmashauri haina pesa ya kutulipa.
"Basi tukamwambia (Kaimu Mkurugenzi) kwa kuwa hana pesa za kutulipa mishahara yetu yote kwa sasa atuwezeshe na atupe ruhusa turudi kwetu tulikotoka hadi hapo watakapokuwa na uwezo wa kutulipa ...ndipo Kaimu Mkurugenzi huyo alipokubali kutupatia ruksa hiyo ila kwa sharti kuwa kila mmoja wetu aandike barua yake binafsi akiomba ruhusa kwa Mkuu wa Shule tunakofundisha, alisema mmoja wa walimu hao aliyejitambulisha kama Clever Moses.
Kwa mujibu wa walimu hao wamekataa kuendelea kukopeshwa kiasi cha Sh 100,000 na Manispaa hiyo, ili wajikimu kimaisha hadi pale itakapokuwa na uwezo wa kuwalipa malimbikizo hayo ya mishahara yao wanayodai.
Tumekuja hapa kwa hiari yetu kama wahitimu wa Chuo Kikuu ngazi ya mshahara kwa mwezi ni Sh 400,000, sisi tumeajiriwa na halmashauri hii na tayari tumeanza kufundisha kwenye vituo vyetu vipya vya kazi tangu Januari mwaka huu hadi leo hii lakini hatuna mshahara.
Maisha kwetu ni magumu tuna madeni lukuki, ikiwemo malipo ya kodi la pango huku tukiwa hatarini kufukuzwa kwenye nyumba ambazo tumepanga, alisema Fadhili Sanga, mmoja wa walimu hao wapya.
Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Sumbawanga, James Biseko alikiri kuwa halmashauri hiyo haina uwezo wa kifedha kwa sasa wa kulipa malimbikizo hayo ya mishahara ya walimu hao wanayodai.
"Ni kweli hawa walimu ni waajiriwa wetu tangu Januari mwaka huu....tumekuwa tukiwakopesha Sh 100,000- siku zilizopita ili wajikimu, lakini mpaka sasa hatuna hiyo pesa ya
kuwalipa. Sasa kama hatuna mie nifanyeje sina la kufanya....mshahara wa mwalimu mpya kwa mwezi baada ya makato yote ni Sh 380,000.
habari leo
MAONI: ni lini serikali itakili kufulia na kupunguza matumizi yake ili kuleta unafuu kidogo kwa wafanyakazi wake wa chini walau kuwalipa mishahara