- Mchele nusu kilo
- Karot 1 kubwa (ipare vizuri)
- Nyanya 3 kubwa
- Vitunguu maji viwili (ukubwa kiasi)
- Bizari ya pilau, curry powder, binzari ya njano na mdalasini 1/2 teaspoon kila kimoja
- Mafuta kiasi
- Mchanganyiko wa mboga, mfano njegere na mahindi machanga (ila hii sio lazima)
- Chumvi kiasi
- Mboga ya spinachi (fungu 1)
- Saumu na tangawizi ya kusaga (1 teaspoon)
Namna ya kutayarisha
Loweka mchele kwa dakika 20.
Weka mafuta katika sufuria, kaanga kitunguu maji hadi karibia kuwa brown
Weka spices zote
Weka tangawizi na saumu
Tia karoti yako uliopara pamoja na vegetable nyengine
Mimina nyanya pamoja na mboga ya spinachi
Koroga hadi wiiwe kiasi
Mimina mchele, weka chumvi na maji ya moto kidogo
Funika punguza moto ili chakula kisiungue
Subiria hadi kuwiva
Andaa tayari kwa kuliwa