Walibya watamkumbuka gaddafi

watu bwana, eti wanasoma magazeti waandishi weneywe vilaza, umepata kukutana na walibya? walioko nje ya libya jinsi wanavyo msema Gadafi? Gdafi ni dictator, ila wasiojua wanamwona malaika, ni kama kagame na museveni.......WAO WENYEWE WANAANDAMANA LEO HII MTANZANIA ANASEMA WATAMKUMBUKA, nacheka mie!
 
upuuzi mtupu.

kwanza habari yenyewe umetoka habari leo

pili: yeye (gaddafi) ni nani hata atawale nchi zaidi ya miaka 40? wengine hawawezi?

:rain::rain:...ebwana we uko juu! inaonekana una busara kama za Sulemani!!! yani una point za ukweli! Na maneno yako yanaonekana yanatoka kwenye kinywa cha juha wa hali ya juu!!! na inaonekana yanatoka kwenye chemchem ya pumba na shudu ambazo hata kuku hawawezi kula! HONGERA BOSS!!!! KEEP IT UP!!:rain::rain:
 
Mkuu Ng'wanangwa ameweka source ya aliko-quote hivyo kwa kua hajaongeza neno yeye awe mjumbe tu! Ila kwa upande mwingine kuna kaukweli ndani yake kwamba tawala dhalimu kwa wazawa ila zenye maslahi kwa mataifa ya magharibi ni halali kwao ila tawala halali kwa wazawa na zinazokinzana na matakwa ya wa-magaharibi basi ni haramu na za kigaidi...kuna somo la kujifunza hapa!
 
Hakuna tunu kubwa duniani kama freedom. Watu wengi wamepigana maisha yao yote mamilioni wamepoteza maisha kwa kupigania freedom. Libya inaweza kuwa na maendeleo na maisha mazuri lakini hakuna freedom.. maisha mazuri bila freedom hayana maana. Ni sawa na nyerere alivyosema 'ni afadhali maskini huru kuliko tajiri mtumwa"

Nakubaliana na wewe kabisa. Kwa kuwajibu walioleta hoja ya tasfiri ya demokrasia, ni kweli tafsiri ya demokrasia ni tofauti lakini kiongozi anayewafunga midomo watu wake, kujilimbikizia mali yeye na familia yake (ambao ndio wanapata nafasi muhimu na mikataba mikubwa), pamoja na kufadhili ugaidi (Lockerbie bombing) huyo unamtathmini vipi? Mafanikio ya Libya kiuchumi hayatokani na sera zozote nzuri za siasa za Gadafi ni utajiri wa mafuta. Na ndio maana kwa sasa Gafadi ana uwezo wa kulipa hao askari wa kupikwa $300 ( dola mia tatu) kwa siku kuwaua walibya wenzake.
 
Back
Top Bottom