Wale waliopata scholarship na sponsors za kusoma Ulaya na US e.t.c tiririkeni hapa!!!

Humble African

JF-Expert Member
Jul 28, 2013
4,779
14,311
Binafsi nimehitimu shahada yangu ya kwanza mwaka 2012 na kupata ufaulu murua tu wa upper second, ila hadi sasa nafanya shughuli zangu za kawaida tu kutokana na ugumu wa kupata ajira kutokana na elimu yangu.

Ila binafsi nina miaka 26, naamini bado kijana sana na ninahisi nina appetite na morali wa kutaka kuendelea na hatua ya masters. nimesikia mara kadhaa kuhusu udhamini wa masomo ughaibuni lakini hadi sasa sijakutana na waliopata bahati hiyo hili na mimi niweze kusurvive na maneno mawili matatu kutoka kwao juu ya kipi muhimu kuwa nacho? na mengineyo muhimu.

karibuni wandugu tujadili na kutafakari pamoja!!

asanteni.
 
Back
Top Bottom