Lomwe ni maarufu sana kwa sababu ya Headmaster Kangero. Kielimu mpaka sasa Lomwe inatisha kielimu wilayani Mwanga. Kangero huenda akawa ni Headmaster wa kwanza hapa Tanzania kuwa kwenye shule moja kwa miaka mingi sana. Huenda ni zaidi ya miaka 30. Mpaka sasa ni Headmaster wa Lomwe. He is man of Discipline. Ni kama Ferguson na Mancheter united, au Mugabe na Zimbabwe au Seiph Blatter na Fifa. Shule zingine kama Shighatini,Minja na Kiriki zimefifia sana kielimu, huenda wakati wowote zikafungwa maana idadi ya wanafunzi wanaosoma hapo ni ndogo sana. Migogoro ya kidini, ujio wa shule nyingi za kata na uongozi mbovu wa shule hizo za Shighatini, Mruma na Kiriki unapelekea kufa kwa shule hizo.