Click_and_go
JF-Expert Member
- Nov 21, 2010
- 451
- 5
DEMOKRASIA inayo mantiki yake ambayo si lazima iwe na tafsiri maarufu ya nchi za Magharibi, kwa kuwa lengo la utawala kwa watawala na watawaliwa mahali popote ni manufaa ambayo watawaliwa wanayatarajia.
Katika nchi za Magharibi, tafsiri maarufu ni ya Abraham Lincoln, Rais wa 16 wa Marekani (Februari 12, 1809 Aprili 15, 1865) aliyesema kuwa demokrasia ni serikali ya watu, iliyoundwa na watu, kwa ajili ya watu.
Hata hivyo maana ya demokrasia kwa watu hao wa Magharibi, haikuwa serikali ya watu, inayotokana na historia yao, hatua yao ya maendeleo ya kijamii na malengo yao.
Kwa kiasi kikubwa tafsiri hiyo ya Magharibi ililenga kuficha walichokusudia, ambacho ni mfumo wa Magharibi kwa ajili ya kuwarithisha watu hata wasio wa Magharibi lakini kwa maslahi ya watu wa Magharibi.
Katika historia ya maendeleo ya binadamu, ambayo kwa kiwango kikubwa iliyowekwa katika
kumbukumbu ni ya watu hao wa Magharibi, demokrasia ilikuwepo na ikabadilika kutokana na historia yao, hatua yao ya maendeleo ya kijamii na malengo yao.
Ndivyo ilivyo kwa Libya, inayo demokrasia ambayo haina maana ni demokrasia isiyobadilika, lakini ni demokrasia iliyopo kwa kiwango cha maendeleo cha nchi hiyo, kilichosababisha kukubalika kwa serikali yake na watu wake,,,,,soma zaidi HabariLeo | Walibya watamkumbuka Gaddafi
Katika nchi za Magharibi, tafsiri maarufu ni ya Abraham Lincoln, Rais wa 16 wa Marekani (Februari 12, 1809 Aprili 15, 1865) aliyesema kuwa demokrasia ni serikali ya watu, iliyoundwa na watu, kwa ajili ya watu.
Hata hivyo maana ya demokrasia kwa watu hao wa Magharibi, haikuwa serikali ya watu, inayotokana na historia yao, hatua yao ya maendeleo ya kijamii na malengo yao.
Kwa kiasi kikubwa tafsiri hiyo ya Magharibi ililenga kuficha walichokusudia, ambacho ni mfumo wa Magharibi kwa ajili ya kuwarithisha watu hata wasio wa Magharibi lakini kwa maslahi ya watu wa Magharibi.
Katika historia ya maendeleo ya binadamu, ambayo kwa kiwango kikubwa iliyowekwa katika
kumbukumbu ni ya watu hao wa Magharibi, demokrasia ilikuwepo na ikabadilika kutokana na historia yao, hatua yao ya maendeleo ya kijamii na malengo yao.
Ndivyo ilivyo kwa Libya, inayo demokrasia ambayo haina maana ni demokrasia isiyobadilika, lakini ni demokrasia iliyopo kwa kiwango cha maendeleo cha nchi hiyo, kilichosababisha kukubalika kwa serikali yake na watu wake,,,,,soma zaidi HabariLeo | Walibya watamkumbuka Gaddafi